TAASISI YA TAWEN YATAMBULISHWA RASMI SHINYANGA



Na Marco Maduhu,SHINYANGA

TAASISI ya Tanzania Women Empowerment Network (TAWEN) ambayo inajihusisha na uwezeshaji wanawake na vijana kiuchumi hapa nchini Tanzania, imetambulishwa rasmi Mkoani Shinyanga.

Utambulisho huo umefanyika leo Septemba 11, 2023 katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, na kushuhudiwa na viongozi mbalimbali akiwemo Katibu Tawala wa Mkoa huo, Wakuu wa wilaya ya Kahama na Shinyanga na baadhi ya viongozi wa UWT Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Christina Mndeme (kulia) akiwa na Mwenyekiti wa Taasisi ya TAWEN Kanda ya Ziwa Neema Edward Mgobela.

Mwenyekiti wa Taasisi ya TAWEN Kanda ya Ziwa Neema Edward Mgobela ambaye pi ni Mwenyekiti wa UWT wilaya ya Ukerewe, amesema katika Mkoa wa Shinyanga hivi karibuni wanatarajia kuanzisha Tawi la Taasisi hiyo, ndiyo maana wameanza kwanza kuitambulisha kwa viongozi ili waifahamu.

“Taasisi yetu ya TAWEN inajihusisha na uwezeshaji wanawake na vijana kiuchumi, na hapa mkoani Shinyanga tunatarajia hivi karibuni kuanzisha Tawi na tutafanya uzinduzi,”amesema Neema.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Christina Mndeme (kulia) akiwa na Mwenyekiti wa Taasisi ya TAWEN Kanda ya Ziwa Neema Edward Mgobela.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Christina Mndeme, ameipongeza Taasisi hiyo pamoja na kuikaribisha mkoani humo, ili kufanya kazi ya kuinua wanawake na vijana kiuchumi.
Picha za pamoja zikipigwa na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.
Picha za pamoja zikiendelea kupigwa.
Picha za pamoja zikiendelea kupigwa na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga .
Picha zikipigwa na Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Johari Samizi.
Picha za pamoja zikipigwa na Mkuu wa wilaya ya Kahama Mboni Mhita.
Awali Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Prof; Siza Tumbo (kulia) akikabidhiwa Bahasha yenye utambulisho wa Taasisi ya TAWEN kutoka kwa Mwenyekiti wa Taasisi hiyo  Kanda ya Ziwa Neema Edward Mgobela.
Awali Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Prof; Siza Tumbo (kulia) akikabidhiwa Bahasha yenye utambulisho wa Taasisi ya TAWEN kutoka kwa Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Kanda ya Ziwa Neema Edward Mgobela.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Prof; Siza Tumbo (kulia) akipiga picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Taasisi ya TAWEN Kanda ya Ziwa Neema Edward Mgobela.
Picha za pamoja zikipigwa na Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Prof; Siza Tumbo.
Picha za pamoja zikiendelea kupigwa.
Picha za pamoja zikiendelea kupigwa.
Picha za pamoja zikiendelea kupigwa.
Picha za pamoja zikiendelea kupigwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post