KAZI 529 ZAPOKELEWA KUWANIA TUZO ZA UMAHIRI ZA UANDISHI WA HABARI ZA TAKWIMU ZA WANAWAKE NA UONGOZI

JUMLA ya kazi 529 za waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari zimewasilishwa kwa ajili ya kuwania tuzo za umahiri za uandishi wa habari za takwimu za wanawake na uongozi.

Miongoni mwa kazi hizo ni pamoja na vipindi vya redio, televisheni, makala za magazeti na zile kutoka katika mitandao ya kijamii zilizoandikwa na kurushwa katika vyombo vyao kuanzia mwezi Janauari hadi Disemba 31, 2023.

Kazi hizo zinaonesha ni jinsi gani waandishi wamekuza mwamko wa kuandika habari za uongozi kwa wanawake ambapo zinashajihisha wanawake na vijana wakike kujiamini zaidi na kuwa na matumaini ya kupata nafasi mbali mbali za uongozi lakini pia zinaielimisha jamii kuhusu umuhimu wa wanawake katika uongozi.

Lengo la tuzo hizo ni kuhimiza waandishi wa habari kutumia kalamu zao na vyombo vya habari kuelimisha umma kuhusu umuhimu wa masuala ya wanawake katika uongozi na hivyo kuongeza ushiriki wa wanawake katika nafasi mbalimbali za maamuzi.

Hii ni mara ya tatu kwa tunzo hizo kufanyika hapa Zanzibar na kwa mwaka huu zinatarajiwa kufanyika mapema mwezi Machi, 2024.

Tuzo za umahiri za uandishi wa habari za takwimu za wanawake na uongozi zinaandaliwa kwa pamoja na  Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania Zanzibar, (TAMWA – ZNZ),  Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA), Jumuiya inayojihusisha na Mazingira, Usawa wa Kijinsia, na Utetezi Pemba (PEGAO), kwa kushirikiana na Ubalozi wa Norway nchini Tanzania.

Dkt. Mzuri Issa,

Mkurugenzi,
TAMWA ZNZ.


====================================================================

PRESS RELEASE:

529 works are being submitted for data journalism excellence awards

for women's leadership.

A total of 529 works of journalists from various media outlets have been submitted for consideration in the competition for data journalism excellence awards for women's leadership reporting.

Among these works are radio and television programs, newspaper articles, and content from social media platforms, all produced and broadcasted by their respective organizations from 1st of January to December 31, 2023.

These works show how journalists have elevated the awareness of reporting on women's leadership, encouraging women and young girls to be more self-confident and hopeful about obtaining various leadership positions. Additionally, they also serve to educate the community on the significance of women in leadership roles.

The aim of these awards is to encourage journalists to use their pens and media platforms to educate the public about the importance of women's issues in leadership, thereby promoting increased women participation in various decision-making positions.

This marks the third occasion for these awards to take place in Zanzibar, and they are expected to be held in early March 2024.

The data journalism excellence awards for women's leadership reporting is jointly organized by the Tanzania Media Women’s Association, Zanzibar (TAMWA-ZNZ), Zanzibar Female Lawyers Association (ZAFELA), the Association for Environment, Gender Equality, and Advocacy in Pemba (PEGAO), in collaboration with the Royal Norwegian Embassy in Tanzania.

Dr. Mzuri Issa, 

Director,

TAMWA ZNZ.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post