DKT. NCHIMBI AZUNGUMZA NA VIONGOZI MBALIMBALI WA CCM DODOMA

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, akizungumza na watumishi wa CCM Makao Makuu pamoja na jumuiya zake, Jumuiya ya Wazazi, Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), kwenye Ukumbi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC), Dodoma, Jumanne, Februari 6, 2024. Wengine meza kuu, ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM - Bara, Ndugu Anamringi Issay Macha na Katibu wa NEC, Fedha na Uchumi, Dkt. Frank George Haule Hawasi.
Baadhi ya Watumishi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Makao Makuu, pamoja na jumuiya zake, Umoja wa Wazazi, Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), wakimsikikiza na kufuatilia kwa makini hotuba ya Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, wakati wa kikao na watumishi hao, katika Ukumbi wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), jijini Dodoma, Jumanne, Februari 6, 2024.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post