KATAMBI AWATAKA WAMILIKI WA SHULE BINAFSI KUWASILISHA MICHANGO YA NSSF KWA WAKATI




Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Patrobas Katambi amewataka wamiliki wa shule zisizo za serikali kuwasilisha michango ya wafanyakazi wao kwa wakati kwenye Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kwa mujibu wa sheria ili kuleta tija kazini.

Akizungumza Oktoba 10, 2023 jijini Dodoma kwenye kikao na wamiliki hao kilichoandaliwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Katambi amesema kumekuwa na malalamiko kuhusu suala la michango ya NSSF na kwamba kupitia kikao hicho serikali itawasikiliza na kutafutia ufumbuzi suala hilo.

Aidha, amewataka kutafutia ufumbuzi migogoro ya kikazi kwenye maeneo yao kwa kuzingatia Sheria ya Ajira na Mahusiano kazini ili shule zisiyumbe.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post