CHATANDA ASHIRIKI MBIO ZA MWENGE WA UHURU..ATAKA WAZAZI KUONGEZA UMAKINI MALEZI YA WATOTO

Mwenyekiti wa UWT Taifa Ndg. Mary Chatanda ameshiriki mbio za Mwenge wa Uhuru Wilayani Mbarali Mkoani Mbeya.

Akizungumza leo katika Mkesha wa Mwenge wa Uhuru Wilayani Mbarali Mwenyekiti Chatanda amewataka wazazi na walezi wa watoto kuwa makini juu ya suala la maadili ambalo limekuwa ni changamoto kubwa katika Taifa letu.

"Ndugu wazazi wenzangu tuwe makini na vijana wetu kwani hali imekuwa mbaya dunia imeharibika tuongeze umakini kwenye suala la malezi ya watoto wetu", Chatanda amesema

UWT IMARA JESHI LA MAMA KAZI IENDELEE


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post