KAMISHINA JENERALI MADAWA YA KULEVYA NA MWANAMFALME WA ZULU AFRIKA KUSINI WATEMBELEA BANDA LA TMDA


Aretas Lyimo, Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya akisaini kitabu Cha wageni wakati alipotembelea Banda la Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania TMDA kwenye maonesho ya 47 ya biashara ya Kimataifa yanayoendelea kwenye viwanja vya Sabasaba Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam Kushoto ni Roberta Feruz Afia Mawasiliano Mwandamizi wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania TMDA
Roberta Feruz Afia Mawasiliano Mwandamizi wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania TMDA akitoa maelezo Kwa Aretas Lyimo, Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya. wakati alipotembelea Banda la Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania TMDA kwenye maonesho ya 47 ya biashara ya Kimataifa yanayoendelea kwenye viwanja vya Sabasaba Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.

Roberta Feruz Afia Mawasiliano Mwandamizi wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania TMDA akitoa maelezo Kwa wananchi mbalimbali waliotembelea Katika Banda Hilo.

Mwana wa Mfalme wa Zulu nchini Afrika ya Kusini Prince Bheki Zulu akimsikiliza Scholastica Njozi Afisa Uhusiano Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania TMDA wakati akimpa maelezo alipotembelea kwenye banda hilo katika maonesho ya 47 ya biashara ya Kimataifa yanayoendelea kwenye viwanja vya Sabasaba Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.
Mwana wa Mfalme wa Zulu nchini Afrika ya Kusini Prince Bheki Zulu akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Uhusiano Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania TMDA kushoto ni Martin Malima na kulia niScholastica Njozi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post