UHAMIAJI SHINYANGA WATOA ELIMU MASUALA YA UHAMIAJI MAADHIMISHO YA WIKI YA SHERIA


Naibu Afisa Uhamiaji Mkoa wa Shinyanga, Mrakibu wa Uhamiaji Lydia Angumbwike (kulia) akimwelezea Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme kuhusu huduma zinazotolewa na Jeshi la Uhamiaji alipotembelea Banda la Uhamiaji wakati wa uzinduzi wa Wiki ya Sheria Mkoa wa Shinyanga leo Jumamosi Januari 27,2024 katika Uwanja wa Zimamoto Mjini Shinyanga.

Jeshi la Uhamiaji Mkoa wa Shinyanga linashiriki Maadhimisho ya Wiki ya Sheria Mkoa wa Shinyanga kwa kutoa elimu kwa wananchi juu ya huduma wanazotoa ikiwemo Utoaji Pasipoti, Vibali vya Ukaazi, Vibali vya kuingia nchini (Visa),kudhibiti uhamiaji haramu, kuendesha kesi za uhamiaji haramu pamoja na kupokea maombi ya uraia.

PICHA na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post