DKT. SHEKALAGE, DKT. JINGU WAKABIDHIANA OFISI RASMI


Na WMJJWM, DODOMA

Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Seif Shekhalage amewasili katika ofisi yake mpya na kukabidhiwa Ofisi hiyo na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara Dkt. John Jingu Leo Agosti 4,2023.

Tukio hilo ni kufuatia mabadiliko yaliyofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzanja Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan yaliyohusisha Baraza la Mawaziri na Makatibu Wakuu hivi karibuni.

Akizungumza na Menejimenti ya Wizara mara baada ya makabidhiano, Dkt. Shekhalage ametoa wito kwa watumishi wote kushirikiana ili kufikia lengo la kuwahudumia Wananchi.

"Nitakuwa tayari kupokea maelekezo ya Mhe. Waziri, niwahakikishie kuwa mimi nitakuwa mtumishi mwenzenu, tutafanya kazi kwa umoja na ushirikiano"

Kwa upande wake Dkt. Jingu ameishukuru Menejimenti na watumishi kwa ushirikiano waliompatia kwa kipindi chote alichofanya kazi Wizarani hapo.

Naye Waziri Mhe. Dkt Dorothy Gwajima akizungumza wakati wa hafla hiyo fupi, amesema lengo la Mheshimiwa Rais kufanya mabadiliko hayo ni jema ili kuendelea kuwatumikia watanzania.

Amemshukuru Dkt. Jingu kwa utendaji wake akiwa Wizarani hapo na kumtaka ashirikiane vozuri na Katibu Mkuu Dkt. Shekhalage katika utendaji kwani Wizara hizo zinategemeana.

"Wizara ya Maendeleo ya Jamii ikifanya vizuri kwenye Jamii,hata kwenye Hospitali zetu wagonjwa watapungua" amefafanua Waziri Dkt. Gwajima.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post