BENKI YA NMB INATOA MPAKA BILIONI 340 KWA WAWEKEZAJI WAKUBWA

Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Baraka Ladislaus akielezea fursa za benki hiyo wakati wa Kongamano la Uwekezaji wa Biashara na Utalii lililofanyika kwenye ukumbi wa Regail Naivera Jijini Tanga ambalo lilifunguliwa na Waziri wa Uwekezaji na Mipango Profesa Kitilya Mkumbo ambaye alimwakilisha Waziri Mkuu Kasim Majaliwa.
Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Baraka Ladislaus akielezea fursa za benki hiyo wakati wa Kongamano la Uwekezaji wa Biashara na Utalii lililofanyika kwenye ukumbi wa Regail Naivera Jijini Tanga ambalo lilifunguliwa na Waziri wa Uwekezaji na Mipango Profesa Kitilya Mkumbo ambaye alimwakilisha Waziri Mkuu Kasim Majaliwa.
Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Baraka Ladislaus akielezea fursa za benki hiyo wakati wa Kongamano la Uwekezaji wa Biashara na Utalii lililofanyika kwenye ukumbi wa Regail Naivera Jijini Tanga ambalo lililofunguliwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia Uwekezaji Profesa Kitilya Mkumbo ambaye alimwakilisha Waziri Mkuu Kasim Majaliwa 
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia Uwekezaji Profesa Kitilya Mkumbo ambaye alimwakilisha Waziri Mkuu Kasim Majaliwa katikati akiwa kwenye picha ya pamoja na Wadau mbalimbali wa maendeleo mkoani humo wakiwemo watumishi wa Benki ya NMB mara baada ya kufungua kongamano hilo
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia Uwekezaji Profesa Kitilya Mkumbo ambaye alimwakilisha Waziri Mkuu Kasim Majaliwa katikati akiwa kwenye picha ya pamoja na Wadau mbalimbali wa maendeleo mkoani humo wakiwemo watumishi wa Benki ya NMB mara baada ya kufungua kongamano hilo


Na Oscar Assenga,Tanga,

BENKI ya NMB imeshirikiki Kongamano la Uwekezaji wa Biashara na Utalii katika Mkoa wa Tanga huku wakibainisha kwamba kwa hivi sasa mwekezaji mkubwa anaweza kuchukua mkopo mpaka bilioni 340 kwa mkopaji mmoja.

Hayo yalibainishwa leo na Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Baraka Ladislaus wakati wa Kongamano la Uwekezaji wa Biashara na Utalii lililofanyika kwenye ukumbi wa Regail Naivera Jijini Tanga ambalo lilifunguliwa na Waziri wa Uwekezaji na Mipango Profesa Kitilya Mkumbo ambaye alimwakilisha Waziri Mkuu Kasim Majaliwa.

Alisema kwamba hivyo kupitia hilo wawekezaji wanaweza kuchangamkia fursa ya mikopo hiyo ili kuweza kujikwamua kiuchumi ambao utakuwa chachu ya kukuza pia mitaji yao na hatimaye kuweza kuchochea ukuaji wa biashara zao.

“Wenzetu wa Simba kama mtaji ni changamoto karibuni sana lakini uwekezaji huo wa Tanga hauwezi kuwezekana bila kuwa na upatikanaji wa huduma za kifedha na wana matawi ya benki zaidi ya 12 kwa wilaya zote nane na wilaya nyengine wana matawi mawili na hivyo hii ni kurahisisha upatikanaji wa huduma za kifedha tunazoziongelea”Alisema

Hata hivyo alisema kwamba benki hiyo wamejipanga vizuri na itaendelea kushirikiana na Serikali ili kuchangiza maendeleo muhimu kwa watanzania .

Meneja huyo wa Kanda aliwaeleza wawekezaji watanzania waliopo mkoani Tanga kwamba benki hiyo inajivunia kushiriki kwenye kongamano na wanataka kuwaambia wawekezaji wa Tanga kwamba inajivunia uwezo wake mkubwa kuwahudumia sekta mbalimbali za uwekezaji na wameanza kuhudumia sekta ya biashara za kati na wadogo kwa kuwa na muda mrefu wa kuwahudumia.

Hata hivyo alisema kwamba pia benki hiyo imeendelea kukuza mtaji wake na niwaambie wawekezaji kwamba benki ina uwezo mkubwa wa kutoa mitaji ambayo itachagiza uwekezaji ambao unaozungumziwa leo ambao umekuwa mkombozi kwao.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post