RC SIMIYU ATEMBELEA VIKUNDI VYA WAJASIRIAMALI 'VIJANA WAPAMBANAJI' BARIADI,...... AHIMIZA MAREJESHO KWA WAKATI KUJENGA UAMINIFU




Bariadi,

Vijana wajasiriamali  Mkoani Simiyu wamehimizwa  kufanya  marejesho ya mikopo inayotolewa na Serikali kwa wakati ili kujenga uaminifu jambo litakalowawezesha kuaminika na kukopeshwa fedha nyingi zaidi jambo  litakayosaidia kukuza mitaji yao na hivyo kujikwamua na umaskini.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Dkt Yahaya Nawanda alipotembelea kikundi Cha Vijana Wajasiriamali almaarufu "Vijana wapambanaji" kilichopo eneo la Stendi kuu ya Mabasi Somanda Wilayani Bariadi wanaojihusisha na shughuli za uchapaji mabango kwa lengo la kutatua Kero zao.

"Kwa uzoefu nilionao nikiwa DC  kwa miaka zaidi ya saba ni kuwa  vikundi vingi vya Vijana vina changamoto ya kutofanya marejesho kwa wakati tofauti na vikundi vya walemavu na wakina mama."Alisema mkuu wa Mkoa Dkt Nawanda. 

Aidha Mkuu wa Mkoa Dkt Nawanda amewapongeza Vijana wapambanaji kwa kuwa mfano mzuri katika kufanya marejesho ya mikopo waliyowezeshwa na Serikali kwa wakati na kuwataka Vijana wengine kuiga mfano.

Kikundi cha Wajasiriamali cha vijana wapambanaji ni moja kati ya Vikundi vya Wajasiriamali Wilayani Bariadi  vilivyonufaika na Mkopo wa Asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya kuwawezesha Vijana,akina Mama na wenye ulemavu.

www.simiyu.go.tz



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post