TEMESA TANGA YAZIDAI TAASISI ZA SERIKALI MADENI ZAIDI YA BILIONI 1.8 ,YAMO MADENI SUGU




Na Oscar Assenga,TANGA.

WAKALA wa Ufundi na Umeme nchini (TEMESA) Mkoani Tanga umesema kwamba unazidai Taasisi za Serikali madeni sugu ya zaidi ya Bilioni 1.8 ambao walikwenda kutengeneza magari yao katika karakana ya wakala huo ambapo mengine ni ya muda mrefu.

Hayo yalisemwa na Meneja wa Temesa Mkoa wa Tanga Mhandisi Jairos Nkoroka wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake ambapo alisema wanaziomba taasisi hizo kulipa madeni yao ili kuuwezesha wakala huo kuendelea kutekeleza shughuli zao kwa ufanisi.

Meneja huyo aliziomba taasisi hizo nazo ziweze kulipa madeni yao kutokana na kwamba nao pia wanadaiwa Bilioni 1.4 na wazabuni ambao wamekuwa wakipeleka vifaa kwa ajili ya kutengeneza magari

“Tunawakumbusha watulipe ili tuweze kuendelea kuwapa huduma kwani kutokufanya hivyo kunaweza kusababisha kutokupata huduma kwa wakati “Alisema

Aidha alisema kwamba madeni mengi ni ya nyuma ambayo wameyarithi na mengine wameyapeleka makao makuu yao kwa utaratibu mwengine na ya mwaka huu wanaendelea kuwadai kuhakikisha wanalipa

“Tumeanzia kitengo cha mahusiano kupitia mabalozi kwa kujenga mahusiano na hivyo kuzaidia wanaodaiwa kuanza kulipa madeni yao na tunaamini tutaendelea kupata mafanikio”Alisema

Aidha alisema ili kuweza kukabiliana na wadai hao sugu Temesa umeingia mkataba na wazabuni wakubwa (40) wa vipuri vya magari mkoani Tanga ili kuondoa ucheleweshaji ambao ulikuwepo hapo awali badala ya kuanza taratibu za manunuzi ambazo siku za nyuma zilikuwa zinawachelewesha.

Alisema wameamua kufanya hivyo ili kuweza kuhakikisha wanaondokana na ucheleweshwaji huo na kwa sasa wanachukua muda mfupi baada ya siku mbili.

Alisema mpango huo utasaidia kuwawezesha kupata vifaa ambavyo walikuwa hawana na vile vyengine ambavyo kwa hiyo kwa sasa ivi magari ya serikali yanayokwenda kufanyiwa matengenezo yanachukua muda mfupi sana na hatimaye kuruhusiwa kuendelea na shughuli zao.

“Hivi sasa tumeingia mikataba na wazabuni wakubwa na matengenezo ya magari ya Serikali yanatakiwa kutengenezwa na Temesa na tukishindwa kutengeneza kutokana na kitaaluma au vifaa kuna utaratibu ambao unafahamika na tunatoa vibali kwenda kwenye karakana nyengine na yanatrngezwa chini ya usimamizi wao”Alisema

“Katika ishu ya vifaa vya matengenezo ya magari tunatumia muda mfupi kulikagua gari na kubaini changamoto zake kutokana na uwepo wa vifaa vya kisasa “Alisema Jairos

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments