MELI TANO ZA WATALII ZATIA NANGA BANDARI YA KILWA MWEZI FEBRUARI
Thursday, February 15, 2024
Mwaka 2024 umeanza kwa rekodi ya ufanisi wa hali ya juu katika kupokea Watalii wanaotumia Bandari ya Kilwa ambapo kwa Mwezi Februari pekee, Meli tano za Watalii zimetia nanga Bandarini hapo na kuhudumiwa.
Bandari ya Kilwa iliyopo Kilwa Masoko Mkoani Lindi, imeendelea kuwa kivutio kikubwa kwa Watalii kutoka Mataifa mbalimbali ambao wanaendelea kuwasili Nchini kujionea vituo vya Utalii.
Meli ya Watalii ya BOUGAINVILLE ambayo ni Meli ya tano kutia nanga Bandarini hapo, imewasili ikiwa na Watalii 133.
Tangu kuanza kuwasili kwa Meli hizo, jumla ya Watalii 593 Wametembelea Vivutio vya Utalii kwa mafanikio na kusifu huduma za Meli zinazotolewa na Wataalamu Wazawa wa TPA ambao wameonesha Weledi na umahiri mkubwa katika majukumu yao ya kuhudumia Meli hizo za Watalii.
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin