KAMPUNI YA JAMBO YAKABIDHI JEZI KWA TIMU YA SOKA YA WANAWAKE 'MWAMVA FDC QUEENS' MICHUANO YA WRCL JIJINI MWANZA

Mwakilishi wa Kampuni ya Jambo Food Products, Chrispin Kakwaya ambaye ni Mkuu wa Idara ya Michezo Jambo Media (kulia) akikabidhi jezi kwa ajili ya Timu ya Soka ya Wanawake Mwamva FDC Queens. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Timu ya Mwamva FDC Queens Mwalimu Aisa Mariki akifuatiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Soka mkoa wa Shinyanga (SHIREFA), Said Mankiligo na Nahodha wa Timu ya Mwamva FDC Queens, Mwajab Athuman.

Na Elizabeth Hassan & Kadama Malunde - Shinyanga
Kampuni ya Jambo Food Products imekabidhi Jezi seti mbili zenye thamani ya shilingi 500,000/= kwa Timu ya Soka ya Wanawake Mwamva FDC Queens ya Mjini Kahama mkoani Shinyanga ambayo inashiriki katika Ligi ya Mabingwa wa mikoa kwa wanawake (Women Region Competition League- WRCL)  jijini Mwanza.


Hafla hiyo imefanyika leo Julai 14, 2023 katika kiwanda cha Kampuni ya Jambo Food Products mjini Shinyanga ambapo mkurugenzi wa Timu ya Mabingwa wa Mkoa wa Shinyanga ya Wanawake 2023 'Mwamva FDC Queens' Mwalimu Aisa Mariki amesema mchango huo wa jezi ni motisha kubwa katika mashindano hayo ya ligi ya mabingwa wa mikoa yatakayoanza kutimua vumbi Julai 16, 2023 katika viwanja vya Alliance School Jijini Mwanza.

"Tunaishukuru sana Kampuni Jambo Food Products kwa kutushika mkono kwa kutupatia jezi hizi, Kampuni hii imekuwa ikitusaidia mara kwa mara kwa vitu mbalimbali na imekuwa mdau mkubwa wa michezo",amesema Mariki.


Mwenyekiti wa Chama cha Soka mkoa wa Shinyanga (SHIREFA), Said Mankiligo ameishukuru Kampuni ya Jambo Food Products imekuwa mdau mkubwa sana katika kusaidia sekta ya michezo katika mkoa wa Shinyanga na kwamba msaada huo utaleta hamasa kwa wachezaji hao wa timu ya wanawake mkoani Shinyanga.


Kwa upande wake Nahodha wa Timu ya Mwamva FDC Queens, Mwajab Athuman amesema watapambana ili kuendelea kuwatia moyo wadau wa soka ikiwemo Kampuni ya Jambo Food Products kwa kuhakikisha timu wanaipandisha daraja.


Akikabidhi jezi hizo, Mwakilishi wa Kampuni ya Jambo Food Products, Chrispin Kakwaya ambaye ni Mkuu wa Idara ya Michezo Jambo Media amesema Kampuni hiyo ilipokea ombi kutoka Chama cha Soka mkoa wa Shinyanga (SHIREFA) kuunga mkono timu hiyo hivyo kutokana na utamaduni wa Kampuni hiyo kusaidia jamii inayowazunguka ndiyo maana wametoa jezi hizo ili timu hiyo ikazitumie kwenye mashindano ya ligi ya mabingwa wa mikoa.
Mwakilishi wa Kampuni ya Jambo Food Products, Chrispin Kakwaya ambaye ni Mkuu wa Idara ya Michezo Jambo Media (kulia) akikabidhi jezi kwa ajili ya Timu ya Soka ya Wanawake Mwamva FDC Queens. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Timu ya Mwamva FDC Queens Mwalimu Aisa Mariki akifuatiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Soka mkoa wa Shinyanga (SHIREFA), Said Mankiligo na Nahodha wa Timu ya Mwamva FDC Queens, Mwajab Athuman.
Mwakilishi wa Kampuni ya Jambo Food Products, Chrispin Kakwaya ambaye ni Mkuu wa Idara ya Michezo Jambo Media (wa pili kulia) akikabidhi jezi kwa ajili ya Timu ya Soka ya Wanawake Mwamva FDC Queens.
Mwakilishi wa Kampuni ya Jambo Food Products, Chrispin Kakwaya ambaye ni Mkuu wa Idara ya Michezo Jambo Media (wa pili kulia) akikabidhi jezi kwa ajili ya Timu ya Soka ya Wanawake Mwamva FDC Queens.
Mwenyekiti wa Chama cha Soka mkoa wa Shinyanga (SHIREFA), Said Mankiligo akizungumza wakati Kampuni ya Jambo Food Products ikikabidhi jezi kwa Timu ya Mwamva FDC Queens
Mwenyekiti wa Chama cha Soka mkoa wa Shinyanga (SHIREFA), Said Mankiligo akizungumza wakati Kampuni ya Jambo Food Products ikikabidhi jezi kwa Timu ya Mwamva FDC Queens
Mwakilishi wa Kampuni ya Jambo Food Products, Chrispin Kakwaya ambaye ni Mkuu wa Idara ya Michezo Jambo Media  akizungumza wakati Kampuni ya Jambo Food Products ikikabidhi jezi kwa Timu ya Mwamva FDC Queens

Mwakilishi wa Kampuni ya Jambo Food Products, Chrispin Kakwaya ambaye ni Mkuu wa Idara ya Michezo Jambo Media akizungumza wakati Kampuni ya Jambo Food Products ikikabidhi jezi kwa Timu ya Mwamva FDC Queens
Mkurugenzi wa Timu ya Mwamva FDC Queens Mwalimu Aisa Mariki akizungumza wakati Kampuni ya Jambo Food Products ikikabidhi jezi kwa Timu ya Mwamva FDC Queens
Nahodha wa Timu ya Mwamva FDC Queens, Mwajab Athuman akizungumza wakati Kampuni ya Jambo Food Products ikikabidhi jezi kwa Timu ya Mwamva FDC Queens
Picha ya kumbukumbu baada ya Kampuni ya Jambo Food Products kukabidhi jezi kwa Timu ya Mwamva FDC Queens
Picha ya kumbukumbu baada ya Kampuni ya Jambo Food Products kukabidhi jezi kwa Timu ya Mwamva FDC Queens

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post