Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2023/24
| ORODHA YA VIFUPISHO |
ASA | Agricultural Seed Agency |
ASDP II | Agriculture Sector Development Programme II |
ATC | Arusha Technical College |
ATCL | Air Tanzania Company Limited |
ATMIS | Agriculture Trade Management Information System |
BRELA | Business Registrations and Licensing Agency |
BTI | Beekeeping Training Institute |
BTIP II | Backbone Transmission Investment Project - II |
CAMARTEC | Centre For Agriculture Mechanization and Rural Technology |
COASCO | Co-operative Audit and Supervision Corporation |
COSTECH | Tanzania Commission for Science and Technology |
CPB | Cereals and Other Produce Board |
DCF | Development Cooperation Framework |
DIT | Dar es Salaam Institute of Technology |
DITF | Dar es Salaam International Trade Fair |
DMDP | Dar es Salaam Metropolitan Development Project |
DMI | Dar es Salaam Maritime Institute |
DUCE | Dar es Salaam University College of Education |
EAC | East Africa Community |
EACOP | East Africa Crude Oil Project |
e-GA | Electronic Government Authority |
e-HRP | Electronic Human Resource Planning |
EIA | Environment Impact Assessment |
e-OPRAS | Electronic Open Performance Review and Appraisal System |
EP4R | Education Program 4 Result |
ESIA | Environment and Social Impact Assessment |
ETH | Engineering Technology Hubs |
FETA | Fisheries Education Training Agency |
FORVAC | Forestry and Value Chain Development Programme |
GePG | Government Electronic Payment Gateway |
GST | Geological Survey of Tanzania |
HCMIS | Human Capital Management Information System |
HESLB | Higher Education Students’ Loans Board |
HGA | Host Government Agreement |
IDRAS | Integrated Domestic Revenue Administration System |
IJA | Institute of Judicial Administration |
IMF | International Monetary Fund |
ISTA | International Seed Testing Agency |
i
JNIA | Julius Nyerere International Airport | |
KIA | Kilimanjaro International Airport | |
LITA | Livestock Training Agency | |
LNG | Liquefied Natural Gas | |
LSP II | Legislative Support Project II | |
MMEM | Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Elimu ya Msingi | |
MSD | Medical Stores Department | |
MSM | Mamlaka za Serikali za Mitaa | |
MTAKUWWA | Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto | |
MTDS | Medium Term Debt Strategy | |
MUCE | Mkwawa University College of Education | |
MUSE | Mfumo wa Ulipaji Serikalini | |
MUST | Mbeya University of Science and Technology | |
NEEC | National Economic Empowerment Council | |
NFRA | National Food Reserve Agency | |
NIDC | National Internet Data Centre | |
NIT | National Institute of Transport | |
NPMIS | National Project Management Information System | |
OECD | Organization for Economic Co-operation and Development | |
OSC | One Stop Centre | |
PFMRP | Public Financial Management Reform Programme | |
PPP | Public-Private Partnership | |
PSSSF | Public Service Social Security Fund | |
REA | Rural Energy Agency | |
REGROW | Resilient Natural Resource Management for Tourism and Growth | |
SELF | Small Entrepreneurs Loan Facility | |
SEZ/EPZ | Special Economic Zone/Export Processing Zone | |
SGR | Standard Gauge Railway | |
SIDO | Small Industries Development Organization | |
SMMRP | Sustainable Management of Mineral Resources Project | |
STAMICO | State Mining Company | |
SUA | Sokoine University of Agriculture | |
SWIOFish | South West Indian Ocean Fisheries Governance and Shared Growth | |
TADB | Tanzania Agricultural Development Bank | |
TAEC | Tanzania Atomic Energy Commission | |
TAFICO | Tanzania Fisheries Corporation | |
TAFIRI TALIRI | Tanzania Fisheries Research Institute Tanzania Livestock Research Institute | |
TAMCO | Tanzania Automobiles Manufacturing Company | |
TANESCO | Tanzania Electrical Supply Company |
|
TARI | Tanzania Agricultural Research Institute |
|
TATC | Tanzania Automotive Technology Centre |
|
TBC | Tanzania Broadcasting Cooperation |
|
TBS | Tanzania Bureau of Standard |
|
TCRA | Tanzania Communication Regulatory Authority |
|
TDCs | Technology Development Centres |
|
TEA | Tanzania Education Authority |
|
TEMDO | Tanzania Engineering and Manufacturing Design Organization |
|
TESP | Teacher Education Support Project |
|
TGC | Tanzania Gemmological Centre |
|
TIRDO | Tanzania Industrial Research and Development Organization |
|
TOSCI | Tanzania Official Seed Certification |
|
TPSF | Tanzania Private Sector Foundation |
|
TTCL | Tanzania Telecommunications Corporation, |
|
UTT - AMIS | Unit Trust of Tanzania- Asset Management and Investor Services |
|
UVIKO-19 | Ugonjwa wa Virusi vya Korona - 19 |
|
YALIYOMO
1.2. Mapitio ya Hali ya Uchumi Kikanda na Kimataifa......................................... 2
1.2.1. Ukuaji wa Uchumi wa Dunia........................................................ 2
1.2.2. Uchumi wa Nchi Zilizoendelea...................................................... 2
1.2.3. Uchumi wa Nchi Zinazoendelea na Zinazoibukia Kiuchumi.................. 2
1.2.4. Uchumi wa Nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara............................ 2
1.3. Mapitio ya Hali ya Uchumi wa Taifa.......................................................... 2
1.3.1. Pato la Taifa na Ukuaji wa Uchumi................................................ 2
1.3.2. Mfumuko wa Bei....................................................................... 2
1.3.3. Sekta ya Nje............................................................................. 2
1.3.4. Sekta ya Fedha......................................................................... 2
1.3.5. Deni la Serikali.......................................................................... 2
1.4.1. Ongezeko la Idadi ya Watu mwaka 2022........................................ 2
1.4.2. Viashiria vya Maendeleo ya Watu.................................................. 2
1.4.2.1. Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini................................... 2
1.4.2.2. Upatikanaji wa Chakula ................................................. 2
MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA MPANGO.......................................................... 2
2.2. Utekelezaji wa Bajeti ya Maendeleo ya Mwaka 2022/23............................... 2
2.3. Hatua za Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo............................................ 2
2.3.1. Miradi ya Kielelezo.................................................................... 2
2.3.2. Kuchochea Uchumi Shindani na Shirikishi....................................... 2
2.3.2.1. Uendelezaji wa Miundombinu na Huduma........................... 2
2.3.2.3. Mapinduzi ya TEHAMA.................................................... 2
2.3.3. Kuimarisha Uwezo wa Uzalishaji Viwandani na Utoaji Huduma............ 2
2.3.3.1. Uzalishaji Viwandani....................................................... 2
2.3.3.2. Ubiasharishaji wa Mazao ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kupitia ASDP II 2
2.3.3.3. Uchimbaji wa Madini, Vito vya Thamani na Gesi Asilia........... 2
2.3.3.4. Huduma....................................................................... 2
2.3.4. Kukuza Biashara na Uwekezaji..................................................... 2
2.3.4.1. Huduma za Biashara na Masoko........................................ 2
2.3.4.2. Kuboresha Mazingira ya Kufanya Biashara na Uwekezaji......... 2
2.3.5. Kuchochea Maendeleo ya Watu.................................................... 2
2.3.5.1. Afya............................................................................ 2
2.3.5.2. Ustawi na Maendeleo ya Jamii.......................................... 2
2.3.5.3. Elimu........................................................................... 2
2.3.5.4. Ardhi, Mipango Miji, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.......... 2
2.3.5.5. Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira............................... 2
2.3.5.6. Hifadhi ya Mazingira na Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi 2
2.3.5.7. Usimamizi wa Maafa Nchini.............................................. 2
2.3.6. Kuendeleza Rasilimali Watu......................................................... 2
2.3.6.1. Ujuzi na Uwezeshaji....................................................... 2
2.3.7. Uwekezaji katika Taasisi na Mashirika ya Umma............................... 2
2.3.8. Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi.................................. 2
2.4.1. Ufuatiliaji wa Miradi katika kipindi cha Mwaka 2022/23...................... 2
2.4.2. Changamoto za Utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2022/23 2
2.4.3. Hatua Zilizochukuliwa Kukabiliana na Changamoto .......................... 2
MIRADI YA KIPAUMBELE KWA MWAKA 2023/24................................................ 2
3.2. Misingi ya Mpango na Shabaha za Ukuaji wa Uchumi.................................. 2
3.2.1. Malengo na Shabaha za Ukuaji wa Uchumi..................................... 2
3.2.2. Misingi (Assumptions) ya Mpango kwa Mwaka 2023/24.................... 2
3.3. Miradi ya Kipaumbele kwa Mwaka 2023/24............................................... 2
3.3.1. Miradi ya Kielelezo..................................................................... 2
3.3.2. Kuchochea Uchumi Shindani na Shirikishi....................................... 2
3.3.2.1. Kuimarisha Mazingira Wezeshi ya Uwekezaji........................ 2
3.3.2.2. Mapinduzi ya TEHAMA.................................................... 2
3.3.2.3. Kuimarisha Miundombinu na Mifumo ya Kitaasisi.................. 2
3.3.3. Kuimarisha Uwezo wa Uzalishaji Viwandani na Utoaji Huduma............ 2
3.3.3.1. Uzalishaji Viwandani....................................................... 2
3.3.3.2. Kilimo, Mifugo na Uvuvi................................................... 2
3.3.3.3. Uchimbaji wa Madini, Vito vya Thamani na Gesi Asilia........... 2
3.3.3.4. Huduma....................................................................... 2
3.3.4. Kukuza Biashara na Uwekezaji..................................................... 2
3.3.4.1. Kuboresha Mazingira ya Uwekezaji na Kukuza Uwekezaji........ 2
3.3.4.2. Kukuza Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi.............................. 2
3.3.4.3. Kukuza Sekta Binafsi....................................................... 2
3.3.4.4. Huduma za Biashara na Masoko........................................ 2
3.3.4.5. Mahusiano na Nchi za Nje na Uchumi wa Kidiplomasia........... 2
3.3.5. Kuchochea Maendeleo ya Watu.................................................... 2
3.3.5.1. Afya............................................................................ 2
3.3.5.2. Ustawi na Maendeleo ya Jamii.......................................... 2
3.3.5.3. Elimu........................................................................... 2
3.3.5.4. Ardhi, Mipango Miji, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.......... 2
3.3.5.5. Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira............................... 2
3.3.5.6. Hifadhi ya Mazingira na Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi 2
3.3.5.7. Hifadhi na Kinga ya Jamii................................................ 2
3.3.6. Kuendeleza Rasilimali Watu......................................................... 2
3.3.6.1. Ujuzi na Uwezeshaji....................................................... 2
3.3.7. Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi.................................. 2
3.3.8. Uwekezaji katika Taasisi na Mashirika ya Umma .............................. 2
UGHARAMIAJI WA MPANGO WA MAENDELEO WA TAIFA 2023/24......................... 2
4.2. Ugharamiaji wa Utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo wa Taifa 2023/24........ 2
4.3. Mikakati ya Vyanzo vya Mapato ya Kugharamia Mpango Mwaka 2023/24........ 2
4.4.1. Mapato ya Kodi na Yasiyo ya Kodi................................................. 2
4.5.1. Mikopo ya Nje........................................................................... 2
4.5.2. Mikopo ya Ndani........................................................................ 2
4.5.3. Misaada ya Nje......................................................................... 2
4.6. Vyanzo Mbadala na Bunifu vya Kugharamia Miradi ya Maendeleo .................. 2
UFUATILIAJI, TATHMINI NA UTOAJI WA TAARIFA............................................. 2
5.2. Misingi na Mbinu za Ufuatiliaji na Tathmini................................................. 2
5.4. Muundo wa Taarifa za Ufuatiliaji na Tathmini.............................................. 2
5.5. Mgawanyo wa Majukumu ..................................................................... 2
VIHATARISHI NA MIKAKATI YA KUKABILIANA NAVYO........................................ 2
6.2. Vihatarishi vya Ndani na Nje na Mikakati ya Kukabiliana Navyo...................... 2
MUHTASARI
Mpango wa Mwaka 2023/24 ni wa tatu katika utekelezaji wa Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 – 2025/26, wenye dhima ya Kujenga Uchumi Shindani na Viwanda kwa Maendeleo ya Watu. Mpango huu ni mwendelezo wa utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 inayotekelezwa kupitia Mpango Elekezi wa Muda Mrefu, 2011/12 – 2025/26. Mpango huu ni muhimu katika kuainisha maeneo mahsusi ya vipaumbele kwa Wizara, Idara Zinazojitegemea, Wakala wa Serikali, Taasisi na Mashirika ya Umma, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa mwaka 2023/24.
Mpango wa Mwaka 2023/24 unajumuisha: Malengo na shabaha za Mpango na Bajeti kwa mwaka 2023/24; maeneo mahsusi ya vipaumbele yaliyozingatia vipaumbele vya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 – 2025/26 na Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020; mfumo wa ugharamiaji wa Mpango; wajibu wa sekta ya umma na binafsi na mgawanyo wa majukumu; na mfumo wa ufuatiliaji, tathmini na utoaji wa taarifa za utekelezaji wa Mpango.
Aidha, Mpango wa Mwaka 2023/24 umeandaliwa kwa mujibu wa matakwa ya Ibara ya 63 (3) (c) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 na Sheria ya Bajeti, Sura 439. Maandalizi ya Mpango wa Mwaka 2023/24 yamezingatia nyaraka za kisera za kitaifa, kikanda na kimataifa ambazo ni: Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025; Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 - 2025/26; Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi kwa Ajili ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020; Dira ya Maendeleo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) 2050; Dira ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika(SADC) 2050; Makubaliano ya Paris kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi; Ajenda 2063 ya Maendeleo ya Afrika; na Malengo ya Maendeleo Endelevu 2030.
Wadau mbalimbali kutoka Wizara, Idara Zinazojitegemea, Wakala wa Serikali, Sekretarieti za Mikoa, Mamlaka za Serikali za Mitaa, Taasisi na Mashirika ya Umma na Sekta Binafsi wameshiriki katika Mchakato wa Maandalizi ya Mpango wa Mwaka 2023/24. Vile vile, Washirika wa Maendeleo wameshirikishwa kupitia majadiliano katika maeneo mahsusi ya ushirikiano, ufadhili wa miradi ya maendeleo na programu za kisekta.
Katika kipindi cha utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2022/23, Mwenendo wa uchumi wa Taifa umeendelea kuimarika ambapo thamani halisi ya Pato ghafi la Taifa kwa be iza mwaka 2015 ilifikia shilingi trilioni 141.9 ikilinganishwa na shilingi trilioni 135.5 mwaka 2021, sawa na ukuaji wa asilimia 4.7, nakisi ya urari ilifikia dola za Marekani milioni 4,441.2 kwa kwa kipindi cha mwezi Julai 2022 hadi Aprili 2023, ikilinganishwa na nakisi ya dola za Marekani milioni 2,516.1 katika kipindi kama hicho mwaka 2022, mikopo kwa sekta binafsi iliongezeka kufikia asilimia 22.5 mwaka 2022 ikilinganishwa na asilimia 10 mwaka 2021. Aidha, viwango vya riba za mikopo ya benki za biashara kwa sekta binafsi kwa mwaka vimeendelea kupungua japo kwa kasi ndogo, kufikia wastani wa asilimia 15.91 mwezi Aprili 2023 kutoka ikilinganishwa na asilimia 16.31 Aprili 2022. Aidha, Katika kipindi cha mwezi Mei 2023, mfumuko wa bei nchini ulifikia wastani wa asilimia 4.0 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 3.8 kwa kipindi kama hicho mwaka 2022, kutokana na changamoto ya mlipuko wa UVIKO – 19 na athari za vita ya Urusi na Ukraine.
Kwa ujumla Mpango wa Mwaka 2023/24 umejumuisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa kipindi cha mwaka 2022/23 na miradi ya kipaumbele kwa mwaka 2023/24. Aidha, utekelezaji wa Mpango kwa mwaka 2023/24 utaendelea kutoa kipaumbele kwa miradi ya kielelezo na kimkakati ikiwemo: Ujenzi wa Reli ya Kati kwa Kiwango cha Kimataifa (Standard Gauge); Kufua Umeme wa Maji wa Julius Nyerere – MW 2,115; kuboresha Shirika la Ndege Tanzania (ATCL); ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi kutoka Hoima (Uganda) hadi Tanga (Tanzania); kuchakata na Kusindika Gesi Asilia kuwa Kimiminika (LNG) – Lindi; makaa ya Mawe (Mchuchuma - Njombe) na Chuma (Liganga - Njombe); na kufua Umeme wa Maji wa Ruhudji (MW 358) – Njombe.
Katika kipindi cha Julai 2022 - Aprili 2023, Wizara ya Fedha na Mipango ikishirikiana na taasisi nyingine za Serikali ilifuatilia miradi na programu za maendeleo 211 kati ya miradi 300 iliyopagwa kufuatiliwa katika kipindi husika. Miradi hiyo inajumuisha miradi ya kielelezo na kimkakati katika maeneo mbalimbali nchini. Ufuatiliaji huo ulibaini hatua zilizofikiwa katika utekelezaji wa miradi, mafanikio, changamoto na mapendekezo. Ufuatiliaji na Tathmini uliwezesha kutolewa kwa maamuzi yanayoongozwa na taarifa sahihi na kwa wakati. Aidha, Serikali itaendelea kuchukua hatua za haraka katika kukabiliana na vihatarishi vitakavyojitokeza katika utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo wa Taifa. Hatua hizo zinajumuisha kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa kutunza mazingira ili kudhibiti uharibifu unaotokana na shughuli za kibinadamu, kuendelea kufuatilia kwa karibu mfumuko wa bei ya bidhaa za chakula ili kutoa ruzuku ya mbolea itakayoongeza uzalishaji pamoja na kutoa ruzuku katika bidhaa za mafuta.
Kitabu cha Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2023/24 kimegawanyika katika sura sita (6): Sura ya kwanza (1) ni mapitio ya hali ya uchumi; Sura ya pili (2) ni mapitio ya utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo wa mwaka 2022/23 katika kipindi cha robo tatu; Sura ya tatu (3) inaelezea miradi na programu ya kipaumbele kwa mwaka 2023/24; Sura ya nne (4) ni ugharamiaji wa Mpango; Sura ya tano (5) inaainisha utaratibu wa ufuatiliaji, tathmini na utoaji taarifa za utekelezaji wa Mpango; na Sura ya sita (6) inaainisha vihatarishi vya utekelezaji wa Mpango na namna ya kukabiliana navyo.
SURA YA KWANZA
HALI YA UCHUMI
1.1. Utangulizi
Sura hii inaelezea mwenendo wa viashiria vya hali ya uchumi nchini, kikanda na dunia kwa mwaka 2022 pamoja na mwelekeo kwa mwaka 2023. Mwenendo wa viashiria hivyo unajenga msingi wa Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2023/24. Kwa ujumla, mwenendo wa ukuaji wa uchumi katika kipindi cha mwaka 2022 umepungua ukilinganisha na ukuaji katika kipindi cha mwaka 2021.
1.2. Mapitio ya Hali ya Uchumi Kikanda na Kimataifa
1.2.1. Ukuaji wa Uchumi wa Dunia
Kwa mujibu wa taarifa ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) ya Aprili 2023 inaonesha kuwa, kasi ya ukuaji wa uchumi wa dunia imepungua kutoka asilimia 6.3 mwaka 2021 hadi asilimia 3.4 mwaka 2022. Upungufu huo unatokana na sababu mbalimbali ikiwemo kasi ndogo ya ukuaji wa uchumi wa China na India; madhara ya janga la UVIKO-19; vita kati ya Urusi na Ukraine; na sera za kupunguza ukwasi katika chumi za Ulaya ili kukabiliana na mfumuko wa bei. Aidha, Uchumi wa dunia unatarajiwa kupungua zaidi na kufikia ukuaji wa asilimia 2.8 mwaka 2023 kutokana na kuendelea kwa vita kati ya Urusi na Ukraine, mabadiliko ya Tabia ya Nchi na Sera za Marekani kuongeza riba.
1.2.2. Uchumi wa Nchi Zilizoendelea
Kiwango cha ukuaji wa uchumi wa nchi zilizoendelea kilipungua na kufikia asilimia 2.7 mwaka 2022 ikilinganishwa na asilimia 5.4 mwaka 2021. Upungufu huu umesababishwa na madhara ya vita kati ya Urusi na Ukraine inayoendelea kuyumbisha uchumi wa dunia hususan kuongezeka kwa gharama za maisha kulikosababishwa na mfumuko wa bei za nishati barani Ulaya na kuongezeka kwa bei za vyakula katika soko la dunia. Aidha, uchumi wa nchi hizi unatarajiwa kupungua na kufikia ukuaji wa asilimia 1.3 mwaka 2023.
1.2.3. Uchumi wa Nchi Zinazoendelea na Zinazoibukia Kiuchumi
Kiwango cha ukuaji wa uchumi wa Nchi Zinazoendelea na Zinazoibukia Kiuchumi ulipungua na kufikia wastani wa asilimia 4.0 mwaka 2022 ikilinganishwa na asilimia 6.9 mwaka 2021. Hii ilitokana na madhara ya vita kati ya Urusi na Ukraine ambayo yameendelea kuathiri uchumi wa nchi hizi. Aidha, kiwango cha ukuaji wa uchumi wa Nchi Zinazoendelea na Zinazoibukia Kiuchumi za Bara la Asia, ikijumuisha China na India kilipungua na kufikia wastani wa asilimia 4.4 mwaka 2022 ikilinganishwa na asilimia 7.5 mwaka 2021.
1.2.4. Uchumi wa Nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara
Ukuaji wa Uchumi kwa Nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara ulipungua kufikia wastani wa asilimia 3.9 mwaka 2022 ikilinganishwa na asilimia 4.8 mwaka 2021. Aidha, uchumi wa nchi hizi unatarajiwa kupungua na kufikia ukuaji wa asilimia 3.6 mwaka 2023. Upungufu huo ulitokana na madhara ya vita kati ya Urusi na Ukraine iliyosababisha mfumuko wa bei za nishati ya mafuta na vyakula. Jedwali Na. 1 linaonesha mwenendo wa ukuaji wa uchumi wa dunia na matarajio.
Jedwali 1: Mwenendo wa Ukuaji wa Uchumi wa Dunia na Matarajio
Kundi/Mwaka |
|
Ukuaji Halisi (asilimia)
|
| Mataraji o (asilimia ) | |||
2017 | 2018 | 2019 | 2020 | 202 1 | 202 2 | 2023 | |
Dunia | 3.8 | 3.6 | 2.8 | -2.8 | 6.3 | 3.4 | 2.8 |
Nchi Zilizoendelea | 2.5 | 2.3 | 1.7 | -4.2 | 5.4 | 2.7 | 1.3 |
Nchi Zinazoendelea na Zinazoibukia | 4.7 | 4.7 | 3.6 | -1.8 | 6.9 | 4.0 | 3.9 |
Nchi Zinazoendelea na Zinazoibukia Kiuchumi za Bara la Asia | 6.6 | 6.4 | 5.2 | -0.5 | 7.5 | 4.4 |
5.3 |
Nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara | 2.9 | 3.2 | 3.3 | -1.7 | 4.8 | 3.9 | 3.6 |
Chanzo: Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF - WEO), Aprili, 2023
1.2.5. Mwenendo wa Ukuaji wa Uchumi kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika
Kiwango cha ukuaji wa Pato la Taifa kwa nchi za ukanda wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kilikuwa cha wastani wa asilimia 4.1 mwaka 2022 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 5.3 mwaka 2021. Aidha, ukuaji wa uchumi kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afirka Mashairiki (EAC) ulikuwa wa wastani wa asilimia 5.3 mwaka 2022 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 6.3 mwaka 2021 kama inavyoonekana katika Jedwali Na. 2.
Jedwali 2: Ukuaji wa Uchumi kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika
Mashariki na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika
Ukuaji wa Uchumi kwa nchi za SADC |
|
| ||
Nchi | 2020 |
| 2021 | 2022 |
Angola | -5.4 |
| 1.1 | 2.8 |
Botswana | -8.7 |
| 11.8 | 6.4 |
Tanzania | 4.8 |
| 4.9 | 4.7 |
DRC | 1.7 |
| 6.2 | 6.6 |
Eswatin | -3.2 |
| 7.9 | 0.5 |
Lesotho | -6 |
| 2.1 | 2.1 |
Madagascar | -4.0 |
| 5.7 | 4.2 |
Malawi | -1.7 |
| 4.6 | 0.8 |
Mauritius | -15.0 |
| 3.5 | 8.3 |
Msumbiji | -1.2 |
| 2.3 | 4.1 |
Namibia | -8.5 |
| 2.7 | 3.8 |
Seychelles | -7.7 |
| 7.9 | 8.8 |
Zambia | -2.8 |
| 4.6 | 3.4 |
Zimbabwe | -5.3 |
| 8.5 | 3.0 |
Afrika ya Kusini | -6.4 |
| 4.9 | 2.0 |
Wastani | -4.6 |
| 5.3 | 4.1 |
Ukuaji wa Uchumi kwa Nchi za EAC |
|
| ||
Burundi | 0.3 |
| 3.1 | 1.8 |
Kenya | -0.3 |
| 7.5 | 5.4 |
Rwanda | -3.4 |
| 10.9 | 6.8 |
DRC | -1.7 |
| 6.2 | 6.6 |
Sudani Kusini | -6.5 |
| 5.3 | 6.6 |
Tanzania | 4.8 |
| 4.9 | 4.7 |
Uganda | -1.3 |
| 6.0 | 4.9 |
Wastani | -1.1 |
| 6.3 | 5.3 |
Chanzo: Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) toleo la Aprili 2023
1.3. Mapitio ya Hali ya Uchumi wa Taifa
1.3.1. Pato la Taifa na Ukuaji wa Uchumi
Mwaka 2022, Mwaka 2022, thamani halisi ya Pato la Taifa kwa bei za mwaka 2015 lilifikia shilingi trilioni 141.9 ikilinganishwa na shilingi trilioni 135.5 mwaka 2021. Aidha, kiwango halisi cha ukuaji wa pato la Taifa kilifikia asilimia 4.7 mwaka 2022 ikilinganishwa na asilimia 4.9 mwaka 2021. Kiwango hicho cha ukuaji kilitokana na: mikakati iliyochukuliwa na Serikali kukabiliana na athari za vita nchini Ukraine; uwekezaji wa kimkakati katika miundombinu ya nishati, maji, afya, elimu, barabara, reli na viwanja vya ndege; kuongezeka kwa uzalishaji wa madini, hususan makaa ya mawe; kuongezeka kwa mikopo kwa sekta binafsi iliyochachua shughuli za kiuchumi; na kuongezeka kwa shughuli za utalii. Kutokana na hatua mbalimbali zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali, Pato ghafi la Taifa linatarajiwa kufikia dola za Marekani billioni 85.42 mwaka 2023/24 kutoka makadirio ya dola bilioni 77.41 mwaka
2022/23.
1.3.2. Mfumuko wa Bei
Vita vya Urusi na Ukraine vimesababisha kupanda zaidi kwa bei ya mafuta duniani, ambayo yamechangia ongezeko la gharama za uzalishaji na usafirishaji wa bidhaa. Mwaka 2022, mfumuko wa bei wa dunia uliongezeka kwa kiwango kikubwa kufikia wastani wa asilimia 8.7 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 4.7 mwaka 2021. Aidha, mfumuko wa bei kwa nchi zilizoendelea uliongezeka na kufikia wastani wa asilimia 7.3 mwaka 2022 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 3.1 mwaka 2021. Vile vile, mfumuko wa bei kwa nchi zinazoendelea za Asia uliongezeka na kufikia wastani wa asilimia 3.8 mwaka 2022 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 2.2 mwaka 2021. Mwaka 2022, mfumuko wa bei kwa nchi za Afrika zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara ulifikia wastani wa asilimia 14.5 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 11.0 mwaka 2021. Kwa ujumla, kuongezeka kwa mfumuko wa bei kulitokana na kupanda kwa bei za nishati na vyakula kulikosababishwa na kuvurugika kwa mnyororo wa uzalishaji kutokana na vita inayoendelea nchini Ukraine pamoja na mabadiliko ya tabianchi.
(a) Mfumuko wa Bei Nchini
Mfumuko wa bei nchini umeendelea kuwa ndani ya lengo la wigo wa kuwa chini ya asilimia 5. Mwaka 2022, mfumuko wa bei ulifikia wastani wa asilimia 4.3 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 3.7 mwaka 2021. Aidha, mfumuko wa bei kwa mwaka unaoishia mwezi Mei, 2023 umebaki kama ilivyokuwa kwa mwaka unaoishia mwezi Mei, 2022 ikiwa ni wastani wa asilimia 4.0. Hali hii imesababishwa na kuongezeka kwa uzalishaji na usambazaji wa bidhaa na huduma; na kuongezeka kwa upatikanaji wa mazao ya chakula katika baadhi ya maeneo nchini na nchi jirani kulikosababishwa na upatikanaji wa mvua katika maeneo yanayotegemea mvua.
Katika kipindi kilichoishia mwezi Mei mwaka 2023, mfumuko wa bei wa vyakula na vinywaji baridi uliongezeka na kufikia asilimia 8.5 ikilinganishwa na asilimia 5.5
katika kipindi kama hicho mwaka 2022. Aidha, mfumuko wa bei usiojumuisha vyakula na nishati (Core Inflation) ulifikia wastani wa asilimia 2.0 katika kipindi cha mwaka unaoishia mwezi Mei 2023 ikilinganishwa na asilimia 3.0 katika kipindi kama hicho mwaka 2022. Kupungua kwa kasi ya upandaji bei ya bidhaa zisizo za vyakula na nishati kulitokana na kuongezeka kwa uzalishaji wa bidhaa hizi nchini, ikiwemo saruji (Kielelezo Na. 1).
Kwa upande mwingine mfumuko wa bei wa nishati, mafuta na ankara za maji ulipungua kutoka asilimia 13.5 katika kipindi cha mwaka unaoishia mwezi Mei 2022 na kufikia asilimia hasi 1.1 kwa mwaka unaoishia mwezi Mei 2023. Hii ilitokana na kupungua kidogo kwa bei ya nishati ya mafuta katika soko la dunia, mfano; kwa mwaka unaoishia mwezi Mei 2022, bei ya dizeli ilipanda kwa asilimia 18.7, petroli asilimia 10.8 na mafuta ya taa kwa asilimia 14.2. Aidha kwa mwaka unaoishia mwezi Mei 2023, bei ya dizeli ilishuka hadi kufikia wastani wa asilimia hasi 0.3, petroli kwa asilimia chanya 1.9 na mafuta ya taa kwa asilimia hasi 2.1
Kielelezo 1: Mwenendo wa Mfumuko wa Bei Nchini (Kwa Mwaka Unaoishia Aprili 2021 hadi Mei 2023)
Chanzo: Ofisi ya Taifa ya Takwimu
(b) Mfumuko wa Bei kwa Nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki
Mfumuko wa Bei kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ulifikia wastani wa asilimia 11.2 mwaka 2022 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 8.6
mwaka 2021. Kuongezeka kwa mfumuko wa bei kulitokana na kupungua kwa uzalishaji wa chakula kwa baadhi ya nchi wanachama na kuongezeka kwa gharama na mahitaji ya mafuta katika nchi hizi. Sababu nyingine ni pamoja na vita vya mara kwa mara katika nchi za Sudani Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Aidha, kwa wastani, viwango vya mfumuko wa bei kwa nchi ya Tanzania, Kenya na Uganda ndivyo pekee viliendelea kuwa ndani ya lengo la Jumuiya la mfumuko usiozidi asilimia 8 kwa mwaka. Kwa upande mwingine, nchi za Burundi na Rwanda ndizo zilikuwa na viwango vikubwa vya mfumuko wa bei mwaka 2022 uliofikia asilimia 18.9 na 13.9 mtawalia ambapo Tanzania ilikuwa na kiwango cha chini zaidi cha mfumuko wa bei wa asilimia 4.3.
Jedwali 3: Mfumuko wa Bei katika Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa Januari 2021 hadi Disemba 2022
Nchi | 2021 | 2022 |
| Mfumuko wa Bei (Asilimia) | |
Tanzania | 3.7 | 4.3 |
Uganda | 2.2 | 6.8 |
Kenya | 6.1 | 7.6 |
Rwanda | 0.8 | 13.9 |
Burundi | 8.3 | 18.9 |
Sudani ya Kusini | 30.2 | 17.6 |
DRC | 9.0 | 9.0 |
Wastani kwa Afrika Mashariki | 8.6 | 11.2 |
Chanzo: Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) toleo la Aprili 2023 na nchi husika.
1.3.3. Sekta ya Nje
Sekta ya nje imeendelea kukabiliwa na changamoto zitokanazo na vita kati nchi ya Ukraine na Urusi pamoja na kuibuka kwa maambukizi mapya ya UVIKO-19. Hali hii imesababisha usumbufu wa mnyororo wa uzalishaji na usambazaji wa bidhaa na huduma duniani na hivyo kupekelea kupanda kwa bei za bidhaa na huduma mbalimbali katika soko la dunia.
(a) Urari wa Malipo ya Kawaida
Kwa kipindi cha mwezi Julai 2022 hadi Aprili 2023, urari wa malipo yote ya nje ulikuwa na nakisi ya dola za Marekani milioni 4,414.2. ikilinganishwa na nakisi ya dola za Marekani milioni 2,516.1 kwa kipindi kama hicho mwaka 2022 Hii ilichangiwa na kuongezeka kwa gharama za uagizaji wa bidhaa kutoka nje ya nchi kutokana na athari hasi kwenye mnyororo wa uzalishaji na ugavi wa bidhaa dunia na malipo ya Serikali nje ya nchi.
(b) Mwenendo wa Biashara ya Bidhaa na Huduma
Urari wa Biashara ya Bidhaa
Urari wa biashara ya bidhaa ulikuwa na nakisi ya dola za Marekani milioni 6,065.6 kwa kipindi cha mwezi Julai 2022 hadi Aprili 2023 ikilinganishwa na nakisi ya dola za Marekani milioni 3,556.8 kwa kipindi kama hicho mwaka 2022. Hii ilitokana na kuongezeka kwa gharama ya uagizaji bidhaa kutoka nje, hususan mafuta ya petroli, mbolea, malighafi za viwandani na bidhaa za ujenzi hususan kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati. Vile vile, vita nchini Ukraine ilisababisha kuongezeka kwa bei za bidhaa kutokana na kuvurugika kwa mnyonyoro wa uzalishaji na ugavi duniani.
Urari wa Biashara ya Huduma
urari wa biashara ya huduma ulikuwa na ziada ya dola za Marekani milioni 2,198.7 kwa kipindi cha mwezi Julai 2022 hadi Aprili 2023 ikilinganishwa na ziada ya dola za Marekani milioni 1,585.1 kwa kipindi kama hicho mwaka 2022, sawa na ongezeko la asilimia 38.7. Hii ilitokana na kuongezeka kwa mapato yatokanayo na shughuli za utalii na usafirishaji kulikosababishwa na kuendelea kuimarika kwa uchumi wa dunia kutokana na kupungua kwa athari za UVIKO-19 pamoja na juhudi za serikali katika kuvutia watalii kutoka nchi mbalimbali duniani.
Urari wa Biashara ya Bidhaa na Huduma
Urari wa biashara ya bidhaa na huduma ulikuwa na nakisi ya dola za Marekani milioni 3,866.9 kwa kipindi cha mwezi Julai 2022 hadi Aprili 2023 ikilinganishwa na nakisi ya dola za Marekani milioni 1,971.7 kwa kipindi kama hicho mwaka 2022.Hii ilichangiwa zaidi na kuongezeka kwa nakisi katika urari wa biashara ya bidhaa kulikosababishwa na ongezeko la gharama za uagizaji wa bidhaa.
(c) Akiba ya Fedha za Kigeni
Akiba ya fedha za kigeni imeendelea kuwa ya kuridhisha kukidhi mahitaji ya uagizaji wa bidhaa na huduma kutoka nje ya nchi. Hadi kufikia Aprili 2023, akiba ya fedha za kigeni ilikuwa dola za Marekani bilioni 4.88 ambayo inatosheleza uagizaji wa bidhaa na huduma kutoka nje ya nchi kwa kipindi cha takriban miezi 4.4. Mahitaji ya nchi kisheria ni kuwa na kiasi cha fedha za kigeni kinachotosheleza uagizaji wa bidhaa na huduma kutoka nje ya nchi kwa muda usiopungua miezi 4.0.
1.3.4. Sekta ya Fedha
(a) Mwenendo wa Viwango vya Riba
Katika kipindi kilichoishia Aprili 2023, riba ya jumla katika soko la fedha baina ya mabenki ilikuwa chini na tulivu japokuwa wastani uliongezeka kidogo hadi asilimia 4.92 kutoka wastani wa asilimia 4.08 kwa kipindi kama hicho mwaka 2022. Aidha, riba ya jumla ya dhamana za Serikali zimeendelea kubaki katika wastani wa asilimia 6.65. Kwa upande mwingine, viwango vya riba za mikopo ya benki za biashara kwa sekta binafsi kwa mwaka 2023 vimeendelea kupungua na kufikia wastani wa asilimia 15.91 Apili 2023 kutoka ikilinganishwa na asilimia 16.31 Aprili 2022. Mwenendo huu ulichagizwa zaidi na utekelezaji wa sera wezeshi ya bajeti, na hatua zilizochukuliwa na Benki Kuu kuchochea ongezeko la ukuaji wa mikopo kwa sekta binafsi na kupunguza riba za mikopo, hatua ambazo zimesababisha baadhi ya benki kutoa mikopo kwa riba ya chini ya asilimia 10 hususan katika shughuli za kilimo kutokana na hatua za kisera zilizochukuliwa na Benki Kuu kupunguza viwango vya riba katika shughuli za kilimo. Wakati huohuo, wastani wa viwango vya riba za amana za muda maalum na za mwaka mmoja ulipungua hadi asilimia 6.79 na asilimia 7.70 kutoka asilimia 6.81 na asilimia 8.28 mwaka 2022, mtawalia.
(b) Ujazi wa Fedha
Kwa mwezi Aprili 2023, Serikali kupitia Benki Kuu ilitekeleza sera ya fedha inayolenga kupunguza kasi ya ongezeko la ukwasi kwenye uchumi ili kukabiliana na shinikizo la kuongezeka kwa mfumuko wa bei linalotokana na mitikisiko ya kiuchumi duniani bila kuathiri kasi ya ukuaji wa shughuli za kiuchumi. Lengo ni kuhakikisha uwepo wa kiwango cha kutosha cha ukwasi kwenye mfumo wa kibenki kuendana na mahitaji halisi ya shughuli mbalimbali za kiuchumi. Kufuatia hali hiyo, ukuaji wa ujazi wa fedha ulikuwa sambamba na malengo ukichangiwa na kuimarika kwa shughuli za kiuchumi zilizokuwa zimeathiriwa na janga la UVIKO - 19 na hivyo kuchochea ongezeko la mahitaji ya mikopo kutoka sekta binafsi. Katika kipindi kilichoishia Aprili 2023, ujazi wa fedha kwa tafsiri pana zaidi (M3) uliongezeka kwa asilimia 17.2 na kufikia shilingi bilioni 39,961.5 kutoka shilingi bilioni 34,087.8 mwezi mwaka Aprili, 2022. Ujazi wa fedha kwa tafsiri pana (M2) ulikua kwa asilimia 15.6 hadi kufikia kiasi cha shilingi bilioni 31,048.8 mwezi Aprili 2023 kutoka shilingi bilioni 26,861.5 katika kipindi kama hicho mwaka 2022. Aidha, ujazi wa fedha kwa tafsiri finyu (M1) uliongezeka kwa asilimia 14.3 na kufikia shilingi bilioni 19,248.3 Aprili, 2023 kutoka shilingi bilioni 16,843.6 katika kipindi kama hicho mwaka 2022.
(c) Mikopo kwa Sekta Binafsi
Sekta ya benki nchini imeendelea kubaki imara, himilivu na yenye kutengeneza faida ikiwa na mtaji na ukwasi wa kutosha katika kutoa mikopo kwa sekta za uchumi na kupunguza umaskini. Mikopo kwa sekta binafsi imeongezeka kufikia shilingi bilioni 28,702.95 kwa mwaka ulioishia Aprili 2023 kutoka shilingi bilioni 23,422.5 Aprili 2022 sawa na ongezeko la asilimia 22.5. Aidha, ukuaji wa mikopo kwa sekta binafsi ulifikia wastani wa asilimia 15.8 katika kipindi cha Aprili 2022 hadi Aprili 2023 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 9.1 katika kipindi kama hicho mwaka 2022 na lengo la asilimia 10.7 kwa mwaka 2022/23. Ukuaji huu umechochewa na utekelezaji wa sera wezeshi za fedha na bajeti, pamoja na hatua zilizochukuliwa na Serikali ikiwemo ulipaji wa malimbikizo ya madai na jitihada nyingine za kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji, hali iliyochochea kuimarika kwa shughuli za kiuchumi nchini.
Katika kipindi cha Aprili 2022 hadi Aprili 2023, ongezeko la mikopo kwa sekta binafsi lilikua kwa kasi zaidi kwenye shughuli za kilimo, mawasiliano na usafirishaji, shughuli binafsi na biashara. Ongezeko la ukuaji wa mikopo kwa shughuli za kilimo lilitokana pia na hatua za kisera zilizochukuliwa Julai 2021, kwa ajili ya kuchochea ongezeko la mikopo na kushusha viwango vya riba katika shughuli za kilimo. Hatua hizo ni pamoja na utoaji wa ruzuku ya mbolea na bidhaa za petroli, punguzo la kodi katika uzalishaji wa mafuta ya kupikia na ongezeko la bajeti kwenye sekta ya kilimo. Aidha, sehemu kubwa ya mikopo imeendelea kuelekezwa katika shughuli binafsi (biashara ndogondogo na biashara za kati) kwa asilimia 38.6, ikifuatiwa na biashara kwa asilimia 16.2, uzalishaji viwandani kwa asilimia 9.6 na kilimo kwa asilimia 8.8.
(d) Mwenendo wa Thamani ya Shilingi
Thamani ya shilingi ya Tanzania dhidi ya sarafu za nchi washirika wakuu wa kibiashara imeendelea kuwa tulivu, licha ya kuwepo kwa changamoto mbalimbali za kiuchumi duniani hususan ongezeko la bei za bidhaa. Hali hii imetokana na utulivu wa mfumuko wa bei nchini ukilinganishwa na nchi washirika wetu wa kibiashara, utekelezaji wa sera thabiti za fedha na bajeti, na uwepo wa chakula cha kutosha nchini. Katika kipindi cha Aprili, 2023 dola moja ya Marekani ilibadilishwa kwa wastani wa shilingi 2,324.07 ikilinganishwa na shilingi 2,322.16 kipindi kama hicho mwaka 2022. Kwa wastani katika kipindi cha Aprili 2022 hadi Aprili 2023 shilingi ya Tanzania ilibadilishwa kwa shilingi 2,310.14. Kutokana na mwenendo huo, thamani ya shilingi imeendelea kupungua kwa kasi ndogo ya chini ya asilimia moja.
(e) Mikopo Chechefu
Ubora wa rasilimali za benki umeendelea kuimarika kutokana na kupungua kwa kiwango cha mikopo chechefu kufikia wastani wa asilimia 5.5 mwezi Aprili 2023 kutoka asilimia 8.3 Aprili 2022. Hali hii ilichangiwa zaidi na hatua mbalimbali zilizochukuliwa na Serikali kwa kuboresha mazingira ya kufanya biashara na kusimamia ukwasi katika uchumi uliowezesha wateja kulipa mikopo kwa wakati pamoja na hatua mbalimbali zilizochukuliwa na Benki Kuu ikiwemo kuhimiza benki za biashara kuongeza umakini katika kuchakata maombi ya mikopo; kuwaondoa katika sekta ya benki wafanyakazi wa benki wasio waaminifu; kuamuru benki kutumia taarifa za mikopo kutoka katika kanzidata ya taarifa za wakopaji; utekelezaji wa kanuni za kuwalinda walaji wa huduma za kibenki kwa kuhakikisha utunzaji wa haki na usawa wa walaji pamoja na wakopaji; na kuhakikisha kunakuwa na uwazi wa taarifa za kifedha kwa kutoa elimu ya fedha kwa watumiaji wa huduma za kifedha. Vilevile, Benki Kuu ilielekeza benki na tasisi za fedha kuwa na mifumo ya udhibiti na utawala bora kwa kupitia upya mifumo iliyopo ili kukidhi mabadiliko na maendeleo katika sekta ya benki.
(f) Ukwasi na Faida za Biashara katika Benki
Sekta ya benki imeendelea kuwa imara na kutengeneza faida ikiwa na mitaji na ukwasi wa kutosha. Viwango vya amana na rasilimali vimeendelea kuongezeka na sekta ya benki imeendelea kuwa imara dhidi ya misukosuko ya ndani na nje. Uwiano wa mtaji wa msingi kwa rasilimali zote ulifikia asilimia 19.6 mwezi Aprili 2023, ikilinganishwa na kiwango kinachokubalika kisheria cha asilimia 10. Aidha, uwiano wa ukwasi wa sekta ya benki kiujumla (Liquid Assets to Demand Liabilities) ulikuwa asilimia 25.37 mwezi Aprili 2023 ikilinganishwa na asilimia 27.89 katika kipindi kama hicho mwaka 2022. Uwiano huu ulikuwa juu ya kiwango cha chini kinachokubalika kisheria cha angalau asilimia 20 na hivyo kuendelea kuwa toshelevu kwa mahitaji ya shughuli mbalimbali za kiuchumi. Sekta ya benki imeendelea kutengeneza faida ambapo faida baada ya kodi (kabla ya ukaguzi wa mahesabu) kwa miezi minne ya kwanza ya mwaka 2023 ilifikia shilingi bilioni 448.5 kutoka shilingi bilioni 374.8 katika miezi minne ya kwanza ya mwaka 2022, sawa na ongezeko la asilimia 19.7
(g) Soko la Upili la Hatifungani
Hatifungani za Serikali
Mauzo ya hatifungani za Serikali zilizoorodheshwa kwenye Soko la Hisa la Dar es Salaam katika kipindi kilichoishia Machi 2023 yalipungua na kufikia shilingi trilioni 2.93, ikilinganishwa na shilingi trilioni 3.21 zilizorekodiwa katika kipindi kilichoishia Machi 2022. Kupungua kwa mauzo ya hatifungani za Serikali kumetokana na marekebisho yaliyofanywa kwenye riba za hatifungani za Serikali, na hivyo kuwafanya wawekezaji kuwa na malengo ya kuendelea na umiliki wa hatifungani zao hadi kipindi zitakapoiva yaani holding to maturity. Marekebisho ya riba za hatifungani za Serikali yaliyofanywa ni kama ifuatavyo: Hatifungani za miaka 25 (kutoka 15.95% hadi 12.56%); Hatifungani za miaka 20 (kutoka 15.49% hadi 12.10%); Hatifungani za miaka 15 (kutoka 13.50% hadi 11.150%); Hatifungani za miaka 10 (kutoka 11.44% hadi 10.25%); Hatifungani za miaka 7 (kutoka 10.08% hadi 9.48%); Hatifungani za miaka 5 (kutoka 9.18% hadi 8.60%); Hatifungani za miaka 2 (kutoka 7.82% hadi 7.60%).
Hatifungani za Kampuni (Corporate Bonds)
Mauzo ya hatifungani za kampuni zilizoorodheshwa kwenye Soko la Hisa la Dar es Salaam katika kipindi kilichoishia Machi 2023, yalipungua na kufikia shilingi milioni 850.25 ikilinganishwa na shilingi bilioni 1.14 zilizorekodiwa katika kipindi kilichoishia Machi 2022. Kupungua kwa mauzo ya hatifungani za kampuni kumetokana na sehemu kubwa ya wawekezaji kuwa na malengo ya kuendelea na umiliki wa hatifungani zao hadi kipindi zitakapoiva yaani holding to maturity kutokana na faida na manufaa ya uwekezaji kwenye bidhaa hizi ikilinganishwa na bidhaa zingine kwenye masoko ya fedha.
Mifuko ya Uwekezaji wa Pamoja
Mwenendo wa uwekezaji katika Mifuko ya Uwekezaji wa Pamoja (Collective Investment Schemes) katika kipindi kilichoishia Machi 2023 ulikuwa mzuri. Thamani ya jumla ya uwekezaji katika mifuko ya uwekezaji wa pamoja iliongezeka kwa asilimia 69.17 na kufikia shilingi trilioni 1.44 katika kipindi kilichoishia Machi 2023, ikilinganishwa na shilingi bilioni 852.21 katika kipindi kilichoishia Machi 2022. Ongezeko hili limetokana na uhamasishaji pamoja na matumizi ya teknolojia katika utoaji wa huduma kwa wawekezaji. Jedwali lifuatalo linaonesha mwenendo wa uwekezaji katika Mifuko ya Uwekezaji wa Pamoja.
Jedwali 4: Mwenendo wa Uwekezaji katika Mifuko ya Uwekezaji wa Pamoja
| 31 Machi 2023 |
31 Machi 2022 |
Ongezeko la thamani | ||||
Meneja wa Mifuko |
Jina la Mfuko | Thamani ya Mfuko (TSH) | Bei ya Kipande (TSH) | Thamani ya Mfuko (TSH) | Bei ya Kipande (TSH) | Ongeze ko la Thaman i ya Mfuko | Ongeze ko la Bei ya Kipande (%) |
UTT AMIS Plc | Mfuko wa Umoja | 311,546,992,055.25 | 903.7726 | 279,862,683,242.28 | 808.9271 | 11.32% | 11.72% |
Mfuko wa Wekeza Maisha | 8,200,947,926.48 | 772.1019 | 3,396,285,286.69 | 680.9052 | 141.47% | 13.39% | |
Mfuko wa Watoto | 9,568,813,873.36 | 569.5515 | 5,141,290,669.40 | 503.8917 | 86.12% | 13.03% | |
Mfuko wa Jikimu | 19,448,126,708.07 | 162.7009 | 18,074,006,916.99 | 154.7339 | 7.60% | 5.15% | |
Mfuko wa Ukwasi | 695,715,800,912.18 | 352.5116 | 365,591,173,928.37 | 312.5168 | 90.30% | 12.80% | |
Mfuko wa Hatifungani | 382,593,090,196.94 | 115.4184 | 180,146,881,623.94 | 113.1666 | 112.38% | 1.99% | |
Watumishi Housing Investmen ts |
Mfuko wa Faida | 14,634,005,454.77 | 102.5569 | Mfuko wa Faida ulikuwa bado haujapata idhini ya kutoa huduma ya uwekezaji. | |||
Thamani ya Jumla | 1,441,707,777,12 7.05 |
| 852,212,321,667.67 |
| 69.17% |
|
Chanzo: UTT AMIS Plc
(h) Mwenendo wa Soko la Hisa
Mwenendo wa biashara katika soko la hisa hupimwa kwa kuzingatia viashiria vya ufanisi wa soko. Viashiria hivyo ni pamoja na: Thamani ya Mauzo ya hisa; Mtaji wa Soko (Market Capitalisation); Fahirisi za Soko (Share Index); na ushiriki kwenye Soko la Hisa. Katika kipindi cha kuanzia Machi 2022 hadi Machi 2023 mwenendo wa Soko la Hisa la Dar es Salaam ulikuwa wa kuridhisha. Ufanisi huu uliotokana na juhudi za Serikali katika kutoa elimu ya masuala ya uwekezaji na fursa na faida za kuwekeza katika masoko ya mitaji na dhamana.
Mtaji wa Soko la Hisa
Mtaji wa Soko la Hisa kwa kampuni za ndani yaani Domestic Market Capitalisation katika kipindi kilichoishia Machi 2023 uliongezeka kwa asilimia 16.97 na kufikia shilingi trilioni 10.82 ikilinganishwa na shilingi trilioni 9.25 katika kipindi kilichoishia Machi 2022. Aidha, Mtaji wa Jumla wa Soko la Hisa yaani Total Market Capitalisation katika kipindi kilichoishia Machi 2023 uliongezeka kwa asilimia 2.47 na kufikia shilingi trilioni 15.74 ikilinganishwa na shilingi trilioni 15.36 katika kipindi kilichoishia Machi 2022. Kuongezeka kwa mtaji wa Soko la Hisa kulitokana na kuongezeka kwa bei ya hisa za baadhi ya kampuni zilizoorodheshwa katika Soko la Hisa. Kampuni hizo ni pamoja na CRDB Bank Plc, DSE Plc, National Investment Company Limited (NICO), NMB Bank Plc, Swissport Tanzania Plc, Tanga Cement Plc, na TOL Gases Limited.
Mauzo ya Hisa
Mauzo ya hisa katika Soko la Hisa yaliongezeka kwa asilimia 2.90 na kufikia shilingi bilioni 119.21 katika kipindi kilichoishia Machi 2023, ikilinganishwa na mauzo ya shilingi bilioni 115.85 katika kipindi kilichoishia Machi 2022. Kuongezeka kwa mauzo kumetokana na kuongezeka kwa ushiriki wa wawekezaji katika masoko ya mitaji kutokana na elimu inayotolewa na Serikali kupitia Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana kwa kushirikiana na wadau wengine.
Fahirisi ya Soko (Market Index)
Fahirisi ya soko kwa hisa za kampuni za ndani yaani Domestic Market Index katika kipindi kilichoishia Machi 2023, iliongezeka kwa alama 573.50 na kufikia alama 4,091.56 ikilinganishwa na alama 3,518.06 zilizorekodiwa katika kipindi kilichoishia Machi 2022. Aidha, Fahirisi ya soko kwa hisa za kampuni zote yaani All Share Index katika kipindi kilichoishia Machi 2023, iliongezeka kwa alama 40.15 na kufikia alama 1,888.79 ikilinganishwa na alama 1,848.64 zilizorekodiwa katika kipindi kilichoishia Machi 2022. Kuongezeka kwa alama za fahirisi kunaashiria ufanisi wa soko hususan kuongezeka kwa bei za hisa za kampuni zilizoorodheshwa DSE, ambazo zinatoa huduma katika sekta za viwanda na fedha.
1.3.5. Deni la Serikali
Hadi kufikia mwezi Aprili 2023, deni la Serikali lilikuwa shilingi bilioni 79,100.19 sawa na ongezeko la asilimia 13.9 ikilinganishwa na Shilingi bilioni 69,440.01 kwa kipindi kama hicho mwaka 2022. Kati ya kiasi hicho, deni la nje ni shilingi bilioni 51,162.60 na deni la ndani ni Shilingi bilioni 27,937.59. Ongezeko la deni limetokana na: kupokewa kwa fedha za mikopo kwa ajili ya kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya barabara, reli, viwanja vya ndege, umeme, elimu na afya.Tathmini ya uhimilivu wa deni la Serikali iliyofanyika Desemba, 2022 imeonesha kuwa deni ni himilivu na viashiria vya deni viko ndani ya wigo unaokubalika kimataifa katika kipindi cha muda mfupi, wa kati na mrefu (Jedwali Na. 5).
Jedwali 5: Tathmini ya Uhimilivu wa Deni (Asilimia) kwa Mwaka 2022
Viashiria Vya Uhimilivu | Ukom o | 21/2 2 | 22/2 3 | 23/2 4 | 24/2 5 | 25/2 6 | 26/2 7 | 27/2 8 | 32/3 3 |
|
|
| Deni la Nje |
|
|
|
|
| |
Uwiano wa thamani ya sasa ya Deni kwa Pato la Taifa | 40 | 18.1 | 17.7 | 17.3 | 16.4 | 15.8 | 15.8 | 16.3 | 15.4 |
Uwiano wa thamani ya sasa ya Deni kwa Mauzo ya Nje ya Nchi | 180 | 119.6 | 113.4 | 108.1 | 104.0 | 101.9 | 101.3 | 99.7 | 92.1 |
Viashiria Vya Uhimilivu | Ukom o | 21/2 2 | 22/2 3 | 23/2 4 | 24/2 5 | 25/2 6 | 26/2 7 | 27/2 8 | 32/3 3 |
Uwiano wa Ulipaji wa Deni kwa Mauzo ya Nchi | 15 | 13.5 | 14.1 | 9.6 | 8.9 | 8.5 | 8.2 | 8.8 | 10.6 |
Uwiano wa Ulipaji wa Deni kwa Mapato | 18 | 14.1 | 14.9 | 10.4 | 9.6 | 9.3 | 9.3 | 10.9 | 12.2 |
Deni la Serikali (Ndani na Nje) |
|
|
| ||||||
Uwiano wa Thamani ya sasa ya Deni kwa pato la Taifa | 55 | 32.5 | 31.9 | 30.9 | 29.5 | 28.4 | 27.8 | 28.6 | 30.8 |
Uwiano wa Thamani ya sasa ya Deni kwa Mapato | N/A | 217 | 207 | 202 | 196 | 194 | 195 | 207.7 | 207.1 |
Uwiano wa Ulipaji wa Deni kwa Mapato | N/A | 34.0 | 41.6 | 33.3 | 30.5 | 27.6 | 27.7 | 30.1 | 41.0 |
Chanzo: Wizara ya Fedha na Mipango, Desemba 2022
Katika kuhakikisha kuwa Deni la Serikali linaendelea kuwa himilivu, Serikali inatekeleza mikakati ifuatayo:
(i) Kuhakikisha mikopo inayopewa kipaumbele ni ile yenye masharti nafuu kadri inavyopatikana. Aidha, hali hiyo inajidhihirisha katika bajeti inayopendekezwa ambapo mikopo nafuu imeongezeka kwa asilimia 22.8 na yenye masharti ya kibiashara imepungua kwa asilimia 14.4;
(ii) Mikopo yenye masharti ya kibiashara itaelekezwa katika miradi inayochochea kasi ya ukuaji wa uchumi na mauzo nje ya nchi; na
(iii) Kuboresha mikakati ya kukusanya mapato ya ndani ili kuhakikisha sehemu kubwa ya bajeti inagharamiwa na mapato ya ndani pamoja na kupunguza matumizi yanayoweza kuepukika bila kuathiri uendeshaji wa shughuli za
Serikali.
Aidha, mnamo Machi 2023, kampuni za Fitch Ratings na Moody’s Investors Service zilianza zoezi la kuifanyia nchi tathmini ya kukopesheka katika masoko ya fedha ya kimataifa. Zoezi hilo lilikamilika ambapo kampuni ya Moody’s Investors Service ilichapisha matokeo ya tathmini hiyo mwezi Mei 2023 na kampuni ya Fitch Ratings mwezi Juni 2023. Kwa mujibu wa matokeo hayo, Tanzania imewekwa katika daraja la B2 POSITIVE na Kampuni ya Moody’s Investors Service pamoja na daraja la B POSITIVE na Kampuni ya Fitch Ratings ambayo yanaashiria taswira chanya kwa nchi kimataifa. Pamoja na mambo mengine, matokeo hayo yamechangiwa na mwenendo mzuri wa ukuaji wa uchumi, usimamizi makini wa deni la Taifa, kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji kwa sekta binafsi, kuimarisha ushirikiano wa kimataifa pamoja na kuleta maridhiano ya kisiasa ndani ya nchi. Kukamilika kwa zoezi hilo, kutaiwezesha nchi kutambulika katika masoko ya fedha ya kimataifa na hivyo, kuongeza wigo wa upatikanaji wa mikopo kwa Serikali na sekta binafsi.
1.4. Maendeleo ya Watu
1.4.1. Ongezeko la Idadi ya Watu mwaka 2022
Kwa mujibu wa matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, idadi ya watu Tanzania imeongezeka na kufikia watu 61,741,120 mwaka 2022 kutoka watu 44,928,923 mwaka 2012 sawa na ongezeko la wastani wa asilimia 3.2. Kati ya idadi hiyo, wanawake ni 31,687,990 sawa na asilimia 51.3 na wanaume ni 30,053,130 sawa na asilimia 48.7 ya watu wote. Matokeo ya sensa ni nyenzo muhimu katika mipango jumuishi na maendeleo endelevu ya nchi.
Aidha, kwa mujibu wa Utafiti wa Watu Wenye Uwezo wa Kufanya Kazi 2020/21, idadi ya nguvu kazi yenye umri wa miaka 15 na kuendelea imeongezeka kwa asilimia 20.6 kutoka watu 25,750,116 na kufikia watu 31,047,894 sawa na asilimia 54.8 ya idadi ya watu wote mwaka 2020/21. Kuongezeka kwa nguvu kazi ni fursa kubwa nchini katika shughuli mbalimbali za uzalishaji pamoja na sekta za huduma na masoko. Kwa upande mwingine, ongezeko la watu linaweza kuwa na athari hasi ikiwepo ongezeko la bajeti katika utoaji wa huduma mbalimbali za kijamii.
1.4.2. Viashiria vya Maendeleo ya Watu
Katika kuendelea kuboresha maendeleo ya watu, Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo: uboreshaji wa huduma za afya; utoaji wa elimu msingi na sekondari bila ada; usambazaji wa umeme mijini na vijijini; utoaji wa huduma ya maji mijini na vijijini; na utoaji wa elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi. Kutokana na utekelezaji wa miradi na programu mbalimbali za maendeleo, kumekua na matokeo chanya katika viashiria vya maendeleo ya watu ikiwemo:
(i) Kuongezeka kwa makadirio ya wastani wa umri wa kuishi kutoka miaka 67.8 (2023) hadi miaka 68.3 (2024) na makadirio ya wastani wa miaka 68.8 kwa mwaka 2025. Aidha, wastani wa umri wa kuishi kwa kuzingatia jinsia, unakadiriwa kufikia miaka 70.7 kwa wanawake na miaka 65.7 kwa wanaume mwaka 2024;
(ii) Vifo vya watoto umri chini ya miaka mitano vimepungua kwa asilimia 36 kutoka vifo 67 kwa vizazi hai 1,000 mwaka 2016 hadi kufikia vifo 43 kwa vizazi hai 1000 mwaka 2022;
(iii) Kupungua kwa vifo vitokanavyo na uzazi kutoka vifo 432 kwa kila vizazi hai 100,000 mwaka 2014/15 hadi vifo 250 kwa kila vizazi hai 100,000 mwaka 2020/21;
(iv) Kuongezeka kwa idadi ya watanzania wanaonufaika na huduma za bima za afya kutoka asilimia 21.2 ya Idadi ya watu mwaka 2019/20 hadi asilimia 30.6 mwaka 2021/22;
(v) Kuongezeka kwa kiwango cha uandikishaji wa wanafunzi wa elimu ya msingi kutoka 1,631,085 mwaka 2021 hadi wanafunzi 1,680,365 mwaka 2022, sawa na ongezeko la asilimia 3.0;
(vi) Hali ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama imeimarika kwa wananchi wa vijijini kutoka wastani wa asilimia 70.1 mwaka 2020 hadi asilimia 77 mwezi Desemba, 2022 na kwa upande wa maeneo ya mijini kutoka wastani wa asilimia 84 mwaka 2020 hadi wastani wa asilimia 88 mwezi Desemba, 2022; na
(vii) Kuunganishwa kwa jumla ya vijiji 10,127 kati ya vijiji 12,318 vya Tanzania Bara sawa na asilimia 82.21.
1.4.2.1. Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini
Serikali kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini imeendelea na jitihada za kupunguza umaskini nchini ambapo hadi Machi 2023 jumla ya kaya 1,371,916 zilizokidhi vigezo vya kuingia katika Kipindi cha Pili cha Mpango kutoka maeneo yote ya utekelezaji 186 kwa Tanzania Bara, Pemba na Unguja kwa Zanzibar ambapo jumla ya shilingi bilioni 218 zilitumika. Aidha, kazi nyingine zilizotekelezwa ni pamoja na: jumla ya vikundi 12,054 viliundwa vyenye jumla ya wanachama 165,608 (wanawake 137,451 na wanaume 28,157) kwenye Mamlaka 72 za utekelezaji kwa Tanzania Bara; na na jumla ya miradi 14,236 iliibuliwa na jamii na kuanza kutekelezwa katika mamlaka za utekelezaji 123 ambapo jumla ya kaya za walengwa 660,000 zimeshiriki katika kutekeleza miradi hiyo yenye thamani ya jumla ya shilingi bilioni 40.2.
1.4.2.2. Upatikanaji wa Chakula
Taarifa ya Tathmini ya Mwisho ya Uzalishaji wa Mazao ya Chakula Msimu wa 2021/2022 inaonesha kuwa, hali ya uzalishaji wa mazao ya chakula umefikia tani 17,148,290 kwa mlinganisho wa nafaka (Grain Equivalent) ambapo mazao ya nafaka ni tani 9,233,298 na mazao yasiyo nafaka ni tani 7,914,992. Aidha, Mahitaji ya chakula kwa mwaka 2022/23 ni tani 15,053, 299 ambapo na ziada ni tani 2,095,256 za chakula. Kiwango cha Utoshelevu wa chakula (Self Sufficiency Ratio – SSR) nchini kinatarajiwa kuwa na ziada kwa uwiano wa asilimia 114 mwaka 2022/23.
SURA YA PILI
MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA MPANGO
2.1. Utangulizi
Sura hii inaeleza kwa muhtasari utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2022/23 hadi Aprili 2023. Aidha, Sura hii inaainisha bajeti iliyotengwa kwa ajili ya kugharamia miradi ya maendeleo, kiasi cha fedha kilichotumika na hatua mbalimbali zilizofikiwa katika utekelezaji wa baadhi ya miradi ya maendeleo. Vile vile, Sura hii inabainisha changamoto zilizojitokeza katika kipindi cha utekelezaji wa Mpango na mikakati ya kukabiliana nazo.
2.2. Utekelezaji wa Bajeti ya Maendeleo ya Mwaka 2022/23
Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2022/23 umetengewa jumla ya shilingi bilioni 15,006.0, sawa na asilimia 36.2 ya Bajeti ya Serikali ambapo shilingi bilioni 12,306.9, sawa na asilimia 82.0 ya bajeti ya fedha za maendeleo ni fedha za ndani na shilingi bilioni 2,699.1, sawa na asilimia 18.0 ni fedha za nje.
Ridhaa ya matumizi ya fedha za maendeleo iliyotolewa katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Mei, 2023, ni shilingi bilioni 12,885.09 sawa na asilimia 93.67 ya lengo katika kipindi hicho. Kati ya kiasi hicho kilichotolewa, shilingi bilioni 11,145.51 ni fedha za ndani na shilingi bilioni 1,739.58 ni fedha za nje. Aidha, baadhi ya maeneo ya kipaumbele yaliyopatiwa fedha za maendeleo katika kipindi husika ni kama ifuatavyo:
(i) Shilingi bilioni 1,164.34 kwa ajili ya Mradi wa Kufua Umeme wa Maji wa Julius Nyerere katika Mto Rufiji – MW 2,115;
(ii) Shilingi bilioni 1,289.46 kwa ajili ya ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kimataifa (Standard Gauge Railway);
(iii) Shilingi bilioni 1,151.11 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa barabara kuu, barabara za mikoa, barabara za mijini na vijijini na madaraja;
(iv) Shilingi bilioni 652.1 kwa ajili ya kugharamia mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu;
(v) Shilingi bilioni 274.71 kwa ajili ya kuimarisha usafirishaji majini ikiwemo ujenzi na ukarabati wa bandari, ununuzi na ukarabati wa meli na vivuko katika bandari za maziwa makuu;
(vi) Shilingi bilioni 290.14 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji mijini na vijijini;
(vii) Shilingi bilioni 199.29 kwa ajili ya ukarabati wa Reli ya Kati (Mfuko wa Maendeleo ya Reli);
(viii) Shilingi bilioni 295.3 kwa ajili ya kugharamia elimumsingi na sekondari bila ada ikijumuisha mahitaji ya wanafunzi wote wa shule za msingi na sekondari
za Serikali na posho ya madaraka kwa wakuu wa shule, waratibu elimu kata na walimu wakuu;
(ix) Shilingi bilioni 202.51 kwa ajili ya mradi wa usambazaji umeme vijijini kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA); na
(x) Shilingi bilioni 159.23 kwa ajili ununuzi wa dawa, vifaa, vifaa tiba na vitendanishi pamoja na chanjo za watoto kupitia MSD
2.3. Hatua za Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo
2.3.1. Miradi ya Kielelezo
Hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa miradi ya kielelezo ni kama ifuatavyo:
(i) Mradi Na. 4281: Ujenzi wa Reli ya Kati kwa Kiwango cha Kimataifa (SGR)
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa njia ya reli kwa kipande cha Dar es Salaam – Morogoro (km 300) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 98.14 ikiwa ni pamoja na ujenzi wa njia ya kuelekea bandarini (Port link) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 34.97; kipande cha Morogoro – Makutupora (km 422) umefikia asilimia 93.83; kipande cha Mwanza - Isaka (km 341) asilimia 31.07; kipande cha Makutupora- Tabora (km 371) asilimia 7.0; kipande cha Tabora - Isaka (km 165) asilimia 2.39; na kusaini mkataba wa ujenzi wa reli ya SGR kipande cha Tabora – Kigoma (km 506).
Shughuli nyingine zilizotekelezwa ni: Ununuzi wa vichwa viwili (2) vya treni na mabehewa 30 kwa ajili ya majaribio na uendeshaji wa awali; kufanyika kwa sehemu ya malipo kwa ajili ya ununuzi wa vichwa vya treni 17 vya umeme na seti za treni 10 za kisasa (Electric Multiple Unit - EMU) kwa ajili ya uendeshaji ambapo utengenezaji wa vichwa vya treni umefikia asilimia 42.1 na utengenezaji wa seti za treni umefikia asilimia 38.1; kununuliwa kwa mabehewa 59 ya abiria ambapo mabehewa 14 yamewasili nchini na mabehewa 45 yaliyosalia utengenezaji unaendelea ambao umefikia asilimia 95; na ununuzi wa mabehewa 1,430 ya mizigo ambapo utengenezaji umefikia asilimia 42. Jumla ya shilingi bilioni 1,289.46 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(ii) Mradi Na. 3172: Kufua Umeme wa Maji wa Julius Nyerere (MW 2,115)
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa handaki la kuchepusha maji (diversion tunnel); kukamilika kwa ujenzi wa kingo ndogo za juu na chini, ukuta wa bwawa kuu ambapo utekelezaji umefikia asilimia 94.85, handaki la kupeleka maji kwenye mitambo (power waterway) asilimia 99.08, jengo la mitambo (power house) (asilimia 68.30), kituo cha kupokea na kusafirishia umeme (switchyard) (asilimia 98.87), kingo saidizi za kuzuia maji yasitoroke (asilimia 84.47), nyumba za makazi ya watumishi (asilimia
92.69), barabara za kudumu (asilimia 38.71) na daraja la kudumu (asilimia 96.87). Kwa ujumla utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 86.89. Aidha, zoezi la ujazaji maji linaendelea ambapo hadi kufikia tarehe 23 Mei, 2023 kina cha maji ya bwawa kimefikia mita 160.51 kutoka usawa wa bahari. Jumla ya shilingi bilioni 1,164.3 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(iii) Mradi Na. 4294: Kuboresha Shirika la Ndege Tanzania
Hatua iliyofikiwa ni: Kufanyika kwa sehemu ya malipo ya ununuzi wa ndege nne (4) ambazo ni ndege moja (1) aina ya Boeing 767-300F ya mizigo iliyowasili tarehe 03 Juni, 2023, ndege mbili (2) aina ya Boeing 737-9 Max inayotarajiwa kuwasili mwezi Agosti 2023 na nyingine mwezi Desemba 2023 na ndege moja (1) aina ya Boeing 787-8 Dreamliner inayotarajiwa kuwasili mwezi Februari, 2024; ukarabati wa miundombinu katika karakana ya KIMAFA katika Kiwanja cha Ndege cha Kilimanjaro (KIA) unaendelea ambapo utekelezaji umefikia asilimia 85. Aidha, ununuzi wa vifaa na vipuri kwa ajili ya kuwezesha kufanya matengenezo makubwa na madogo kwa ndege zote katika hanga zote za JNIA na KIA unaendelea; kuanza ukarabati wa nyumba 38 zilizopo KIA na ujenzi wa majengo matatu ya kuhifadhia mizigo katika viwanja vya ndege vya JNIA, KIA na Songwe. Vile vile, ATCL imeendelea kutoa huduma ya usafiri wa anga katika vituo 24 ambapo vituo 14 ni vya ndani ya nchi na vituo 10 nje ya nchi. Jumla ya shilingi bilioni 138.47 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(iv) Mradi Na. 3155: Kuchakata na Kusindika Gesi Asilia kuwa Kimiminika (Liquefied Natural Gas - LNG) – Lindi
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na tafiti za kisayansi (geoscience) na tafiti za mitambo itakayosimikwa katika eneo la mradi; na kukamilika kwa majadiliano ya Mkataba Hodhi (HGA) kati ya Serikali na Wawekezaji. Aidha, Mshauri elekezi (Kampuni ya Baker Botts) ambaye anaishauri Serikali kuhusu masuala ya sheria, fedha, biashara, uchumi na masoko ameendelea na kazi kwa kushirikiana na Timu ya Majadiliano ya Serikali (GNT). Jumla ya shilingi bilioni 5.49 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(v) Mradi Na. 3176: Ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi kutoka Hoima (Uganda) hadi Tanga (Tanzania) lenye urefu wa km 1,443
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa malipo ya fidia kwa wananchi 387 kati ya 388 waliopisha maeneo 14 ya ujenzi wa kambi zitakazotumika wakati wa ujenzi wa bomba. Aidha, hadi kufikia mwezi Aprili, 2023 wananchi 9,325 kati ya 9,508 wanaopisha eneo la mkuza wa bomba walikuwa wamelipwa jumla ya shilingi bilioni 31.89 na taratibu za malipo kwa waliobaki zilikuwa zinaendelea. Vilevile, Serikali iliendelea kulipia asilimia 15 ya hisa zake katika Kampuni ya EACOP, ambapo jumla ya dola za Marekani milioni 138.2 zimekwishalipwa. Kazi nyingine zilizotekelezwa ni pamoja na kuendelea na ujenzi wa kituo cha kuweka mfumo wa kupasha joto mabomba (thermal insulation plant) katika kijiji cha Sojo, Nzega Tabora ambapo utekelezaji umefikia asilimia 87 na kutoa Kibali cha Ujenzi wa Mradi, ikiwa ni hatua muhimu katika maandalizi ya kuanza ujenzi wa Mradi. Jumla ya shilingi bilioni 75.48 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(vi) Mradi wa Kiwanda cha Sukari Mkulazi
Hatua iliyofikiwa ni Kusafishwa kwa eneo lenye ukubwa wa hekta 710 kati ya hekta 790 zilizokuwa zimebaki bila kusafishwa. Eneo la shamba lililolimwa na kupandwa miwa limefikia ukubwa wa hekta 3,011 kati ya eneo la hekta 3,600 linalotarajiwa kulimwa na kupandwa miwa. Kupatikana kwa Mkandarasi wa ujenzi wa bwawa kubwa lenye uwezo wa kujaza maji kiasi cha mita za ujazo milioni 3.5 ambapo ujenzi umefikia asilimia 28; ujenzi wa kiwanda cha sukari Mbigiri umefikia asilimia 90; na kununuliwa kwa mtambo wa kupakia miwa "Cane Loader". Jumla ya shilingi bilioni 39.84 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(vii) Mradi Na. 4015: Daraja la Kigongo – Busisi (Mwanza)
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa daraja pamoja na barabara unganishi zenye urefu wa km 1.66 ambapo ujenzi umefikia asilimia 72. Jumla ya shilingi bilioni 126.7 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(viii) Mradi Na. 4191: Daraja Jipya la Selander (Tanzanite Dar es Salaam) Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa barabara unganishi zenye urefu wa km 5.2. Jumla ya shilingi bilioni 1.74 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(ix) Mradi Na. 1122: Magadi Soda Engaruka
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa uthamini wa mradi, vitabu vya uthamini wa fidia vimewasilishwa kwa Mthamini Mkuu wa Serikali na gharama ya fidia iliyohakikiwa ni shilingi bilioni 14.8. Jumla ya shilingi milioni 385.26 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(x) Mradi Na. 3171: Makaa ya Mawe Mchuchuma
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa uhakiki wa mali na kuanza kulipa fidia kwa wananchi wanaopisha mradi katika vitongoji vya Nkomang’ombe, Idusi, Kilomos, Ntiule na Mhambalasi. Aidha, jumla ya shilingi bilioni 5.41 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na zoezi la ulipaji wa fidia.
(xi) Mradi Na. 3161: Chuma Liganga
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa uhakiki wa mali na kuanza kulipa fidia kwa wananchi watakaopisha mradi katika katika vitongoji vya Mnyusi, Ilongi na Myorua katika Kijiji cha Mundindi na Kitongoji cha Luhaha katika Kijiji cha Amani. Aidha, jumla shilingi bilioni 10.36 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na zoezi la ulipaji wa fidia.
(xii) Kanda Maalumu za Kiuchumi ikiwemo Eneo Maalumu la Uwekezaji Bagamoyo
Mradi Na. 4920: Eneo Maalumu la Uwekezaji Bagamoyo
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa kazi ya kuhuisha upembuzi yakinifu na Mpango Kabambe katika eneo husika, kupatikana kwa mkandarasi wa kujenga barabara kwa kiwango cha lami (Asphalt Concrete) yenye urefu wa kilometa 3 katika eneo lililoanza kujengwa viwanda lililopo Zinga – Bagamoyo. Jumla ya shilingi milioni 103 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(xiii) Mradi Na. 4702: Ujenzi wa Bandari ya Uvuvi – Kilwa Masoko
Hatua iliyofikiwa ni kukamilika kwa kazi ya usanifu wa kina (Detail Design) na kuanza kazi ya uchimbaji.
(xiv) Mradi Na. 3165: Kufua Umeme wa Maji wa Ruhudji (MW 358) – Njombe
Hatua iliyofikiwa ni: kukamilika kwa uhuishaji wa Upembuzi Yakinifu; uthamini wa mali za wananchi watakaopisha mradi; na tathmini ya athari za mazingira na jamii.
(xv) Mradi Na. 3167: Kufua Umeme wa Maji wa Rumakali (MW 222) - Njombe
Hatua iliyofikiwa ni: kukamilika kwa uhuishaji wa Upembuzi Yakinifu; na tathmini ya athari za mazingira na jamii.
2.3.2. Kuchochea Uchumi Shindani na Shirikishi
2.3.2.1. Uendelezaji wa Miundombinu na Huduma
A. Reli
(a) Mradi Na. 4213: Mfuko wa Reli
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ununuzi wa mabehewa 22 ya abiria kwa ajili ya reli ya MGR; kukamilika kwa ukarabati wa mabehewa 52 ya mizigo na mabehewa sita (6) ya abiria na kuanza kutoa huduma; na kukamilika kwa uboreshaji wa mfumo wa mawasiliano na umeme katika njia ya reli ya MGR kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza. Jumla ya shilingi bilioni 199.29 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(b) Uboreshaji wa Reli ya TAZARA
Hatua iliyofikiwa ni: Kuunganishwa kwa vichwa vinane (8) katika Mfumo wa Ufuatiliaji wa Mwenendo wa Mabasi ya masafa marefu na treni; usafirishaji wa tani 244,492 za mizigo ikilinganishwa na tani 210,161 zilizosafirishwa katika kipindi kama hicho 2021/22 sawa na ongezeko la asilimia 16.3; kusafirishwa kwa abiria 300,476 hadi Aprili, 2023 ikilinganishwa na 296,307 katika kipindi kama hicho; na kusainiwa kwa mikataba ya kutumia njia ya reli kwa kulipia tozo (Access Fee) na ya kusafirisha mizigo kwa kutumia njia ya reli.
B. Barabara na Madaraja
Barabara za Lami Zinazofungua Fursa za Kiuchumi
(i) Mradi Na. 4147: Barabara ya Kidatu – Ifakara – Lupilo - Malinyi – Londo – Lumecha/Songea (km 499)
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa kipande cha Kidatu – Ifakara (km 68) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 77. Jumla ya shilingi bilioni 17.74 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(ii) Mradi Na. 4149: Barabara ya Makutano – Natta – Mugumu/Loliondo – Mto wa Mbu (km 235)
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa sehemu ya Sanzate – Natta (km 40) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 29; Tarime – Mugumu (km 86) sehemu ya Mogabiri – Nyamongo km 25 (asilimia 8); na kuendelea na maandalizi ya ujenzi wa kipande cha Natta – Mugumu (km 45). Jumla ya shilingi bilioni 12.69 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(iii) Mradi Na. 4190: Barabara ya Itoni – Ludewa - Manda (km 211) Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ujenzi wa kipande cha Lusitu – Mawengi (km 50); na kuendelea na ujenzi wa sehemu ya Itoni – Lusitu (km 50) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 2. Jumla ya shilingi bilioni 15.26 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(iv) Mradi Na. 4193: Barabara ya Handeni – Kiberashi – Kijungu – Kibaya – Njoro – Olboloti – Mrijo Chini – Dalai – Bicha – Chambalo – Chemba – Kwa Mtoro - Singida (Km 460)
Hatua iliyofikiwa ni kuendelea na ujenzi wa sehemu ya Handeni – Kiberashi (km 50) sehemu ya Handeni - Mafuleta (km 20) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 11.61 na sehemu ya Mafuleta – Kileguru (km 30) taratibu za manunuzi zinaendelea. Jumla ya shilingi bilioni 2.41 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(v) Mradi Na. 4188: Barabara ya Mbeya – Makongolosi – Manyoni - Mkiwa (km 528)
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa barabara ya Noranga – Itigi – Mkiwa (km 56.9) kwa kiwango cha lami sehemu ya Noranga – Itigi (Mlongaji – km 25) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 12; ujenzi wa barabara za Itigi Mjini (km 10) umefikia asilimia 70; na sehemu ya Mlongaji - Mkiwa (km 31.9) taratibu za manunuzi zinaendelea. Jumla ya shilingi bilioni 15 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(vi) Mradi Na. 4112: Barabara ya Kigoma – Kidahwe – Uvinza – Kaliua – Tabora (km 389.7)
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa kipande cha Chagu – Kazilambwa (km 36) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 74.4; kuendelea kwa ujenzi wa kipande cha Uvinza – Malagarasi (km 51.1) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 26; na ujenzi wa
Urambo Roundabout unaendelea na umefikia asilimia 60. Jumla ya shilingi bilioni 29.93 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(vii) Mradi Na. 4041: Barabara ya Kitai – Lituhi (km 90) na Daraja la Mnywamaji
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Kitai – Lituhi (km 90) sehemu ya Amanimakoro – Ruanda (km 35) na ujenzi wa daraja la Mnywamaji ambapo utekelezaji umefikia asilimia 22; na sehemu ya Luanda – Ndumbi Port (km 50) taratibu za manunuzi zinaendelea. Jumla ya shilingi bilioni 5.99 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(viii) Mradi Na. 4174: Upanuzi wa Barabara ya Kimara – Kibaha (km 25.7) Ikijumuisha Upanuzi wa Madaraja ya Kibamba, Kiluvya na Mpiji
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi kwa kipande cha Kimara – Kibaha Mizani (km 19.2) na upanuzi wa madaraja ya Kibamba, Kiluvya na Mpiji ambapo utekelezaji umefikia asilimia 86. Jumla ya shilingi bilioni 5.68 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(ix) Mradi Na. 4024: Barabara ya Nanganga - Ruangwa - Nachingwea (km 145)
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi kwa kiwango cha lami kwa kipande cha Nanganga – Ruangwa (km 53.2) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 59. Aidha, taratibu za manunuzi zinaendelea kwa sehemu ya Ruangwa – Nachingwea (km 57.6). Jumla ya shilingi bilioni 7.87 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(x) Mradi Na. 4101: Barabara ya Tanga - Pangani – Makurunge (km 174.5)
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa kipande cha Tanga - Pangani (km 50) kwa kiwango cha lami ambapo utekelezaji umefikia asilimia 62 na barabara ya Pangani – Mkange (km 214.5), sehemu ya Tungamaa – Mkange (km 95.2) utekelezaji umefikia asilimia 19.2; na ujenzi wa Daraja la Pangani lenye urefu wa mita 525 na barabara unganishi (km 25.6) umefikia asilimia 3. Jumla ya shilingi bilioni 20.35 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(xi) Mradi Na. 4014: Barabara ya Kibaoni - Majimoto - Muze - Kilyamatundu (km 152)
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa barabara ya Ntendo – Muze – Kilyamatundu (km 200) sehemu ya Ntendo – Kizungu (km 25) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 14. Jumla ya shilingi bilioni 4.43 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(xii) Mradi Na. 4022: Barabara ya Njombe - Makete - Isyonje (km 157.4) Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ujenzi sehemu ya Moronga – Makete (km 53.5) kwa kiwango cha lami; na kuanza kwa ujenzi wa barabara ya Isyonje – Makete (km 50) Sehemu ya Kitulo – Iniho (km 36). Jumla ya shilingi bilioni 6.61 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(xiii) Mradi Na. 4123: Barabara ya Dumila – Kilosa (km 141)
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa sehemu ya Rudewa - Kilosa (km 24) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 93. Jumla ya shilingi bilioni 1.26 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
Barabara Zinazounganisha Tanzania na Nchi Jirani
(i) Mradi Na. 4124: Barabara ya Sumbawanga - Matai - Kasanga Port (km 117)
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa barabara ya Matai – Kasesya (km 50) kwa kiwango cha lami sehemu ya Matai – Tatanda (km 25) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 12 na sehemu ya Tatanda – Kasesya (km 25) taratibu za manunuzi zinaendelea. Jumla ya shilingi bilioni 5.97 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(ii) Mradi Na. 4115: Barabara ya Marangu - Tarakea - Rongai – Kamwanga/ Sanya Juu (km 271)
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa barabara ya Kiboroloni – Kiharara – Tsuduni – Kidia (km 10.8) kwa kiwango cha lami ambapo utekelezaji umefikia asilimia 46. Jumla ya shilingi bilioni14.69 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(iii) Mradi Na. 4154: Barabara ya Sumbawanga - Mpanda - Nyakanazi (km 432.56)
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea kwa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami ya Mpanda – Mishamo – Uvinza Sehemu ya Vikonge – Luhafwe (km 25) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 11 na sehemu ya Luhafwe – Mishamo Jct (Bulamata) – km 37.25 taratibu za manunuzi zinaendelea; na kuendelea na ujenzi wa barabara ya Kibaoni – Sitalike (km 71) sehemu ya Kibaoni – Mlele Jct (km 50) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 5 na sehemu ya Mlele Jct – Sitalike (km 21) taratibu za manunuzi zinaendelea. Jumla ya shilingi bilioni 27.17 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(iv) Mradi Na. 4141: Barabara ya Nyamuswa – Bunda – Kisorya (km 107.4)
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ujenzi wa kipande cha Kisorya - Bulamba (km 107.4) kwa kiwango cha lami. Jumla ya shilingi bilioni 17.96 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(v) Mradi Na. 4162: Barabara ya Mwigumbi - Maswa - Bariadi - Lamadi (km 121)
Hatua iliyofikiwa ni kukamilika kwa ujenzi wa barabara ya mchepuo wa Maswa (km 11). Jumla ya shilingi bilioni 21.37 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(vi) Mradi Na. 4164: Barabara ya Kidahwe - Kasulu – Kibondo - Nyakanazi (km 341.25)
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa sehemu za Kanyani Junction – Mvugwe (km 70.5) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 56, Mvugwe – Nduta Junction (km 59.35) asilimia 66, Kibondo Junction – Kabingo (km 62.5) asilimia 77 na Nduta Junction – Kibondo (km 25.9) asilimia 58. Jumla ya shilingi bilioni 57.7 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(vii) Mradi Na. 4128: Barabara ya Kyaka – Bugene – Kasulo (km 183.1)
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa sehemu ya Bugene – Kasulo –Kumunazi & Kyaka – Mutukula (km 124) sehemu ya Bugene – Burigi Chato National Park (km 60) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 12. Aidha ujenzi wa sehemu ya Kyaka – Bugene (km 59.10) umekamilika. Jumla ya shilingi bilioni 14.06 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
Barabara za Mikoa na Kupunguza Msongamano
(a) Mradi Na. 4138: Barabara za Kupunguza Msongamano Jijini Dar es Salaam (km 138.5)
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa barabara ya Goba – Matosa – Temboni (km 6) ambapo ujenzi wa km 1 umekamilika; na kuendelea kwa usanifu wa kina kwa ajili ya ukarabati na upanuzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Mwai Kibaki (km 9.1). Jumla ya shilingi bilioni 1.52 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(b) Mradi Na. 4145: Kasulu – Manyovu pamoja na barabara za kuingia Kasulu mjini (km 68)
Hatua iliyofikiwa ni kuendelea na ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Kasulu – Manyovu pamoja na barabara za kuingia Kasulu Mjini (spur roads) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 46. Jumla ya shilingi milioni 329.97 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(c) Mradi Na. 4132: Barabara za Mikoa (km 770.50)
Hatua iliyofikiwa ni: Kujengwa kwa jumla ya kilometa 23.11 za barabara za mikoa kwa kiwango cha lami na jumla ya kilometa 253.67 zilikarabatiwa kwa kiwango cha changarawe. Aidha, utekelezaji wa miradi ya madaraja/makalavati ulifikia asilimia 88.82 ambapo madaraja madogo 40 yalijengwa kwa kutumia fedha za Mfuko Mkuu wa Serikali na madaraja madogo 26 yalijengwa kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara. Jumla ya shilingi bilioni 27.43 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(d) Mradi Na. 4285 Miundombinu ya Mabasi Yaendayo Haraka (Dar es Salaam)
Awamu ya Pili
Hatua iliyofikiwa ni kuendelea na ujenzi wa Lot 1 inayohusisha barabara zenye urefu wa km 20.3 (Mbagala - Mzunguko wa Bandari (Bendera Tatu) – Kariakoo, Barabara ya Kawawa – barabara ya Morogoro (Magomeni), Barabara ya Chang’ombe – Barabara ya Kilwa) ambapo ujenzi umefikia asilimia 90. Jumla ya shilingi bilioni 179.89 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
Awamu ya Tatu
Hatua iliyofikiwa ni kuendelea na ujenzi wa barabara za Azikiwe na Maktaba, Bibi Titi, Uhuru na Nyerere hadi Gongo la Mboto zenye jumla ya kilomita 23.6 na kituo kikuu cha mabasi Kariakoo; Shaurimoyo na Uhuru kupitia Buguruni hadi TAZARA umeanza ambapo utekelezaji umefikia asilimia 5. Jumla ya shilingi bilioni 34.75 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(e) Mradi Na. 4146: Barabara ya Mzunguko katika Jiji la Dodoma
Hatua iliyofikiwa: Kuendelea na ujenzi kwa kiwango cha lami kwa barabara ya mzunguko (Dodoma City Outer Dual Carriageway Ring Road Lot 1 & 2 km 112.3), sehemu za barabara ya Nala – Veyula – Mtumba – Ihumwa Dry Port (km 52.3) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 25; Ihumwa - Dry Port – Matumbulu – Nala (km 60) asilimia 19; Kikombo Jctn – Chololo – Mapinduzi (JWTZ HQ) asilimia 6.5. Jumla ya shilingi bilioni 23.62 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
Barabara za Vijijini na Mijini
Mradi Na. 4170: Matengenezo na Ukarabati wa Barabara
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa matengenezo ya barabara yenye urefu wa km 14,826.35; kukamilika kwa ujenzi wa bararaba kwa kiwango cha lami zenye urefu wa km 163.83 na barabara za changarawe zenye urefu wa km 4,724.15, mifereji ya maji ya mvua yenye urefu wa mita 5,267.85; ujenzi wa madaraja 75 na makalavati 95. Jumla ya shilingi bilioni 420.58 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
Ujenzi wa Nyumba za Serikali na Madaraja
(a) Mradi Na. 4126: Ujenzi wa Madaraja Makubwa
Hatua iliyofikiwa ni: jumla ya madaraja makubwa nane (8) yamejengwa na kukamilika ambayo ni Daraja la Tanzanite (DSM), Daraja la Gerezani (DSM), Daraja la Mpwapwa (Dodoma), Daraja la Kiegeya (Morogoro), Daraja la Ruhuhu (Ruvuma), Daraja la Kitengule (Kagera) na Daraja la Msingi (Singida). Jumla ya shilingi bilioni 3.9 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(b) Mradi Na. 4020: Daraja Jipya la Wami (Pwani)
Hatua iliyofikiwa ni kukamilika kwa ujenzi wa daraja la Wami lenye urefu wa mita 510 na barabara unganishi (km 4.3). Jumla ya shilingi bilioni 14.85 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(c) Mradi Na. 6327: Ujenzi na Ukarabati wa Majengo ya Serikali
Hatua iliyofikiwa: Kukamilika kwa ujenzi wa nyumba 20 za Viongozi Jijini Dodoma na kufanya maandalizi ya kuanza awamu ya II; kukamilika kwa ukarabati wa nyumba 66 kati ya 431 zilizohamishiwa TBA kutoka CDA; kuendelea na ujenzi wa nyumba 150 (Awamu I) za makazi ya watumishi wa umma katika eneo la Nzuguni Jijini Dodoma, ambapo utekelezaji umefikia asilimia 92 na ujenzi wa nyumba 150 nyingine (Awamu ya II) za watumishi wa Umma Jijini Dodoma umefikia asilimia 3; kukamilika kwa ujenzi wa nyumba tano (5) za majaji katika mikoa ya Kilimanjaro, Tabora, Shinyanga na Mtwara na ujenzi wa nyumba moja (1) katika mkoa wa Kagera umefikia asilimia 40; kukamilika kwa ukarabati wa nyumba 40 za viongozi Dodoma eneo la Area D; kuendelea na ukarabati wa nyumba 30 za viongozi mikoani na matengenezo kinga ya majengo ya Magomeni Kota ambapo utekelezaji umefikia asilimia 60; kuendelea na ukarabati wa nyumba zinazomilikiwa na TAMISEMI/NHC katika mikoa 20 zilizohamishiwa TBA ambao umefikia asilimia 67.5; kuendelea na ujenzi wa nyumba za watumishi Temeke Kota ambapo utekelezaji umefikia asilimia 19; na kukamilika kwa ujenzi wa Ghorofa za Watumishi wa Umma katika eneo la Magomeni Kota Awamu ya II “Block” A na ujenzi katika Block B umefikia asilimia 27.
Shughuli nyingine zilizotekelezwa ni: Kukamilika kwa ujenzi wa karakana ya TEMESA katika Mkoa wa Simiyu Awamu ya I na ukarabati wa karakana za Vingunguti na MT Depot Awamu ya I; kuendelea na ukarabati wa karakana za TEMESA mikoa ya Mwanza, Tabora, Kigoma, Mara, Arusha na Mtwara; kukamilika kwa usanifu na usakinishaji (installing) wa Mfumo wa Usimamizi na Ufuatiliaji wa Matengenezo ya Magari, Umeme na Elektroniki na kuanza kwa majaribio ya mfumo katika mikoa ya Iringa, Dodoma na Dar es Salaam; kuendelea na usanifu wa ukarabati wa karakana ya Kisasa katika Mkoa wa Dodoma. Jumla ya shilingi bilioni 17.32 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(d) Mradi Na. 6580: Mradi wa Uendelezaji wa Jiji la Dar es Salaam (DMDP)
Hatua iliyofikiwa ni: Ukamilishaji wa ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilomita 5.3 kwa kiwango cha lami; ukamilishaji wa ujenzi wa mitaro ya maji ya mvua kilomita 1.8; na maandalizi ya uendelezaji wa Bonde la Mto Msimbazi. Jumla ya shilingi bilioni
71.38 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
C. Usafiri Majini
(i) Mradi Na. 4295: Ujenzi na Ukarabati wa Meli
Hatua zilizofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa Meli ya MV Mwanza Hapa Kazi Tu umefikia asilimia 83; kuendelea na ukarabati wa meli ya MV Umoja umefikia asilimia 75.8; kuendelea na ukarabati wa meli ya MT Sangara umefikia asilimia 90.7; Kukamilisha taratibu za kupata Mkandarasi ili kuwezesha kusaini mkataba wa ujenzi wa meli mpya tatu (3) pamoja na chelezo ambapo meli mbili (2) zitajengwa katika Ziwa Tanganyika, meli moja (1) itajengwa katika Ziwa Victoria na Chelezo itajengwa Ziwa Tanganyika. Jumla ya shilingi bilioni 23.19 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(ii) Mradi Na. 4201: Uboreshaji wa Usalama wa Usafiri katika Ziwa Victoria
Hatua zilizofikiwa ni; Kuendelea na taratibu za kumpata Mkandarasi kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Uratibu wa Masuala ya Utafutaji na Uokozi katika Ziwa Victoria (Maritime Rescue Cordination Centre-MRCC, Mwanza; Kukamilisha ununuzi wa mkandarasi kwa ajili ya ujenzi wa Vituo vidogo vitatu (3) vya utafutaji na Uokozi (Search and Rescue- SARs) katika Ziwa Victoria kwenye eneo la Kanyara-Geita, Ukerewe na Musoma; na Kumpata mzabuni kwa ajili ununuzi wa Boti moja (1) ya matibabu (Ambulance Boat) na boti mbili (2) za Utafutaji na Uokozi. Jumla ya shilingi milioni 751.63 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(iii) Vivuko
(a) Mradi Na. 4125: Ujenzi wa Maegesho ya Vivuko
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa upanuzi wa jengo la abiria katika maegesho ya Magogoni – Kigamboni upande wa Kigamboni Jijini Dar es Salaam; kukamilika kwa ujenzi na ukarabati wa maegesho katika vituo sita (6) vya Magogoni – Kigamboni, Kilambo - Namoto, Utete-Mkongo, Iramba – Majita, Nyakaliro – Kome na Kasharu – Buganguzi; kukamilika kwa ujenzi wa miundombinu ya majengo ya kusubiria abiria, ofisi na fensi katika vituo vya Bugolora – Ukara; kuendelea na ujenzi wa miundombinu ya jengo la abiria na ofisi na uzio katika eneo la Kinesi (Mwigobero) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 20 na vituo vya Nyakarilo – Kome na Kisorya – Rugezi vipo kwenye hatua za manunuzi; ujenzi wa maegesho ya Mayenzi – Kanyinya umefikia asilimia 50 ya utekelezaji na maegesho ya Muleba – Ikuza yapo kwenye hatua za manunuzi; ujenzi wa maegesho mapya ya Ijinga – Kahangala (Magu) umefikia asilimia 40 na Bwiro – Bukondo (Ukerewe) umefikia asilimia 80. Jumla ya shilingi milioni 696.17 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(b) Mradi Na. 4139: Ujenzi wa Vivuko Vipya
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa kivuko kipya cha Kisorya – Rugezi ambapo ujenzi umefikia asilimia 57; ujenzi wa vivuko vya Ijinga – Kahangala (Magu), Bwiro – Bukondo (Ukerewe), Nyakarilo – Kome (Buchosa) umefikia asilimia 35. Aidha, maandalizi ya kuanza ujenzi wa kivuko kipya cha pili kitakachotoa huduma kati ya Nyamisati – Mafia (Pwani) yanaendelea na taratibu za kumpata Makandarasi wa ujenzi wa vivuko vipya vya Bayugu - Mbalika zimekamilika. Vile vile, ununuzi wa kivuko kipya cha Magogoni - Kigamboni upo kwenye hatua za mwisho za manunuzi. Jumla ya shilingi bilioni 9.41 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(c) Mradi Na. 4144: Ukarabati wa Vivuko
Hatua iliyofikiwa: Kukamilika kwa Ukarabati wa vivuko vya MV Musoma, MV Kazi, MV TEMESA na MV Tanga; na kuendelea na ukarabati wa vivuko vya MV Misungwi ambapo utekelezaji umefikia asilimia 95, MV Nyerere (asilimia 70), MV Kilombero (asilimia 75), MV Ujenzi (asilimia 68), MV Kitunda (asilimia 30), MV Kyanyabasa (asilimia 30) na ukarabati wa kivuko cha MV Magogoni umeanza. Jumla ya shilingi bilioni 3.83 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
D. Bandari
(a) Mradi Na. 4227: Uboreshaji wa Bandari ya Dar es Salaam
(i) Bandari ya Dar es Salaam
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na awamu ya pili ya utekelezaji wa mradi ambapo shughuli zilizotekelezwa ni: Kuchimba na kupanua lango la kuingilia meli na eneo la kugeuzia meli hadi kufikia kina cha mita 15.5 ambapo utekelezaji umefikia asilimia 96; na kuendelea na ununuzi wa wakandarasi kwa ajili ya kuanza ujenzi wa kuongeza kina kutoka mita 12 hadi kufikia mita 14.5; na kuanza kwa ukarabati Gati Na. 8 – 11. Jumla ya shilingi bilioni 48.83 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(ii) Bandari ya Tanga
Hatua iliyofikiwa ni: Uboreshaji wa Bandari ya Tanga gati namba 1 na 2 umefikia asilimia 99. Jumla ya shilingi bilioni 181.38 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(iii) Bandari Kavu katika Eneo la Ruvu
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ujenzi wa mkongo wa Taifa, nyumba za makazi, ofisi na ufungaji wa umeme; kuendelea na ujenzi wa yadi na sakafu ngumu (pavement) yenye ukubwa wa hekta tano (5) kwa ajili ya kuhifadhi shehena za mizigo ambapo umefikia asilimia 90; na kuendelea na ujenzi wa barabara ya zege yenye urefu wa kilomita 15.5 kutoka barabara kuu ya Morogoro hadi Vigwaza/Kwala ambapo umefikia asilimia 99. Jumla ya shilingi bilioni 48.84 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(b) Bandari za Maziwa Makuu
(i) Ziwa Victoria
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na maandalizi ya awali ya ujenzi wa Bandari za Bukoba na Kemondo Bay; kuendelea na hatua za ununuzi wa Mkandarasi kwa ajili ya ujenzi wa Bandari ya Mwanza South; na kuendelea na hatua za mwisho za kufanya Usanifu wa Kina (Detailed Engineering Design) kwa ajili ya ujenzi wa Mwanza North ikijumuisha miundombinu ya Reli (SGR). Jumla ya shilingi bilioni 3.96 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(ii) Ziwa Tanganyika
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ujenzi wa Gati katika Bandari mpya ya Karema; kuendelea na usanifu wa ujenzi wa Passenger Lounge na ukuta wa mizigo wa Lighter Quay katika Bandari ya Kibirizi na gati la Bandari ya Ujiji ambapo utekelezaji umefikia asilimia 69; na kukamilika kwa ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Bandari ya Kigoma. Jumla ya shilingi bilioni 17.5 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(iii) Ziwa Nyasa
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ujenzi wa sakafu ngumu katika bandari ya Kiwira na Itungi; kuendelea na ujenzi wa sehemu ya kuegesha meli (ramp) katika bandari ya Kiwira; na kukamilika kwa ujenzi wa sehemu ya kuegesha meli katika bandari ya Ndumbi. Jumla ya shilingi milioni 200 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
E. Usafiri wa Anga
(a) Mradi Na. 6267: Institutional Support
(i) Uendeshaji wa Jengo la Tatu la Abiria (JNIA TB III) na Kuboresha
Huduma katika Viwanja vya Ndege
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na uboreshaji wa uzio katika Kiwanja cha Dodoma ambapo utekelezaji umefikia asilimia 75; kazi ya usimikaji wa mfumo wa taa za kuongozea ndege katika kiwanja cha ndege cha Dodoma ilifikia asilimia 40; kuendelea na manunuzi ya gari la Zimamoto; kukamilika kwa uboreshaji wa uzio wa Kiwanja cha Ndege cha Julius Nyerere pamoja na kufunga mfumo ya ufuatiliaji mienendo ya shughuli za kiusalama na uendeshaji (CCTV) katika eneo linalozunguka barabara ya kutua na kuruka ndege katika kiwanja; na kukamilisha ulipaji wa malipo ya fidia kwa wakazi waliopisha upanuzi wa kiwanja cha Ndege cha Dodoma. Jumla ya shilingi bilioni 22.68 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(ii) Mradi wa Ununuzi na Ufungaji wa Rada Nne (4) za Kuongoza Ndege za Kiraia JNIA, KIA, Mwanza na Songwe
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ufungwaji wa rada nne (4) za kuongoza ndege za kiraia katika viwanja vya ndege vya Julius Nyerere, Kilimanjaro, Songwe na Mwanza. Jumla ya shilingi bilioni 10.35 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(b) Mradi Na. 4290: Ununuzi wa Rada, Vifaa na Ujenzi wa Miundombinu ya Hali ya Hewa
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa matengenezo ya rada mbili (2) za hali ya hewa zitakazofungwa katika mikoa ya Mbeya na Kigoma; kuendelea na utengenezaji wa rada mbili (2) zitakazofungwa katika mikoa ya Kilimanjaro na Dodoma ambapo utekelezaji umefikia asilimia 75; kukamilika kwa ununuzi na ufungaji wa vifaa mbalimbali vya hali ya hewa ikiwemo seti tano (5) za vifaa vya utambuzi wa matukio ya radi vilivyofungwa Musoma, Mwanza, Bukoba, Tabora na Kibondo pamoja na vifaa vya kupima hali joto ilivyofungwa katika Kituo cha hali ya hewa kilichopo Singida; kukamilika kwa ununuzi na ufungaji wa kompyuta maalum “Cluster Computer” yenye uwezo mkubwa wa kuchakata taarifa za hali ya hewa iliyofungwa katika Kiwanja cha Ndege cha Julius Nyerere (JNIA); kukamilika kwa ukarabati wa ofisi ya hali ya hewa na nyumba tatu (3) za wafanyakazi zilizopo Mahenge; na kuendelea na ukarabati wa ofisi ya hali ya hewa katika Kiwanja cha Ndege cha Songea. Jumla ya shilingi bilioni 6.17 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(c) Mradi Na. 6377: Kuboresha Miundombinu na Ununuzi wa Vifaa vya Kufundishia
(i) Chuo cha Taifa cha Usafirishaji - NIT
Hatua iliyofikiwa ni: Kusainiwa kwa mkataba kwa ajili ya ununuzi wa vifaa maalum (Full Motion Cabin Crew Mock-up and Fixed Cabin Crew Mock-up) vya mafunzo kwa Wahudumu ndani ya ndege; kuendelea na ujenzi wa majengo nane (8) kwa ajili ya madarasa, maabara, karakana na ofisi za watumishi ambapo majengo matano (5) yanajengwa katika kampasi ya Mabibo – Dar es salaam na majengo matatu (3) katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro; kununuliwa kwa Aircraft Engineering System Trainers (runnerable turbo jet engine na motorised cutway piston engine) na Virtual Maintenance Trainer (VMT) for Boeing 737-800 kwa ajili ya mafunzo ya Wahandisi wa Matengenezo ya Ndege. Jumla ya shilingi bilioni 2.50 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(ii) Chuo cha Bahari Dar es Salaam - DMI
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea kufanya sehemu ya malipo kwa ajili ya kununua mtambo (full mission crane simulator) wa kufundishia kwa ajili ya kuongeza ubora na umahiri katika kuhudumia mizigo kwenye meli na vyombo vingine vya usafirishaji. Jumla ya shilingi milioni 275.41 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(d) Mradi Na. 4209: Kiwanja cha Ndege cha Mwanza
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa upanuzi wa maegesho ya ndege, uzio wa kiwanja, maegesho ya magari; na kukamilika kwa usanifu wa jengo la abiria. Jumla ya shilingi milioni 27.5 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(e) Mradi Na. 4220: Kiwanja cha Ndege cha Mtwara
Hatua iliyofikiwa ni kukamilika kwa kazi ya upanuzi na ukarabati kwa awamu ya kwanza na mradi upo katika kipindi cha uangalizi. Jumla ya shilingi bilioni 6.05 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(f) Mradi Na. 4206: Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa Songwe
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilka kwa ukarabati wa tabaka la juu la barabara ya kutua na kuruka ndege, ufungaji wa taa za kuongozea ndege na ujenzi wa uzio wa usalama; kukamilika kwa ukarabati wa eneo la usalama kwenye barabara ya kutua na kuruka ndege na usimikaji wa taa; na kuendelea kukamilisha jengo jipya la abiria pamoja na ufungaji wa mifumo na vifaa vyake ambapo utekelezaji umefikia asilimia 98. Jumla ya shilingi bilioni 4.66 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(g) Mradi Na. 4226: Viwanja vya Ndege vya Mikoa
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa upanuzi wa njia ya kutua na kuruka ndege, kufungwa kwa mfumo wa kuongozea ndege katika kiwanja cha Ndege Dodoma; kukamilika kwa ujenzi wa barabara ya kutua na kuruka ndege katika kiwanja cha Ndege cha Geita; kukamilika kwa kazi za upanuzi na ukarabati wa Kiwanja cha Ndege cha Songea na ukarabati wa barabara ya kutua na kuruka ndege kwa kiwango cha changarawe katika kiwanja cha Nachingwea; kukamilika kwa ulipaji wa fidia kwa wananchi waliopisha ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Lake Manyara na Tanga; kuendelea na ukarabati wa njia ya kuruka na kutua ndege kwa kiwango cha lami katika kiwanja cha ndege Lindi; na kuendelea na ujenzi na ukarabati wa viwanja vya Ndege vya Iringa (asilimia 50), Musoma (asilimia 47) na Moshi (asilimia 22). Jumla ya shilingi bilioni 18.53 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(h) Mradi Na. 4286: Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi awamu ya kwanza inayohusisha ujenzi wa barabara ya kutua na kuruka ndege, barabara ya viungio, maegesho ya ndege, pamoja na usimikaji wa taa za usalama na kuongozea ndege ambapo utekelezaji umefikia asilimia 18. Aidha, kwa upande wa awamu ya pili inayohusisha ujenzi wa Jengo la Abiria, Jengo la kuongozea Ndege, Kituo cha Zimamoto, Kituo cha Hali ya Hewa na Vituo vidogo nane (8) vya kufua umeme utekelezaji umefikia asilimia 2. Jumla ya shilingi bilioni 51.44 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(i) Mradi Na. 4221: Kiwanja cha Ndege cha Sumbawanga
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na maandalizi ya kuanza ujenzi wa barabara ya kutua na kuruka ndege na viungio vyake, maegesho ya ndege, jengo la abiria, jengo la kuongozea ndege, jengo la uchunguzi wa hali ya hewa, barabara ya kuingia na kutoka kiwanjani na maegesho ya magari pamoja na ufungaji wa taa na mitambo ya kuongozea ndege ambapo kwa sasa taratibu za kusaini Mkataba na Mkandarasi mpya zinaendelea. Jumla ya shilingi milioni 29.14 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(j) Mradi Na. 4222: Kiwanja cha Ndege cha Shinyanga
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na maandalizi ya kuanza ujenzi wa barabara ya kutua na kuruka ndege na viungio vyake, maegesho ya ndege, jengo la abiria, jengo la kuongozea ndege, jengo la uchunguzi wa hali ya hewa, barabara ya kuingia na kutoka kiwanjani na maegesho ya magari pamoja na ufungaji wa taa na mitambo ya kuongozea ndege ambapo utekelezaji umeanza na mradi upo katika hatua za maandalizi (Mobilization). Jumla ya shilingi milioni 29.04 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(k) Mradi Na. 4159: Kiwanja cha Ndege cha Tabora
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na maandalizi ya ujenzi wa barabara ya kuruka na kutua ndege, jengo jipya la abiria, barabara ya kuingia na kutoka kiwanjani, maegesho ya magari, barabara ya kiungio na jengo la uchunguzi wa hali ya hewa ambapo utekelezaji umeanza na mradi upo katika hatua za maandalizi (Mobilization). Jumla ya shilingi milioni 16.94 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
F. Nishati
Miradi ya Kufua umeme
(i) Mradi Na. 3164: Kinyerezi I Extension (MW 185)
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ufungaji wa mitambo mitambo minne (4) yenye uwezo wa kuzalisha Megawati 185 na mitambo hiyo kuwashwa na umeme unaozalishwa kuingizwa katika Gridi ya Taifa. Jumla ya shilingi bilioni 52.18 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(ii) Mradi Na. 3169: Kufua Umeme wa Maji Rusumo (MW 80)
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ujenzi wa bwawa, handaki la kupitishia maji, kituo cha kupoza na kuchochea umeme (switchyard), jengo la utawala na nyumba 24 za kudumu; kuendelea na ujenzi wa jengo la mitambo ambapo utekelezaji umefikia asilimia 98.89 na ufungaji wa mitambo ya kufua umeme asilimia 97. Kwa ujumla mradi umefikia asilimia 99. Jumla ya shilingi bilioni 15.71 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
Miradi ya Usafirishaji na Usambazaji wa Umeme
(i) Mradi Na. 3111: Uimarishaji wa Gridi ya Taifa (National Grid Stabilization)
Hatua iliyofikiwa ni: Kuunganishwa kwa Mkoa wa Kigoma pamoja na Wilaya za Ngara na Biharamulo katika gridi ya Taifa kutokea kituo cha Nyakanazi; kuendelea na ujenzi wa njia ya msongo wa kV 132 kutoka Tabora hadi Katavi; na kuwapata Wakandarasi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya kuimarisha miundombinu ya umeme katika mikoa mbalimbali nchini. Jumla ya shilingi bilioni 88.06 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(ii) Njia ya Kusafirisha Umeme wa Msongo wa kV 220 (Rusumo – Nyakanazi)
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa malipo ya fidia kwa wananchi wanaopisha eneo la mradi; kukamilika kwa usimikaji wa nguzo na uunganishaji wa nyaya za umeme; na kukamilika kwa ujenzi wa kituo cha kupoza umeme cha Nyakanazi. Kwa ujumla utekelezaji wa mradi umekamilika. Jumla ya shilingi bilioni 6.94 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(iii) Mradi Na. 3175: Njia ya Kusafirisha Umeme wa Msongo wa kV 400 kutoka Singida - Arusha – Namanga
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Singida hadi Arusha; kuendelea na ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Arusha hadi Namanga; na kuendelea na ujenzi wa kituo cha kupoza umeme cha Lemugur katika eneo la Kisongo mkoani Arusha. Kwa ujumla utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 95. Jumla ya shilingi bilioni 5.96 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(iv) Mradi Na. 3179: Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme Msongo wa kV 400 kutoka Rufiji – Chalinze – Kinyerezi - Dodoma
Awamu ya kwanza (Rufiji - Chalinze): Hatua iliyofikiwa ni: Ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme imefikia asilimia 93.5 na kituo cha kupoza umeme asilimia 64. Jumla ya shilingi bilioni 89.41 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
Awamu ya pili (Chalinze – Dodoma na Chalinze - Kinyerezi): Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea kulipa fidia wananchi wanaopisha mradi kati ya Kinyerezi – Chalinze na Chalinze - Dodoma; na kukamilika kwa tathmini ya Athari za mradi kwa Mazingira na Jamii pamoja na upembuzi yakinifu. Jumla ya shilingi bilioni 9.42 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(v) Mradi Na. 3166: Njia ya Kusafirisha Umeme wa Msongo wa kV 400 - North West Grid Extension (Iringa – Mbeya - Sumbawanga –
Mpanda - Kigoma – Nyakanazi)
Awamu ya Kwanza: Iringa – Mbeya – Tunduma – Sumbawanga (TAZA):
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa taarifa za tathmini (evaluation reports) za zabuni za Wakandarasi Wajenzi wa mradi ambapo taratibu za kupata kibali (No Objection) kutoka kwa Wafadhili zinaendelea; na kuendelea na ulipaji wa fidia kwa wananchi 6,500 wanaopisha mradi ambapo wananchi 4,750 wamelipwa. Jumla ya shilingi bilioni 16.43 zimetumika kulipa fidia hiyo kwa kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
Awamu ya Pili:Kigoma hadi Nyakanazi:
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa asilimia 90 ya ulipaji wa fidia katika eneo la Kidahwe na eneo la mkuza wa njia ya usafirishaji umeme; kukamilika kwa ununuzi wa vifaa vya ujenzi wa miundombinu ya kusambaza umeme; kuendelea na ujenzi wa njia ya kusafirishia umeme ambao umefikia asilimia 53; kuendelea na taratibu za kuwapata wakandarasi wa vituo vya kupoza umeme vya Nyakanazi na Kidahwe pamoja na njia za usambazaji umeme. Jumla ya shilingi bilioni 6.93 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(vi) Mradi Na. 3113: Usambazaji wa Nishati Vijijini
Hatua iliyofikiwa ni: Kuunganishwa kwa jumla ya vijiji 10,127 kati ya vijiji 12,318 vya Tanzania Bara sawa na asilimia 82.21. Jumla ya shilingi bilioni 202.51 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
Miradi ya Usambazaji wa Gesi Asilia
(i) Mradi Na. 3162: Usambazaji wa Gesi Asilia Mikoa ya Dar es Salaam, Mtwara, Lindi na Pwani
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika usanifu wa mradi; kukamilika Tathmini ya Athari kwa Mazingira; kupatikana kwa Mkandarasi wa ujenzi; kuendelea na ujenzi wa vituo viwili (2) vya CNG, kimoja maeneo ya uwanja wa Ndege mkabala na Terminal III na kingine katika uwanja wa Posta uliopo barabara ya Sam Nujoma mkoani Dar es Salaam; kuendelea na ujenzi wa bomba la usambazaji wa gesi asilia lenye urefu wa kilomita 12.4 kutoka Mwenge hadi Mbezi Beach kupitia barabara ya Bagamoyo ambapo hadi kufikia mwezi Aprili, 2023 umefikia asilimia 44.2; kuendelea na ujenzi wa bomba la kusambaza gesi katika maeneo ya Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) na Mlimani City. Kupitia mradi huu, migahawa mitatu (3) na maabara moja (1) katika chuo cha DUCE pamoja na migahawa 12 iliyopo Mlimani City Mall itaunganishwa ambapo kwa sasa taratibu za kumpata Mkandarasi wa ujenzi zinaendelea; kuendelea na ujenzi wa bomba la gesi asilia kutoka valvu namba tatu (BVS 3) kuelekea Kata za Mnazi Mmoja na Mingoyo mkoani Lindi ambapo utekelezaji umefikia asilimia 60. Aidha, kukamilika kwa bomba hili kutawezesha nyumba 209 za awali zilizounganishwa na miundombinu ya gesi asilia kutumia gesi hiyo.Jumla ya shilingi bilioni 8.89 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
2.3.2.2. Kuimarisha Miundombinu na Mifumo ya Kitaasisi
A. Kuimarisha Shughuli za Mfuko wa Bunge
(i) Mradi Na. 6360: Ujenzi wa Miundombinu ya Bunge
Hatua iliyofikiwa ni: kuendelea ujenzi wa nyumba mbili (2) katika eneo la Kilimani , ambapo hatua ya utekelezaji umefi6103kia asilimia 78.05; kukamilika kwa tathmini ya mahitaji ya mitambo kwa ajili ya ulinzi na usalama na malipo ya awali yamefanyika; na kukamilika kwa ujenzi wa makazi ya Katibu wa Bunge (kilimani – Dodoma). Jumla ya shilingi bilioni 2.54 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023
(ii) Mradi Na. 6318: Ukarabati wa Majengo ya Ofisi
Hatua iliyofikiwa ni kukamilika kwa ukarabati wa jengo la utawala, ukumbi wa Msekwa, ununuzi na ufungwaji wa vipuri vya mtambo wa kupooza hewa katika ukumbi wa Bunge; na kukamilika kwa ukarabati wa kumbi mbili za Bunge na uzio kwa ajili ya usalama. Jumla ya shilingi milioni 388 katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
B. Kuimarisha Uwazi na Uwajibikaji katika Utumishi wa Umma
Utumishi wa Umma na Utawala Bora
(i) Mradi Na. 6315: Ujenzi wa Makazi ya Viongozi Wakuu Wastaafu wa
Kitaifa
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa nyumba ya makazi ya Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John P. Magufuli ambapo utekelezaji umefikia asilimia 99; kuendelea na ukarabati wa nyumba ya makazi ya Rais wa Awamu ya Kwanza Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius K. Nyerere ambapo utekelezaji umefikia asilimia 58; na kuendelea na ujenzi wa Klabu ya Viongozi - Makao Makuu eneo la Nzuguni ambapo ujenzi umefikia asilimia 65. Jumla ya shilingi bilioni 4.44 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(ii) Mradi Na. 6284: Programu ya Maboresho katika Utumishi wa Umma Awamu ya Tatu
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ujenzi wa Mfumo wa Taarifa za Kiutumishi na Mishahara (HCMIS) na kuboreshwa kwa moduli ya Watumishi Portal yenye huduma za kielektroniki za uhamisho wa watumishi, mikopo ya watumishi, taarifa binafsi za mtumishi na hati ya malipo ya mishahara; na kuibuliwa na kuboreshwa kwa mifumo mipya ikiwemo mifumo ya e-Mrejesho, e-Mikutano, e-Rufaa, e-Dodoso pamoja na Shared Helpdesk. Jumla ya shilingi bilioni 3.02 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
C. Mfuko wa Mahakama
(i) Mradi Na. 6310: Ujenzi na Ukarabati wa Majengo ya Mahakama za Wilaya
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ujenzi wa Mahakama ya wilaya ya Manyoni; na kuendelea na ujenzi wa Mahakama za wilaya za Liwale ambapo utekelezaji umefikia asilimia 70, Kwimba (asilimia 80), na Ulanga (asilimia 35). Jumla ya shilingi bilioni 3.8 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili 2023.
(ii) Mradi Na. 6327: Ujenzi na Ukarabati wa Majengo ya Serikali Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa nyumba ya Jaji Mkuu ambapo utekelezaji umefikia asilimia 35; na ujenzi wa jengo la ghorofa sita kwa ajili ya makazi ya Majaji jijini Dodoma ambapo utekelezaji umefikia asilimia 54. Jumla ya shilingi billioni 2.6 zimetumika katika kipindi Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(iii) Mradi Na. 6312: Ujenzi na Ukarabati wa Majengo ya Mahakama za Mwanzo
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa Mahakama za Mwanzo tisa (9) ambapo Mahakama ya Mwanzo Madale (Dar es Salaam) utekelezaji umefikia asilimia 85, Kinesi - Rorya (asilimia 99), Mahenge - Kilolo (asilimia 97), Luilo – Ludewa (asilimia
95), Newala – Newala (asilimia 75) na Usevya – Mlele (asilimia 95); Nyakibimbili -
Bukoba (asilimia 90), Kabanga – Ngara (asilimia 80) na Mlimba na Mang’ula – Morogoro (asilimia 85). Jumla ya shilingi bilioni 3.0 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili 2023.
(iv) Mradi Na. 6314: Ujenzi na Ukarabati wa Majengo ya Mahakama Kuu
Hatua iliyofikiwa ni kukamilika kwa ukarabati wa jengo la Mahakama Kuu Tabora na Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi. Jumla ya shilingi milioni 370 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili 2023.
(v) Mradi Na. 6215: Mradi wa Uboreshaji wa Huduma za Mahakama (Citizen Centric Judiciary Modernisation Project)
Hatua iliyofikiwa ni kukamilika kwa ujenzi wa Mahakama za wilaya 18 za Kyerwa na Misenyi (Kagera), Mbogwe na Nyang’wale (Geita), Itilima na Busega (Simiyu), Gairo, Mvomero na Kilombero (Morogoro), Kakonko, Buhingwe na Uvinza (Kigoma), Butiama na Rorya (Mara), Songwe (Songwe), Tanganyika (Katavi), Kaliua (Tabora) na Mkinga (Tanga). Jumla ya shilingi bilioni 17.5 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili 2023.
D. Utawala Bora na Utawala wa Sheria
(a) Mradi Na. 5501: Kuimarisha Upatikanaji wa Haki za Binadamu
Hatua iliyofikiwa ni: Kuwajengea uwezo watumishi 45 kutoka katika Wizara na Taasisi za Serikali kuhusu uratibu na utoaji wa taarifa za utekelezaji wa mikataba ya kulinda, kuhifadhi na kuendeleza haki za binadamu nchini; na kuandaa rasimu ya mpango kazi wa pili wa kitaifa wa kulinda haki za binadamu nchini kwa kupata maoni ya pande zote mbili za Muungano wa Tanzania. Jumla ya shilingi milioni 78 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(b) Mradi Na. 5502: Mpango Kazi Endelevu wa Kupambana na Rushwa Hatua iliyofikiwa ni: Kuandaa rufaa za viashiria vya rushwa na kuviwasilisha TAKUKURU; kukamilisha kushughulikia mashauri 15 ya rushwa kubwa katika mahakama ya rushwa na uhujumu uchumi; kufanya mapitio ya majalada 55 ya kesi za rushwa kwa ajili kuwajengea uwezo Wakuu wa Mashtaka wa Mikoa mitano (5) ya Dar es Salaam, Dodoma, Arusha, Mbeya na Mwanza ya Programu ya Kujenga mfumo Endelevu wa Kupambana na Rushwa Tanzania. Jumla ya shilingi bilioni 1.2 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(c) Mradi Na. 5507: Upatikanaji wa Haki za Wanawake na Watoto wa Kike
Hatua iliyofikiwa ni: Kuratibu kikao kazi cha wadau wanaotekeleza Eneo Na. 5 la MTAKUWWA la Usimamizi na Utekelezaji wa Sheria ili kuimarisha ulinzi na usalama wa wanawake na Watoto; na Kuzindua Kampeni ya Huduma ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia “Mama Samia Legal Aid Campaign” (2023/24- 2025/26) pamoja na mkakati wake wa utekelezaji inayolenga kutoa elimu ya kisheria, mirathi, ndoa, na taratibu za upatikanaji wa haki na wajibu kwa mujibu wa sheria na katiba ya nchi. Jumla ya Shilingi milioni 135 zilitumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(d) Mradi Na. 5508: Upatikanaji wa Haki kwa Maendeleo Endelevu
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa maandalizi ya mahitaji ya mfumo wa kubadilishana taarifa miongoni mwa Taasisi za Haki Jinai; na kukamilika kwa andiko la kutungwa kwa Sera ya Adhabu. Jumla ya shilingi milioni 967 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(e) Mradi Na. 6201: Haki Mtandao
Hatua iliyofikiwa ni: Kuwajengea uwezo washiriki 65 ambao ni Watoa Huduma za Msaada wa Kisheria, Wasaidizi wa Kisheria, Wasajili Wasaidizi, na Madawati ya Huduma za Kisheria kwenye Magereza na Polisi; na kukamilisha mpango wa mawasiliano ya huduma zinazotolewa na Wizara kwa wananchi. Jumla ya shilingi milioni 225 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(f) Mradi Na. 6207: Kuboresha Uwajibikaji wa Kitaasisi katika Kupambana na Rushwa na Kuongeza wigo wa kuifikia Haki
Hatua iliyofikiwa ni: kufanyika kwa ukaguzi kwa Taasisi 34 za Watoa Huduma ya Msaada wa Kisheria kutoka wilaya 27 za mikoa tisa (9) ya Tanzania Bara; Kufanya maadhimisho ya Wiki ya Msaada wa Kisheria Mkoa wa Kigoma ambapo wananchi 4,150 (wanaume 1,617, wanawake 2,416 na watoto 117) walipatiwa huduma ya msaada wa kisheria; na kutoa huduma ya msaada wa kisheria kwa mahabusu na wafungwa kwa njia ya huduma ya msadaa wa kisheria inayotolewa na mawakili bila malipo (Pro Bono) katika magereza ya Segerea na ukonga ambapo jumla ya wafungwa 56 walipatiwa huduma ikiwemo wanawake 23 na Watoto 33. Jumla ya shilingi milioni 400 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(g) Mradi Na. 6517: Haki ya Mtoto
Hatua iliyofikiwa ni: Kuandaa taarifa ya utekelezaji wa Mkakati wa Pili wa Haki Mtoto na kuwasilisha kwenye kikao cha Jukwaa la Haki Mtoto; kukamilisha kukusanya maoni ya wananchi kuhusu maboresho ya Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 na kuandaa marekebisho ya Sheria husika; kusajili jumla ya watoto 319,624 wenye umri chini ya miaka mitano katika mikoa 23 ya Tanzania Bara inayotekeleza mpango huo; Kukamilisha kuboresha mfumo wa utoaji Haki – Jinai kwa Watoto; kufanya ukaguzi wa watoto wanaokinzana na sheria katika mikoa 26 ya Tanzania Bara na mikoa mitatu (3) ya Kimashtaka ambayo ni Temeke, Kinondoni na Ilala. Jumla ya shilingi bilioni 5.2 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(h) Mradi Na. 6389: Ujenzi wa Majengo ya Ofisi
(i) Mradi wa Ujenzi wa Majengo ya Ofisi ya Taifa ya Mashtaka
Hatua iliyofikiwa ni: kuendelea na ujenzi wa majengo ya Huduma Jumuishi za Sheria yanayojengwa na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka katika mikoa ya Kimashtaka ya Morogoro (asilimia 75), Ilala (Kinyerezi) (asilimia 98), Pwani (asilimia 98) na Mbeya (asilimia 75), Shinyanga (asilimia 35), Manyara (asilimia 35), Njombe (asilimia 10), Katavi (asilimia 10) na Rukwa (asilimia 15). Jumla ya shilingi bilioni 5.56 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(ii) Mradi wa Ujenzi wa Majengo ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa
Serikali
Hatua iliyofikiwa ni: kuendelea na ujenzi wa jengo la Huduma Jumuishi za Sheria la Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jijini Mwanza (asilimia 45); Jumla ya shilingi milioni 733.9 zimetumika katika Julai, hadi Aprili, 2023.
(iii) Ujenzi wa Mji wa Serikali Mtumba - Dodoma
Hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa majengo ya Serikali ni: Kuendelea na Awamu ya Pili ya ujenzi wa majengo ya Wizara katika mji wa Serikali Mtumba ambapo ujenzi wa majengo 24 umefikia wastani wa asilimia 65 na ujenzi wa jengo moja (1) la Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) umefikia asilimia 56. Jumla ya shilingi bilioni 93.83 zimetumika katika Julai, hadi Aprili, 2023.
(iv) Ujenzi wa Makao Makuu ya Mahakama Dodoma
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa Jengo la makao makuu Jijini Dodoma ambapo utekelezaji umefikia asimilia 89. Jumla ya shilingi bilioni 16.9 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili 2023.
(v) Ofisi na Makazi ya Viongozi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa majengo 49 ya muda mrefu ya Halmashauri ambapo majengo tisa (9) kati ya hayo yamekamilika; kuendelea na ujenzi wa majengo 30 kwa Halmashauri zilizohamisha Makao Makuu ambapo jengo moja la Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika limekamilika; na kuendelea na ujenzi wa majengo 30 mapya ya utawala na ujenzi wa nyumba 46 za wakurugenzi na nyumba 78 za wakuu wa idara. Jumla ya shilingi bilioni 87.11 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(vi) Ofisi na Makazi ya Viongozi katika Sekretarieti za Mikoa
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa Ikulu Ndogo katika Mkoa wa Njombe ambapo utekelezaji umefikia asilimia 98; kuendelea na ukamilishaji wa nyumba za Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mkoa wa Njombe (2); kuendelea na ukamilishaji wa nyumba za Makatibu Tawala wa Wilaya za Momba ambapo utekelezaji umefikia asilimia 95; kukamilika kwa ukarabati wa nyumba ya Wakuu wa Wilaya za Ludewa na Siha; kuendelea na ujenzi wa nyumba ya Mkuu wa Wilaya Kibiti ambapo uko hatua ukamilishaji; kuanza ujenzi na ukarabati wa nyumba za wakuu wa wilaya za Iramba, Mbinga, Buhigwe, Mbinga na Momba; na kuanza ujenzi wa uzio wa nyumba ya mkuu wa Wilaya ya Same; kukamilika kwa nyumba za Makatibu Tawala wa mikoa ya Katavi na Njombe na kuanza ujenzi wa nyumba za wahudumu na vibanda vya walinzi ambazo zipo hatua za manunuzi; na kuendelea na ujenzi wa nyumba za Makatibu Tawala wa Mikoa ya Ruvuma na Songwe; na kukamilika kwa nyumba za Wakuu wa Mikoa ya Njombe na Songwe.
Shughuli nyingine zilizofanyika ni: Kuanza ujenzi wa Ofisi za Wakuu wa Wilaya za Kakonko, Same, Hai, Gairo, Malinyi na Ulanga; kukamilika kwa ukarabati wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani; kuendelea na ujenzi wa ofisi za wakuu wa Mikoa ya Geita na Songwe ambapo utekelezaji upo hatua ya ukamilishaji; ukarabati wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa wa Dodoma, Iringa, Kigoma, Kilimanjaro, Ruvuma na Rukwa; na upanuzi wa Ofisi za Wakuu wa Mikoa ya Singida na Kilimanjaro; kuendelea na ujenzi wa ofisi za Tarafa katika Mikoa ya Kilimanjaro (8), Arusha (2), Pwani (5), Mtwara (5), Songwe (4), Katavi (3), Dodoma (3), Mwanza (11), Morogoro (5), Ruvuma (2) na Kigoma (1); na kuendelea na ujenzi wa jengo jipya la Soko la kisasa la Kariakoo ambapo utekelezaji uko hatua ya kumwaga zege kwenye ghorofa ya 4. Aidha, ukarabati wa jengo la zamani unaendelea ambapo utekelezaji umefikia asilimia 56. Jumla ya shilingi bilioni 33.26 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(i) Mradi Na. 6209: Mfuko wa Kuchochea Maendeleo ya Jimbo
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika Mamlaka za Serikali za Mitaa ikiwemo kusaidia ujenzi wa vituo vya afya, vyumba vya madarasa, vyumba vya maabara na miundombinu ya maji na umeme. Jumla ya shilingi bilioni 18.8 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
E. Mradi Na. 6501: Vitambulisho vya Taifa
Hatua iliyofikiwa ni: Kusajiliwa na kutambuliwa kwa watu 774,594 kati yao wageni 575 na wakimbizi 49 na kufanya jumla ya watu waliosajiliwa kufikia 23,960,323 katika mikoa na wilaya zote Tanzania Bara na Zanzibar; kununuliwa kadi ghafi 6,123,438 za kuzalisha vitambulisho; kuchakatwa kwa maombi na kuzalishwa kwa namba za utambulisho wa Taifa (NIN) 623,247 na kufanya jumla namba za utambulisho wa Taifa (NIN) zilizozalishwa kufikia 20,126,693; kuzalishwa na kusambazwa kwa vitambulisho 1,059,716. kwa wananchi na kufanya jumla ya vitambulisho vilivyozalishwa na kusambazwa kufikia 12,097,933; kuunganishwa na kuboreshwa kwa mifumo na miundombinu ya mtandao wa mawasiliano kati ya Ofisi za Usajili za Wilaya na Makao Makuu ambapo ofisi nne (4) zimeunganishwa na kufanya jumla ya ofisi zilizounganishwa kufikia 143; na kuunganishwa kwa Taasisi 14 katika mfumo wa Usajili na Utambuzi na kufanya jumla ya taasisi zilizounganishwa na mfumo kufikia 75. Jumla ya shilingi billion 4.48 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023
F. Usalama wa Raia
(i) Mradi Na. 6302: Ujenzi wa Ofisi na Nyumba za Makazi Tanzania Bara
Hatua iliyofikiwa ni: kukamilika kwa ujenzi wa vituo vitatu (3) vya Polisi vya Daraja “A” Kigamboni, Korogwe na Wanging’ombe, Daraja “B” Ruangwa, Daraja ‘C’ Kirongwe Tarime Rorya; kukamilika kwa ujenzi wa majengo ya Ofisi ya Kamanda wa Polisi wa Mkoa na Mkuu wa Kikosi cha kutuliza ghasia Singida; kukamilika kwa ofisi ya mkoa wa kipolisi Tarime Rorya; kukamilika kwa ujenzi wa majengo mawili (2) ya ghorofa tatu (3) yenye uwezo wa kuishi familia 24 za askari Mabatini – Mwanza; kukamilika kwa ujenzi wa uzio wa kutenganisha eneo la Makao Makuu ya Polisi/CID na eneo la RPC Dodoma; kuendelea na ujenzi wa kituo cha Polisi Daraja ”C” na ujenzi wa nyumba za makazi ya askari Ludewa ambapo utekelezaji umefikia asilimia 65, kituo cha Polisi Daraja “A” katika Mji wa Serikali Mtumba Dodoma (asilimia 80), Daraja “C” Mbande Temeke (asilimia 80), Draja “C” Chang’ombe Dodoma (asilimia 50); ujenzi wa ofisi za makamanda wa Polisi za Mikoa ya Mara (asilimia 95), Katavi (asilimia 75), Njombe (asilimia 60) na ujenzi wa nyumba 3 za kuishi Makamishna wa Polisi Jijini Dodoma umefikia (asilimia 99). Jumla ya shilingi bilioni 1.39 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023
(ii) Mradi Na. 6303: Ujenzi wa Ofisi na Nyumba za Makazi Zanzibar
Hatua iliyofikiwa ni: kukamilika kwa ujenzi wa kituo cha Polisi Mkokotoni Zanzibar, kukamilika kwa ujenzi wa kituo cha Polisi Daraja “C” Kaskazini – Kusini Unguja; kuendelea na ujenzi wa kituo cha Polisi Kizimkazi ambapo utekelezaji umefikia asilimia 65; kukamilika kwa ujenzi wa ofisi za makamanda wa polisi za mkoa wa Kusini na Kaskazini Unguja; kukamilika kwa majengo manne (4) ya kuishi familia nane (8) za askari Mfikiwa Kusini Pemba; na kukamilika kwa ukarabati wa majengo saba (7) ya ghorofa ya kuishi familia 28 za Askari katika Kambi ya Ziwani – Zanzibar. Jumla ya shilingi milioni 739.3 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023
G. Uhamiaji
Mradi Na. 6301: Ujenzi wa Ofisi za Mikoa za Uhamiaji
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika na kukabidhiwa kwa Ofisi ya uhamiaji ya Mkoa wa Geita, Manyara na Lindi; kuendelea na ujenzi wa ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Mtwara ambapo utekelezaji umefikia asilimia 75, Lindi (asilimia 90) na Ofisi ya Makao Makuu ya Uhamiaji Dodoma (asilimia 44); kuendelea na awamu ya kwanza ya ujenzi wa chuo cha mafunzo ya uhamiaji cha Raphael Kubaga kilichopo Boma Kichakamiba wilayani Mkinga (Tanga) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 94; na ujenzi wa Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Manyara asilimia 97. Jumla ya shilingi bilioni 5.70 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
2.3.2.3. Mapinduzi ya TEHAMA
A. Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
(i) Mradi Na. 4283: Ujenzi wa Mkongo wa Mawasiliano wa Taifa
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa upembuzi yakinifu wa ujenzi mpya wa Kilomita
1,600 za Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano na vituo 15 vya kutoleo huduma za Mkongo; kuendelea na kazi za upembuzi yakinifu kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Taifa cha Data Zanzibar; kukamilika kwa ununuzi wa mitambo kwa ajili ya vituo 112 vya kutolea Huduma (transmission and power equipment) ambapo usimikaji umefanyika kwenye vituo 61 vya kutolea huduma (Point of Presence-POPs and Optical Line Amplifiers OLA); kuendelea na ujenzi wa njia mpya za Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano wenye jumla ya Kilomita 4,442; kujengea uwezo kwa wataalamu 114 wa usimamizi na uendeshaji wa Mkongo wa Taifa nchini pamoja na wataalamu wengine 817 katika eneo la usalama mtandao; kukamilika kwa utungwaji wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (Data Protection Act, 2022); na kutoa elimu kwa umma kuhusu usalama wa mtandao kwa wananchi 453, shule za sekondari 3 (wanafunzi 968), vyuo vikuu 8 (wanachuo 656) na wananchi takriban milioni 5.2 kupitia Vyombo vya Habari (TV-9, Redio-8, magazeti-7). Jumla ya shilingi bilioni 54.3 zimetumika hadi Aprili 2023.
(ii) Mradi Na. 4234: Mfumo wa Anwani za Makazi
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa uboreshaji wa programu ya Mfumo wa Kidijitali wa Anwani za Makazi; kufanya mapitio ya baadhi ya sheria, Kanuni na Matamko (Establishment order) zinazoguswa na utekelezaji wa Mfumo wa Anwani za Makazi; kukamilika kwa uhakiki wa taarifa za miundombinu ya Anwani za Makazi pamoja na taarifa za makazi zilizokusanywa katika Operesheni Anwani za Makazi kwenye Halmashauri 23, ambazo ni Majiji ya Dar es Salaam, Mwanza, Dodoma, Arusha, Mbeya na Tanga, Manispaa za Moshi, Kinondoni, Temeke, Ubungo, Kigamboni, Ilemela, Mjini, Magharibi A, Magharibi B pamoja na Halmashauri za Kaskazini A, Kaskazini B, Chakechake, Meru, Mtwara Mikindani, Micheweni, Kusini na Kati; kutoa elimu kwa umma kuhusu Anuani za Makazi kwa wafanyabiashara 166 wa Mkoa wa Dodoma, watumishi 80 kutoka Wizara za Kisekta na watanzania takribani milioni 4.5 kwa kupitia vyombo vya habari; na kutungwa kwa Kanuni ndogo za Anwani za Makazi ambazo zimetumika katika kutekeleza mradi wa Anwani ya Makazi. Jumla ya shilingi bilioni 16.3 zimetumika hadi Aprili 2023.
(iii) Mradi Na. 4280: Tanzania ya Kidijitali
Hatua iliyofikiwa ni: Kusainiwa kwa mkataba na Mshauri Mwelekezi wa kusanifu na kusimamia ujenzi wa Taasisi ya TEHAMA na vituo vitano vya Ubunifu vya kikanda; kuboreshwa kwa miundombinu ya intaneti yenye kasi (broadband) na kuunganisha taasisi 18 kwenye mtandao wa Serikali; kuendelea na kazi ya upembuzi yakinifu kwa ajili ya vituo vya huduma pamoja utakaosaidia kurahisisha utendaji kazi wa vituo hivyo (Business Process re-engeering); kusainiwa kwa mkataba baina ya Wizara na Mshauri Mwelekezi kwa ajili ya usanifu wa Mfumo wa Kitaifa wa Usimamizi wa Taarifa za Takwimu za TEHAMA (NISMIS); kuandaa Mpango Mkakati wa Mfumo wa Kitaifa wa Usimamizi wa Taarifa za Takwimu za TEHAMA (NISMIS) unaojumuisha viashiria vya TEHAMA; kukamilika kwa Mpango Mkakati wa Uchumi wa Kidijitali (Digital economy Framework 2023-2033) utakaosaidia kuongeza matumizi ya kidijitali kwa huduma zinazotolewa na Serikali pamoja na Sekta binafsi; kukamilisha upembuzi yakinifu kwa ajili ya kufanya mapitio ya sera na sheria zinazosimamia TEHAMA; na kuwajengea uwezo wataalam wa TEHAMA nchini kwa kuwapatia watalaam 17 mafunzo ya muda mfupi. Jumla ya shilingi bilioni 21.39 zimetumika hadi Aprili 2023..
(iv) Mradi Na. 4279: Upanuzi wa Usikivu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC)
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa awamu ya kwanza ya ujenzi wa studio za redio (TBC Taifa na TBC FM) na za ukombozi wa Nchi Kusini mwa Afrika katika jengo la utangazaji barabara ya Nyerere; kukamilika kwa taratibu za manunuzi ya kumpata Mzabuni kwa ajili ya Ufungaji wa Mitambo ya redio na TEHAMA katika studio za redio barabara ya Nyerere pamoja na jengo la TBC2 awamu ya pili; kukamilika kwa taratibu za manunuzi za kuwapata wazabuni kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi wa Upanuzi wa Usikivu redio za TBC katika maeneo 9; kuendelea na ujenzi wa makao makuu ya TBC Jijini Dodoma; na kukamilika kwa upembuzi yakinifu wa michoro na mifumo kwa ajili ya ukamilishaji wa jengo la Kituo cha Taifa cha Televisheni (TVT) litakalotumika kwa ajili ya Chaneli ya Utalii ya Tanzania Safari na utawala. Jumla ya shilingi bilioni 6.55 zimetumika hadi Aprili 2023.
(v) Mradi Na. 6567: Habari kwa Umma
Hatua iliyofikiwa ni: Kuandaliwa na kurushwa kwa vipindi ishirini (25) vya Televisheni vinavyohusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC1); kuchapisha na kusambaza nakala 5,000 za jarida la NCHI YETU linaloelezea mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita na utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwemo ya kimkakati; kuratibu mikutano ya Taasisi za Serikali 48 katika kutoa taarifa za utekelezaji wa shughuli zake kwa umma kupitia vyombo vya habari; na kukamilika kwa malipo ya kifaa cha kurushia matangazo mubashara aina ya Live U. Jumla ya shilingi milioni 876.69 zimetumika hadi Aprili 2023.
(vi) Mradi Na. 6505: Kufunga Mtambo Mpya wa Kisasa wa Uchapaji
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa kiwanda cha Kupiga Chapa; na kuwasili kwa mitambo tisa (9) ya uchapaji ambapo jumla ya shilingi bilioni 12.41 zimetumika hadi Aprili 2023.
(vii) Mradi Na. 6226: Kujenga Kituo Kikuu cha Kuendeleza Ubunifu wa TEHAMA na Vituo Vidogo vya Kuendeleza Sekta ya TEHAMA Nchini Hatua iliyofikiwa ni: kusainiwa kwa mkataba na mkandarasi kwa ajili ya kufanya matengenezo na maboresho ya jengo la TEHAMA ziko katika hatua za ukamilishaji; kukamilika kwa upembuzi yakinifu wa kuainisha mahitaji ya vifaa vinavyohitajika kwa ajili ya uundwaji wa bidhaa za TEHAMA hapa nchini; kujenga uwezo kwa wabunifu na watengeneza bidhaa za TEHAMA 165 wa kanda ya Dar es Salaam na Arusha juu ya namna bora ya kukuza bunifu zao ili ziweze kutoa ajira na kuchangia pato la Taifa; na kukamilika kwa matengenezo ya Portal ya wataalamu wa TEHAMA. Jumla ya shilingi milioni 500 zimetumika hadi Aprili 2023.
2.3.3. Kuimarisha Uwezo wa Uzalishaji Viwandani na Utoaji Huduma
2.3.3.1. Uzalishaji Viwandani
(i) Mradi Na. 6103: Kituo cha Kuendeleza Teknolojia ya Magari Tanzania
Hatua iliyofikiwa ni: Kuanzisha karakana kuu ya kukalibu chuma na kiwanda cha
Metal Galvanization; Kununua mitambo kwa ajili ya Maabara ya Utafiti; na Kujenga uwezo na kuendeleza utafiti na kuhawilisha teknolojia ya magari (kufanya Reverse Engineering ya pampu za magari ya Zimamoto na kufanya utafiti na kuzalisha prototype ya Magari ya Deraya). Jumla ya shilingi bilioni 12.0 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023
(ii) Mradi Na. 4486: Uzalishaji Viwandani kupitia Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili (ASDP II)
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na mapitio ya mikakati ya sekta ndogo za nguo na mavazi, ngozi na bidhaa za ngozi na kuanza kutengeneza mikakati mipya ya mafuta, korosho na mkakati wa kuvikuza na kuviendeleza viwanda; kuanza kwa uandishi wa mkakati wa bidhaa za nguo na mavazi; kuendelea kufanya tathmini ya uzalishaji wa magunia ya mkonge na biashara ya magunia ya jute; kuendelea na ukamilishaji taratibu za umiliki wa ardhi yenye ukubwa wa ekari 62 iliyoko Kahama mkoani Shinyanga; kukamilika kwa utambuzi na tathmini ya kongano za viwanda vya mazao ya kilimo na sekta nyingine yenye fursa za ukuaji wa jasiriamali ndogo na za kati katika mikoa yote ya Tanzania Bara. Jumla ya shilingi milioni 633.08 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(iii) Mradi Na. 4948: Kuimarisha Uzalishaji Viwandani kupitia Uboreshaji wa Ubora na Tija - KAIZEN
Hatua iliyofikiwa ni: Kuongezeka kwa idadi ya waratibu wa KAIZEN viwandani kutoka 200 hadi kufikia 230 pamoja na idadi ya viwanda vilivyonufaika na huduma hii kutoka 135 ya hadi kufikia 150; kuongezeka kwa idadi ya mikoa iliyofikiwa na huduma za KAIZEN kutoka 8 hadi 12 ambapo takribani viwanda 16 vimenufaika na mafunzo na kufanikisha kuongeza wakufunzi 36 wapya; na kufanyika kwa mafunzo kwa washiriki 20 kutoka Unguja na 70 kutoka Pemba.
(iv) Mradi Na. 6260: Mradi wa Kusaidia Taasisi
(a) Kiwanda cha Mashine na Vipuri KMTC
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ununuzi na usimikaji wa mashine ya overhead crane; kukamilika kwa ununuzi wa vifaa vinavyohitajika kwa ajili ya tanuru ikiwemo Induction furnace; kukamilika kwa ujenzi wa msingi na kuendelea na usimikaji wa kinu cha kuyeyushia chuma (induction furnace) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 98; na kukamilika kwa ukarabati wa mfumo wa umeme kwa asilimia 99; kukamilika kwa majaribio na mafunzo ya namna ya kutumia kinu cha kuyeyushia chuma kwa awamu ya kwanza, na kuendelea kwa awamu ya pili. Jumla ya shilingi milioni 760.95 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(b) Eneo la Kongano ya Viwanda – TAMCO
Hatua iliyofikiwa ni kupatikana kwa mkandarasi kwa ajili ya ujenzi wa barabara yenye urefu wa mita 320 (China boda road). Jumla ya shilingi milioni 28.7 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(c) Mradi wa kuunganisha Matrekta ya URSUS
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea kufanya mazungumzo na Serikali ya Poland kupitia wawakilishi wa Timu Maalum ya Serikali ya Majadiliano (GNT); na kuendelea kufuatilia madeni kwa wakulima 716 waliokopa matreka hayo. Jumla ya shilingi milioni 200.0 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(d) Kongane la Viwanda Nyanza
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ukarabati wa ghala Na. 1 na kuendelea na ukarabati wa ghala Na. 2 ambapo utekelezaji umefikia asilimia 10. Jumla ya shilingi milioni 84.1 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(e) Mradi wa Kiwanda cha Viuadudu (TBPL)
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa jaribio la pili la viwatilifu; kuendelea na ujenzi wa barabara ya ndani (Viuatilifu Road) yenye urefu wa mita 230 ambapo ujenzi umefikia asilimia 75. Jumla ya shilingi bilioni 1.24 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(f) Mradi wa Makaa ya Mawe wa Katewaka
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa uthaminishaji wa mali za waathirika 689 wa mradi wa makaa ya mawe Katewaka katika Kijiji cha Nkomang’ombe katika Kitongoji cha Nyambalapi na Mhumbi. Jumla ya shilingi milioni 357.1 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(g) Kufanya Maandalizi ya Uchimbaji wa Chuma Ghafi (iron ore) Maganga Matitu
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa uthaminishaji na uhakiki wa mali za wananchi 381 wanaopisha mradi na maandalizi ya vitabu vya taarifa ya uthaminishaji yanaendelea. Jumla ya shilingi milioni 179.2 zimetumika hadi kufikia mwezi Aprili, 2023.
(h) Kituo cha Zana za Kilimo na Ufundi Vijijini - CAMARTEC
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa Kiwanda Darasa cha kubangua Korosho katika Wilaya ya Manyoni mkoani Singida kwa kuandaa vifaa na mashine 129; kuanza ujenzi wa Kitivo cha Teknolojia za Kihandisi (KITEKI) wilaya ya Karatu mkoani Arusha kwa kuandaa jumla ya mashine 49 na zana nyingine za kilimo; kufanyika kwa utafiti wa kubaini mahitaji na matumizi ya zana za kilimo, mifugo, uvuvi na teknolojia za vijijini katika Mikoa ya Songwe (Momba), Dodoma (Chemba) na Arusha (Karatu); kufanyika kwa ukarabati wa majengo mawili ya Utawala (Block A na Block B) na nyumba mbili zilizopo katika Kiwanja Na.18 Themi Hill na Kiwanja Na. 83 Kanisa Road (Uzunguni); ununuzi wa mashine tatu (3) kwa ajili ya Karakana ya kituo (mashine 2 za kuchomelea na Gen Set 1 ya kufua umeme). Jumla ya shilingi milioni 873.75 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(i) Shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania - TIRDO
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa zoezi la ukusanyaji wa taarifa za tathmini ya viwanda na kuainisha fursa za uwekezaji katika Kanda ya Kaskazini; kuendelea na ujenzi wa jengo la utawala ili kutoa nafasi ya kuanzisha kituo cha Taarifa za Viwanda na Ubashari wa teknolojia na viatamizi kwa wabunifu wa teknolojia ambapo ujenzi umefikia asilimia 45; kukamilika kwa ununuzi wa vifaa vya upimaji ubora bila kuharibu (Non Destructive Testing - NDT) wa mabomba ya mafuta na gesi ili kuendelea kukidhi viwango vya kimataifa. Jumla ya shilingi milioni 856.13 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(j) Shirika la Uhandisi na Usanifu wa Mitambo – TEMDO
Hatua iliyofikiwa ni: Kufanyika kwa unakili na kufanya maboresho ya mchoro wa mtambo wa kuchakata mkonge uliopo Tanga; kuendelea na utafiti wa teknolojia ya kutengeneza matofali yanayohimili joto kali kwa awamu ya pili; kukamilika kwa mitambo midogo minne (4) ya sukari; kuendelea na utengenezaji wa Mtambo wa kutengeneza sukari kwa kiwango cha mjasiriamali wa kati (sugar mini-plant, Capacity 200TCD); kuendelea na maboresho ya karakana kwa kuweka mfumo wa upepo na umeme kwenye mashine ya kupaka rangi (painting booth); kuendelea na usanifu na utengenezaji wa vifaa tiba (vitanda, drip stand, examination bed, delivery bed, hospital screens, bed side lockers, biomedical waste incinerators, 6-body Mortuary cabinets na milango ya kuzuia mionzi). Jumla ya shilingi milioni 998.00 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(k) Uendelezaji wa Viwanda Vidogo (SIDO)
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa michoro ya majengo ya viwanda (industrial sheds) katika Mkoa wa Iringa na ukarabati katika Mikoa ya Dar es Salaam, Mbeya, Arusha, Tabora na kumalizia jengo la Nyasa Mkoa wa Ruvuma; kukamilika kwa ujenzi wa jengo la kiwanda Tanga na kuendelea ujenzi wa majengo ya viwanda katika mikoa ya Singida - Manyoni (1), Shinyanga – Kahama (2) na Geita - Chato (2); kuandaliwa kwa vipimo vya Mashine ya kukeleza vyuma, kukata na kukunja mabati, kuchomelea na kukata vyuma kwa ajili ya kuimarisha Kituo cha Uendelezaji Teknolojia (TDCs) katika mkoa wa Arusha; kusimikwa kwa mashine ya kukeleza vyuma, kukata na kukunja mabati, kuchomelea na kukata vyuma kwa ajili ya kuimarisha vituo vya Uendelezaji Teknolojia katika Mikoa ya Kilimanjaro na Mbeya; kuzalishwa kwa mashine 228 na vipuli 1,374 za aina mbalimbali kupitia Vituo saba (7) vya kuendeleza Teknolojia (TDCs) kwa ajili ya viwanda vidogo; na kutolewa mafunzo kwa wafanyakazi wa SIDO kuhusu utumiaji wa mfumo wa ofisi mtandao. Jumla ya shilingi bilioni 1.60 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(l) Mchango wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii Katika Uchumi wa Viwanda
Kilimanjaro International Leather Industries Co Ltd (KLICL)
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na awamu ya pili ya ujenzi wa kiwanda cha kuchakata ngozi ambapo utekelezaji umefikia asilimia 45, maabara na kantini (asilimia 99), Jengo la Jenereta (asilimia 99) na barabara za ndani na mitaro ya maji ya mvua (asilimia 50) ambapo utekelezaji wa jumla wa mradi umefikia asilimia 95; na kuendelea na ujenzi wa miundombinu wezeshi ikiwemo maji taka, barabara za ndani na uzio katika kiwanda cha ngozi. Jumla ya shilingi bilioni 122 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023
Kiwanda cha Nyama cha Nguru Hills Ranch - Morogoro
Hatua iliyofikiwa ni: kukamilika kwa ukarabati wa majengo, mifumo ya umeme na maji, majokofu ya upoozaji, uunganishaji wa umeme mkubwa na ufungaji wa mashine pamoja na majaribio ya mashine na mifumo ya uendeshaji. Jumla ya shilingi bilioni 20.35 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
Kiwanda cha Kuchakata Tangawizi cha ‘Mamba Ginger Factory Limited
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ukarabati wa majengo ya kiwanda; unganishaji wa umeme mkubwa na ufungaji wa mashine, majaribio ya mashine na mifumo ya uendeshaji. Jumla ya shilingi bilioni 1.782 katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
Kiwanda cha Chai cha Mponde - Tanga
Hatua iliyofikiwa ni: kukamilika kwa ukarabati wa majengo, mitambo, mifumo ya umeme na maji pamoja na majaribio ya mitambo. Jumla ya shilingi milioni 500 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(v) Mradi Na. 4933: Uendelezaji wa Kanda Maalumu za Kiuchumi
Eneo Maalumu la Uwekezaji Mtwara Free Port Zone
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ujenzi wa miundombinu ya maji, umeme na barabara za ndani ya eneo la mradi zenye urefu wa km 1.06; na kukamilika kwa usanifu wa jengo la Kituo cha Pamoja cha Huduma (One Stop Center Building).
2.3.3.2. Ubiasharishaji wa Mazao ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kupitia ASDP II
A. Kilimo
(a) Mradi Na. 4486: Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili - ASDP II
(i) Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Umwagiliaji
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa skimu mpya 19 zenye ukubwa wa hekta 45,564 katika mikoa ya Mbeya, Iringa, Dodoma, Mwanza, Tabora, Morogoro, Kilimanjaro, Manyara, Shinyanga, Mara, Simiyu na Rukwa; kuendela na ukarabati wa skimu 19 zenye ukubwa wa hekta 13,243 katika mikoa ya Mbeya, Iringa, Mwanza, Katavi, Ruvuma, Tanga, Morogoro, Kilimanjaro, Manyara na Tabora; na kuendelea na ujenzi wa mabwawa 10 yenye jumla ya mita za ujazo 122,545,000 ya katika mikoa ya Dodoma, Tabora, Mwanza, Shinyanya, Manyara, Singida na Rukwa. Aidha, jumla ya ajira 298,635 zimezalishwa katika miradi hii. Jumla ya shilingi bilioni 96.43 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(ii) Kuwezesha Uanzishwaji wa Mashamba Makubwa ili kuwa Kitovu Cha Teknolojia Bora kwa Wakulima Wadogo
Hatua iliyofikiwa ni: Kubainisha mashamba makubwa (Block farms) yenye ukubwa wa ekari 264,841.50 kwa ajili ya vijana katika Mikoa ya Kigoma Kigoma (ekari 36,719.75) Mbeya (ekari 52,165), Njombe (ekari 87,000), Dodoma (ekari 33,4543), Singida (ekari 50,000) na Kagera (ekari 5,503.75); kupimwa kwa afya ya udongo wa mashamba hayo na kusafishwa kwa hekta 520 za shamba la Mlazo-Ndogowe; kusafishwa kwa Shamba la Chinangali lenye ukubwa wa hekta 160 kwa ajili ya uwekezaji; kusafishwa kwa mashamba yenye ukubwa wa ekari 77.8 katika Kituo na Vyuo vya Bihawana (ekari 22), Mlingano (ekari 4), Uyole (ekari 3), Mubondo (ekari 10), Ukiriguru (ekari 8.9), NSI - Kidatu (ekari 2.4), Horti Tengeru (ekari 4), Mtwara (ekari 10), Ilonga (ekari 3.5) na Tumbi (ekari 10); na kudahiliwa kwa vijana 4,000 kwa ajili ya kupewa mafunzo katika vyuo vya kilimo kuanzia mwezi Machi, 2023 kabla ya kupewa ardhi ya kilimo. Jumla ya shilingi bilioni 3.0 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(iii) Kuimarisha Vituo vya Utafiti na Utafiti wa Mbegu Bora
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa Ofisi za TARI Makao Makuu - Dodoma ambapo utekelezaji umefikia asilimia 41; kuendelea na ujenzi wa Kituo cha TARI Kihinga – Kigoma ambapo utekelezaji umefikia asilimia 68; kuanza kwa ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji kwenye jumla ya hekta 854 za vituo 16 vya utafiti; kujenga ghala tano (5) zenye vyumba vya ubaridi (cold rooms) zenye uwezo wa kuhifadhi tani 2,075 za mbegu katika vituo vya TARI Selian, Hombolo, Tumbi, Naliendele na Dakawa umefikia asilimia 20; kuanza ujenzi wa uzio katika eneo la kituo cha TARI Uyole lenye hekta 1,042; kununua vifaa na vitendanishi vya maabara ya udongo na bioteknolojia za TARI Mlingano na TARI Mikocheni; kufanya ugunduzi wa teknolojia mbalimbali kwa kukamilisha mapendekezo ya kupitisha aina 15 za mbegu mpya kwa Kamati ya Kitaalam ya Mbegu ambapo mbegu saba (7) ni za maharage, 3 za mtama, 5 za zabibu, na 2 za zao la migomba; kutunza vinasaba 33,332 vya mazao ya mpunga (729), mtama (416), uwele (105), ulezi (3), alizeti (39), zabibu (26), migomba (128), maharage (10), muhogo (20), korosho (30,000), pamba (328), mahindi (250), viazi vitamu (6), miwa (107), minazi (7), michikichi (3), mkonge (60), na kakao (17) kwa ajili ya utafiti na uhifadhi wa mbegu za asili. Jumla ya shilingi bilioni 15.65 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(iv) Kuimarisha Huduma za Ugani, Vyuo vya Mafunzo ya Kilimo na Vituo vya Mafunzo ya Wakulima
(a) Ukarabati wa Vyuo vya Kilimo na Vituo vya Mafunzo ya Wakulima
Hatua iliyofikiwa ni: Kudahiliwa kwa wanafunzi 3,151 wa mwaka wa kwanza na wa pili katika vyuo 14 vya mafunzo ya kilimo; kutoa huduma ya chakula kwa wanafunzi wa vyuo 14 vya mafunzo ya kilimo; na kuendelea na ukarabati wa miundombinu katika vyuo vya Kilimo Tumbi, Igurusi, Ilonga na National Sugar Institute. Jumla ya shilingi bilioni 7.14 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(b) Kuimarisha Huduma za Ugani
Hatua iliyofikiwa ni: Kuboresha mazingira ya utoaji huduma kwa kununua na kusambaza pikipiki 5,889 kwa maafisa ugani katika mikoa 25; kununua na kusambaza viti 1,020 na meza 23 katika Vituo vitano (5) vya Rasilimali za Kilimo vya Kata (WARCs) nane (8) katika mikoa ya Dodoma, Singida na Simiyu; kutoa mafunzo kwa maafisa ugani 142 wa Halmashauri 142 kutoka katika mikoa 25 kuhusu matumizi ya vifaa vya kupima afya ya udongo; na kutoa mafunzo kwa maafisa ugani 203 kuhusu kilimo biashara na matumizi ya mfumo kwa kutumia simu ya mkononi (M – Kilimo). Jumla ya shilingi bilioni 12.78 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(v) Kuongeza Tija na Uzalishaji
(a) Upatikanaji wa Mbegu Bora
Hatua iliyofikiwa ni: Kuzalishwa na kusambazwa tani 1,004 za mbegu bora za Alizeti kwa wakulima kwa bei ya ruzuku katika wilaya 39 za mikoa ya Dodoma, Kagera, Mbeya, Mwanza na Singida. Kati ya kiasi hicho, tani 300 zimezalishwa na Sekta Binafsi; kuzalisha miche 170,924 ya parachichi na miche 394,000 ya chikichi; kuendelea na ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji katika shamba la Kilimi (Nzega) lenye ukubwa wa hekta 400, Arusha (hekta 200) na Msimba (Kilosa) hekta 200 ambapo utekelezaji umefikia asilimia 25.0; kukamilika kwa upimaji wa maji (geological survey) na kutambua maeneo sita (6) ya kuchimba visima katika shamba la Arusha; kukamilika kwa uchimbaji wa visima virefu sita (6) katika shamba la mbegu la Msimba; kuongeza eneo jipya la hekta 1,300 kwa ajili ya kuzalisha mbegu bora katika mashamba ya Kilimi - Nzega (hekta 300), Msimba - Kilosa (hekta 400), Mwele - Tanga (hekta 300) na Namtumbo - Ruvuma (hekta 300); kuendelea na ukarabati wa ghala la kuhifadhi mbegu la msimba ambao umefikia asilimia 90 na usimikaji wa mtambo mpya wenye uwezo wa kuchakata tani tatu (3) za mbegu kwa saa katika ghala hilo umefikia asilimia 85; ununuzi wa matrekta sita (6) na zana zake kwa ajili ya mashamba ya Msungura, Namtumbo, Msimba, Dabaga, Mbozi na Kilimi na ununuzi wa magari matatu (3) ya kusambaza mbegu. Jumla ya shilingi bilioni 19.68 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(b) Upatikanaji wa Mbolea ya Ruzuku
Hatua iliyofikiwa ni: Kutolewa kwa ruzuku ya mbolea tani 449,795 na kusambazwa kwa wakulima katika maeneo mbalimbali nchini; kufanyika kwa usajili wa waingizaji wakubwa wa mbolea 28, mawakala wadogo 3,265 pamoja na wazalishaji wa ndani watatu (3) wa mbolea katika mfumo wa kielektroniki; na kufanyika kwa usajili wa wakulima 3,020,621 kwenye mfumo wa kielektroniki. Jumla ya shilingi bilioni 214.8 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(c) Upatikanaji wa Viuatilifu
Hatua iliyofikiwa ni: Kununuliwa kwa viuatilifu lita 106,000 za kudhibiti visumbufu vya milipuko ya viwavijeshi na lita 82,124 zimesambazwa katika Halmashauri 58 za Mikoa ya Manyara, Singida, Tabora, Katavi, Tanga, Geita, Simiyu, Shinyanga, Ruvuma, Kilimanjaro, Arusha na Dodoma; kununuliwa kwa kilo 2,000 za viuatilifu vya kudhibiti panya katika mikoa ya Morogoro, Mtwara na Lindi pamoja na lita 300 kwa ajili ya kudhibiti nzi wa matunda katika mikoa ya Tanga, Dar es Salaam na Mwanza; kutoa mafunzo ya matumizi salama na sahihi ya viuatilifu kwa wakulima, wafanyabiashara, maafisa ugani, na wanyunyiziaji katika Kanda ya ziwa (Mwanza na Mara), Kanda ya nyanda za juu kusini (Mbeya na Iringa), Kanda ya mashiriki (Morogoro), Kanda ya kusini (Lindi na Mtwara) na Kanda ya kaskazini (Arusha). Jumla ya shilingi bilioni 34.57 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(vi) Kuimarisha Miundombinu ya Kuhifadhi Mazao ya Kilimo
Hatua iliyofikiwa ni Kuendelea na ukarabati wa ghala tano (5) ambapo utekelezaji katika ghala la Litisha umefikia asilimia 97.67, Lipaya (asilimia 21.58), Liula (asilimia 36.62), Hangangadinda (asilimia 57.80) na Lilondo A (asilimia 33.32) katika halmashauri za Songea na Madaba. Jumla ya shilingi milioni 67.74 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(vii) Upatikanaji wa Masoko ya Mazao ya Kilimo Ndani na Nje ya Nchi Hatua iliyofikiwa ni: Kuwezesha Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula - NFRA kununua mahindi tani 17,257.857 na mtama tani 1,036.457 na Bodi ya Mazao Mchanganyiko – CPB kununua mahindi tani 34,484, alizeti tani 2,776, mafuta ghafi tani 85.82, mchele tani 1,797, ngano tani 277, maharage tani 406, mtama tani 3,035.06, maharage ya soya tani 393, maharage ya njano tani 30, korosho ghafi 523, na mpunga tani 7,065; na kuendelea na maandalizi ya kuanzisha mnada wa chai kwa njia ya mtandao ambapo utekelezaji wake umefikia asilimia 9. Jumla ya shilingi bilioni 17.31 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(viii) Kuboresha Mifumo ya Kitaasisi, Bodi na Sheria
(a) Mifumo ya Kielektroniki ya kutoa huduma katika Sekta ya Kilimo Hatua iliyofikiwa ni: Kuanza kutumika kwa Mfumo wa M-Kilimo kwa kutoa huduma ya ushauri wa kilimo bora cha mazao mbalimbali ikiwemo kujibu kero zinazohusu utoaji wa mbolea ya ruzuku kwa wadau wa kilimo 4,548; kusajiliwa kwa wakulima 3,050,621 katika Mfumo wa Kielektroniki wa utoaji wa mbolea ya ruzuku; kuendelea na matumizi ya mfumo wa kutoa huduma za biashara ya mazao (Agriculture Trade Management Information System - ATMIS) ambapo jumla ya wakulima 500 wamesajiliwa na kupata huduma.
(b) Kuimarisha Mifumo ya Upatikanaji wa Mitaji katika Sekta ya Kilimo Hatua iliyofikiwa ni: Kuanzishwa kwa Mfuko wa Maendeleo ya Kilimo; kupungua kwa riba ya mkopo kwa wakulima na kuwa chini ya asilimia 10; kukamilika kwa mapitio ya sera ya mikopo katika mifuko ya pembejeo ambapo hatua za uidhinishwaji zinaendelea na Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) imetoa mikopo ya moja kwa moja (direct lending). Jumla ya shilingi milioni 17 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(ix) Kuimarisha Usimamizi wa Maendeleo ya Ushirika
Hatua iliyofikiwa ni: kukamilika kwa ujenzi wa kiwanda cha TANECU (Newala) cha kubangua korosho chenye uwezo wa kubangua tani 3,500 za korosho kwa mwaka; na kusajiliwa kwa vyama viwili (2) vya ushirika katika vikundi vidogo vya wakulima 120 wa mazao ya mboga na matunda katika mikoa ya Arusha, Mbeya na Njombe. Jumla ya shilingi bilioni 6.3 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(b) Mradi Na. 4499: Kudhibiti Sumukuvu
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa ghala 14 katika mikoa 10 ya Kigoma, Mtwara, Dodoma, Mwanza, Ruvuma, Tabora, Manyara, Geita, Simiyu na Morogoro yenye uwezo wa kuhifadhi tani 21,500 za mahindi na karanga ambapo utekelezaji umefikia wastani wa asilimia 94; kuendelea na ujenzi wa Kituo Mahili cha Usimamizi wa Mazao ya Nafaka (Postharvest Centre of Excellence for Grains) katika Wilaya ya Kongwa ambapo utekelezaji umefikia asilimia 70; kuendelea na ujenzi wa Maabara ya Utafiti wa Magonjwa ya Mimea (Biological Control Unit) Kibaha mkoani Pwani ambapo umefikia asilimia 99; kutoa mafunzo kwa vijana 420 kupitia Chuo cha Mafunzo ya Ufundistadi (VETA) kuhusu utengenezaji wa vihenge vya chuma kwa ajili ya kuhifadhi mazao vijijini; kutoa mafunzo kwa wakulima 60,000 na wafanyabiashara 500 kuhusu udhibiti wa Sumukuvu. Jumla ya shilingi bilioni 17.0 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(c) Mradi Na. 4497: Kuongeza Uhifadhi wa Nafaka
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ujenzi wa vihenge (20) na maghala (4) katika wilaya za Babati, Mpanda na Sumbawanga; kuendelea na ujenzi wa vihenge 36 na ghala nne (4) kwa ajili ya kuongeza uwezo wa kuhifadhi mazao kufikia tani 501,000 katika vituo vya Makambako, Mbozi, Songea, Shinyanga na Dodoma ambapo umefikia wastani wa asilimia 85. Jumla ya shilingi milioni 647.7 fedha za ndani na shilingi bilioni 2.378 fedha za nje zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(d) Mradi Na. 4427: Kuendeleza Kilimo na Uvuvi - AFDP
Hatua iliyofikiwa: Kutolewa kwa mafunzo maalum ya kisayansi ya muda mfupi kwa watafiti 21 (breeders) kuhusu teknolojia ya mbegu kwenye mazao ya mahindi, maharage, alizeti na kunde; kukamilika kwa EIA katika miradi ya ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji katika mashamba ya Msimba (Kilosa), Kilimi (Nzega); ujenzi wa maabara ya mbegu katika mkoa wa Morogoro na katika mashamba ya utafiti ya TARI; na kufanyika kwa usanifu wa ujenzi wa ofisi na ukumbi wa mafunzo, ghala za kuhifadhi mbegu, karakana na nyumba za wafanyakazi katika shamba la Kilimi (Nzega) na Msimba (Kilosa). Jumla ya shilingi bilioni 2.05 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
B. Mifugo
Mradi Na. 4486: Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili
(ASDP II)
(i) Kuimarisha Afya ya Mifugo
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ujenzi wa majosho 97 na kuendelea na ujenzi wa majosho 160 kwenye mamlaka 83 za serikali za mitaa; kununuliwa kwa lita 52,560 za dawa ya kuogesha mifugo kwa ajili ya majosho 2644 na kusambazwa katika mikoa 25 ya Tanzania Bara kwenye mashamba ya Wizara na Taasisi zake; kuwezesha upatikanaji na usambazaji wa chanjo za mifugo dozi 679,827,610 za magojwa mbalimbali ya kipaumbele zikiwemo dozi 160,584,610 zilizozalishwa nchini na kuingizwa jumla ya dozi 519,243,000 kutoka nje ya nchi; kufanyika kwa michovyo 1,040,762,493 (ng’ombe ni 500,572,121 mbuzi 223,982,134, kondoo 250,774,038 na Punda 65,434,200) ya kuogesha mifugo ikilinganishwa na michovyo 446,997,857 iliyofanyika katika kipindi kama hicho mwaka 2022; Jumla ya shilingi bilioni 8.23 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023
(ii) Kuimarisha Huduma za Ugani
Hatua iliyofikiwa ni: Ununuzi wa magari 13 kwa ajili ya uratibu wa ugani na pikipiki 1200 kwa ajili ya kurahisisha utoaji wa huduma za ugani katika Mamlaka za Serikali za Mitaa 184; kupatiwa mafunzo rejea kwa jumla ya maafisa ugani 515 ambapo 487 wa sekta ya umma na 28 wa sekta binafsi kutoka Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka ya Serikali za Mitaa katika kanda zote nane (8) nchini za ambapo jumla ya Halmashauri 119 zimefikiwa; kusajiliwa kwa maafisa ugani 3,018 kati ya 3,201 katika mfumo wa TEHAMA wa utoaji wa huduma za Ugani wa M- Kilimo; na kuendelea na taratibu za uanzishaji wa mashamba darasa ambapo tararibu za ujenzi na ununuzi wa vifaranga 18,000,000 kwa mashamba darasa matano (5) ya ufugaji kuku imefanyika katika Mikoa ya Ruvuma (Songea MC – 3) na Shinyanga (Kishapu - 2) kwa ajili ya vikundi vya wanawake vinavyojishughulisha na ufugaji wa kuku.
Shughuli nyingine zilizotekelezwa ni: kukamilika kwa ujenzi wa mabanda 24 kwa ajili ya unenepeshaji wa mifugo katika Vituo Atamizi vya Uwekezaji vya Vijana vya Mabuki (9); Buhuri Tanga (6); TALIRI Tanga (3) na Kikulula (6); kukamilika kwa ujenzi wa zisima viwili (2) vya maji na miundombinu ambata katika Kituo cha TALIRI Tanga na Mabuki, kuandaliwa kwa shamba lenye ukubwa wa ekari 56 la malisho bora kwa ajili ya unenepeshaji wa mifugo katika Vituo Atamizi; na kununuliwa kwa ng’ombe 2,222 kwa ajili ya utekelezaj wa vituo 8 vya vijana na wanawake 238 vya unenepeshaji wa ng'ombe kwa ajili ya kuuza katika viwanda vya kusindika nyama. Jumla ya shilingi bilioni 8.1 zimetumika hadi Aprili 2023.
(iii) Kuimarisha Huduma za Tafiti
Hatua iliyofikiwa ni: Kununuliwa kwa vifaa shamba vikiwemo matrekta (4), disc plough (3), harrow (2), bailer (1) na forage chopper (1) kwa ajili ya kuwezesha utafiti wa mifugo hususan utafiti wa malisho na kusambazwa katika Vituo vya Utafiti vya TALIRI Tanga, Kongwa, Mabuki, Uyole na Mpwapwa; na kununuliwa kwa mbuzi 2070 aina ya Newala (200) Boers (70), Pare White (225), Gogo White (900), Galla (225) na Sukuma (450) kwa ajili ya shughuli za kitafiti katika vituo vya utafiti wa mifugo; kuanzishwa kwa vituo nane (8) vya uwekezaji vya vijana vyenye uwezo wa kuchukua jumla ya vijana 240 kwa mwaka kwa lengo la kuwawezesha vijana kupata uzoefu katika kuanzisha na kuendeshammiradi ya ufugaji kibiashara, ambapo jumla ya vijana 238 wamesajiliwa katika vituo Atamizi vya LITA na TALIRI; Jumla ya shilingi milioni 800.7 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023
(iv) Uboreshaji wa Mbari kwa ajili ya Uzalishaji wa Maziwa na Nyama
Hatua iliyofikiwa ni: kununuliwa kwa ng’ombe wazazi 1,160 na kusambazwa katika Mashamba ya Serikali ya kuzalisha mitamba ya Mabuki (500), Sao Hill (307) na Kitulo (160); kununuliwa kwa madume bora 366 ya ng’ombe na kusambazwa kwa wafugaji kupitia vikundi vya wafugaji katika Halmashauri saba (7) za Chamwino
(50), Msalala (50), Maswa (50), Chato (50), Mvomero (40),Mkuranga (50), Buchosa (36) na Mkalama (40); na kuzalishwa kwa mitamba 606 na kuongezwa kwenye kundi la ng’ombe wazazi katika mashamba ya Serikali ya kuzalisha mitamba; Kuzalishwa kwa jumla ya dozi 116,558 za mbegu za mifugo katika kituo cha NAIC kwa ajili ya uhimilishaji; kununuliwa kwa Kimiminika cha Hewa Baridi ya Naitojeni lita 7,000 kwa ajili ya uhimilishaji ng’ombe katika kituo cha NAIC; kununuliwa kwa matrekta 3, Bailer 5, mower 5 na Hay rake 5 na kusambazwa katika mashamba ya Serikali ya kuzalisha mitamba kwa ajili ya kuzalisha na kuvuna malisho; kununuliwa kwa dozi 115,000 za vichochezi vya joto kwa ng’ombe ili kutekeleza shughuli za uhimilishaji katika kambi na kununuliwa kwa hereni 150,000 kwa ajili ya kuwavalisha ng’ombe watakao himilishwa katika kambi; kuhimilisha ng’ombe 60,697 kupitia kambi za uhimilishaji. Jumla ya shilingi bilioni 6.9 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(v) Kuimarisha Miundombinu ya Masoko ya Mifugo na Mazao Yake
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa minada minne (4) ya upili ya Mkongeni – Morogoro (70%), Majimoto - Katavi (10%), Utengule – Mbeya (40%) na Lugodalutale – Iringa (40%); kuendelea na ujenzi wa mnada mmoja (1) wa mpakani wa Randa – Mara (20%); na kuendelea na ujenzi wa vituo 10 vya kukusanyia maziwa vya Kwemakame (65%) na Msomera (80%) – Tanga, Malimbika - Dar es Salaam (80%), Magogoni – Morogoro (40%), Lukani – Kilimanjaro (60%), Ngaramtoni – Arusha (60%), Komunge – Mara (27%), Maswa – Simiyu (15%), Karagwe – Kagera (60%) na Mkambako – Njombe (65%).
Shughuli nyingine zilizotekelezwa ni: Ukarabati wa minada miwili (2) ya upili ya Weruweru – Kilimanjaro (98%) na Meserani (98%), ukarabati wa minada miwili (2) ya awali ya Nyanguge (98%) na Buhungulwa – Mwanza (98%); kuendelea na ujenzi wa minada 12 ya awali ya Msomera – Tanga (97%), Lupa – Mbeya (96%), , Kibinda – Simiyu (98%), Nzoka – Songwe (98%), Kilyamatundu – Rukwa (50%), Sikonge (97%) na Urambo (97%) – Tabora na Bukombe (45%) na Kasamwa (40%) – Geita Gwandi (45 %) na Huzi ( 20%) – Dodoma na Kitinku – Singida (20%); kuendelea na ujenzi wa minada miwili (2) ya upili ya Mhunze – Shinyanga (98%) na Wasso – Arusha (75%); na kununuliwa kwa mizani 82 kusambazwa na kuisimikwa katika minada ya awali, upili na mpakani. Jumla ya shilingi bilioni 3.1 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(vi) Kuimarisha Unywaji wa Maziwa Shuleni
Hatua iliyofikiwa ni: kuendelea na utekelezaji wa Mpango wa Unywaji Maziwa Shuleni ambapo idadi ya shule za msingi zinazoshiriki ziliongezeka kutoka 39 hadi shule 130 na idadi ya shule za sekondari nne (4) zimejiunga na mpango huo na kufanya jumla ya shule zote nchini zinazoshiriki mpango huo kufikia 134; kuongezeka kwa vituo vya kuuzia maziwa katika Ofisi za Serikali kutoka vituo 10 na kufikia vituo 18 katika Mikoa ya Dodoma (9), Mbeya (4), Katavi (1), Tanga (1) na Dar es salaam (3). Jumla ya shilingi milioni 56.1 fedha za nje zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023
(vii) Kuimarisha Huduma za Maji, Malisho na Vyakula vya Mifugo
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ujenzi wa mabwawa ya Kimambi na Matekwe – Lindi, na Mhanga (Singida); kukamilika kwa uchimbaji wa kisima cha Matanzi (Pwani), Makatapola (Iringa) na Lwami (Kilimanjaro); kununuliwa kwa Mowers tatu (3), Bailers mbili (2), Hay rakes mbili (2), Desktop Computers nne (4) na Printers mbili (2) na kusambazwa katika mashamba mawili ya Serikali ya kuzalisha mbegu za malisho na malisho ya Vikuge (Kibaha) na Langwira (Mbalali); na kukabidhiwa kwa Mkandarasi wa kusafisha maeneo kwa ajili ya kupanda malisho hekta 175 katika shamba la kuzalisha malisho na mbegu za malisho la Vikuge.
Shughuli nyingine zilizotekelezwa ni: kuendelea na ujenzi wa mabwawa 11 ya
Oloirieni (10%) na Naalaram (90%) – Arusha, Kwekikwembe (35%) na Msomera (35%) – Tanga, Kongwa – Morogoro (10%), Vinyenze – Pwani (10%), Chang’ombe – Mbeya (10%), Kihumbo (20%) na Bukabwa (10%) – Mara, na Kaiwang (05%) na Leralumo (05%) – Manyara na Msaginia – Katavi (60%); kuendelea na uchimbaji wa kisima cha Muhukulu Lilai (Ruvuma) (80%), Kitaraka – Singida (5%), Kapele - Kasinde – Songwe ( 5%) na Maswa – Simiyu (70%); kuingiza umeme na kuendelea na ujenzi wa mfereji wa umwagiliaji ambapo ujenzi umefikia asilima 80 katika shamba la kuzalisha malisho na mbegu za malisho la Langwira; kununuliwa kwa tani 8.56 (Rhodes na Buffel tani 6.105, Juncao tani 2.45) za mbegu za malisho na vipando vya miti malisho 18,025 kutoka mashamba ya Serikali na binafsi na kusambazwa kwa wafugaji kwa vikundi vya uanzishwaji wa mashamba darasa 100 yenye ukubwa wa ekari 520 katika Mamlaka za Serikali za Mitaa 44. Jumla ya shilingi bilioni 1.5 zimetumika katika kipindi cha Julai hadi Aprili 2023.
(viii) Kuboresha Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa kumbi mbili (4) za mihadhara zenye uwezo kuchukua wanafunzi 250 kila moja katika kampasi za Mpwapwa (1), Morogoro (1) na Mabuki (2) ambapo ujenzi umefikia asilimia 30; kuendelea na ujenzi wa hosteli mbili (2) zenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 216 kila moja katika kampasi za Morogoro na Mpwapwa ambapo ujenzi umefikia asilimia 30; na kufungwa kwa samani katika kumbi mbili (2) za mihadhara katika Kampasi ya Tengeru. Jumla ya shilingi milioni 400 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
C. Uvuvi
(a) Mradi Na. 4701: Mradi wa Kikanda wa Usimamizi Shirikishi wa Rasilimali za Uvuvi Kusini Magharibi mwa Bahari ya Hindi – (South West Indian Ocean Fisheries Governance and Shared Growth – SWIOFish)
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ujenzi wa Maabara ya Utafiti wa Uvuvi katika kituo cha TAFIRI - Dar es Salaam; na kuendelea na ujenzi wa jengo la utawala la ofisi ya Hifadhi ya Bahari na Maeneo Tengefu - Mafia ambapo ujenzi umefikia asilimia 90; kuendelea na ujenzi wa awamu ya kwanza ya Kituo cha Ukuzaji Viumbe Maji Bahari – Kunduchi, Dar es Salaam na ununuzi wa samani za ofisi za maabara ya TAFIRI – Dar es Salaam. Jumla ya shilingi bilioni 3.49 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(b) Mradi Na. 4486: Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo (ASDP II)
(i) Kuimarisha na Kuendeleza Ulinzi wa Rasilimali za Uvuvi na Mazingira
Hatua iliyofikiwa ni: kufanyika kwa kaguzi za jumla ya siku kazi 4,743 za operesheni maalum na doria ambazo ni sawa na asilimia 60.8 ya lengo la mwaka la siku kazi 7,800 katika Ziwa Victoria,Tanganyika, Nyasa na Bahari ya Hindi;; kujengwa na kupatiwa samani kwa Ofisi ya Maeneo ya Pamoja ya Usimamizi wa Uvuvi (CFMA) katika Kijiji cha Karema, Wilaya ya Tanganyika (Katavi); kukamilika kwa ujenzi wa ofisi moja (1) ya ulinzi na usimamizi wa rasilimali za uvuvi ya Busega (Simiyu); kuendelea na ujenzi wa ofisi mbili (2) za ulinzi na usimamizi wa rasilimali za uvuvi za Nyakalilo (Sengerema) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 60 na Sota – Rorya (asilimia 50); na kununuliwa kwa pikipiki 50 za maafisa ugani wa uvuvi kwa ajili ya kuimarisha ulinzi na usimamizi wa rasilimali za uvuvi. Jumla ya shilingi milioni 785.0 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(ii) Kujenga na Kuimarisha Miundombinu ya Uvuvi (Mialo na Masoko)
Hatua iliyofikiwa ni: kuendelea na ujenzi ya mialo miwili (2) ya Chifunfu/Kijiweni (Sengerema) na Igabiro (Bukoba) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 90 kwa kila mwalo; kuendelea na usanifu wa ujenzi wa soko la Tunduma (Momba); kuendelea na ujenzi wa mashamba darasa mawili (2) kwa lengo la kutoa huduma za ugani katika Halmashauri za Moshi na Mwanga. Jumla ya shilingi 245.3 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(iii) Kuimarisha Wakala wa Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA)
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ukarabati mdogo wa nyumba tatu (3) za wafanyakazi katika Kampasi ya Nyegezi (Mwanza) na Mbegani (Bagamoyo); kuendelea na ujenzi wa kumbi mbili (2) za mihadhara katika Kampasi ya Nyegezi (Mwanza) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 75, ujenzi wa maabara umefikia asilimia 60 na ukarabati wa kitotoleshi katika Kampasi ya Gabimori – Mara (asilimia 15) na ujenzi wa maabara katika Kampasi ya Mikindani – Mtwara (asilimia 40); Jumla ya shilingi milioni 217.4 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(iv) Kuimarisha Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI)
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa utafiti wa uwingi, bioanuwai na mtawanyiko wa samaki katika Ziwa Tanganyika ambapo jumla ya aina 7 za samaki na sampuli 639 zilikusanywa na kusafirishwa kwenda Uingereza; kufanya utafiti wa majaribio ya matumizi ya mitego/vyungu katika uvuvi wa pweza Tanzania ili kuwezesha uvuvi endelevu wa pweza; kufanya utafiti wa kufuatilia ongezeko la tindikali baharini (ocean acidification) na aina za kaboni (sea water carbonate species) katika maji ya Pwani ya Tanzania. Jumla ya shilingi milioni 599.2 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(c) Mradi Na. 4486: Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo (ASDP II ) na Mradi Na. 4429: Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi
Kujenga na Kukarabati Miundombinu ya Ukuzaji Viumbe Maji
Hatua iliyofikiwa ni: kukamilika kwa ukarabati wa mabwawa makubwa matatu (3) na madogo sita (6) kwa kuotesha nyasi na kujenga mifumo ya kuingiza na kutoa maji katika Kituo cha Rubambagwe (Geita); kukamilika kwa matanki ya maabara (Lab tank), nursery ponds, reservoir na tower pamoja na kuendelea na ujenzi wa Kitotoleshi ambapo utekelezaji umefikia asilimia 60 katika kituo cha kuendeleza Ukuzaji Viumbe Maji Bahari Ruvula – Mtwara; kuendelea na upanuzi wa kituo cha ukuzaji viumbe maji na ujenzi wa ghala moja (1) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 60; kuendelea na ujenzi wa Kitotoleshi cha vifaranga vya samaki na upanuzi wa kituo cha Ruhila (Songea) utekelezaji umefikia asilimia 22; kuendelea na upanuzi wa kituo cha ukuzaji viumbe maji na ujenzi wa ghala moja (1) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 60; kuendelea na ujenzi wa kitotoleshi, ukarabati na upanuzi wa kituo cha ukuzaji viumbe maji cha Nyengedi – Lindi (asilimia 25); na kuendelea na ujenzi wa mashamba darasa sita (6) ya Ufugaji wa Samaki katika Halmashauri za wilaya za Kongwa, Iringa, Njombe, Songea, Tandahimba na Ruangwa ambapo utekelezaji umefikia asilimia 15; kutolewa kwa mafunzo kwa vitendo yanayojulikana kama ATAMIZI kwa vijana 200 wanaojishughulisha na uvuvi pamoja na ukuzaji viumbe maji, ili kuzalisha vijana watakaoshiriki katika usimamizi wa rasilimali za uvuvi na utoaji wa huduma za ugani; kukamilika kwa taratibu za ununuzi wa boti za uvuvi 158 ikiwa ni awamu ya kwanza ya ununuzi wa boti 160 zilizotarajiwa kununuliwa kwa ajili ya kukopesha wavuvi. Jumla ya shilingi bilioni 1.12 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(d) Mradi Na. 4703: Ufufuaji wa Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO) Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ukarabati wa Jengo la Utawala la RAS MKWAVI (Block B); na kuandaa na kuhuisha Bussiness Model na Mpango wa Biashara wa miradi itakayotekelezwa na Shirika. Jumla ya shilingi milioni 29.1 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
2.3.3.3. Uchimbaji wa Madini, Vito vya Thamani na Gesi Asilia
(i) Mradi Na. 1119: Usimamizi Endelevu wa Rasilimali za Madini (Sustainable Management of Mineral Resources Project - SMMRP)
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ujenzi wa vituo vitatu (3) vya umahiri vya Songea, Chunya na Mpanda; kununuliwa na kusimikwa (commissioning) kwa vifaa vya utafiti wa kisayansi (geoscience) na vifaa vya maabara na uchunguzi kwa ajili ya Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania – GST; kununuliwa kwa mitambo ya uchorongaji (mitambo 5 kwa ajili ya wachimbaji wadogo na mitambo 2 ya uzalishaji wa mkaa mbadala) na utengenezaji wa mkaa unaotokana na makaa ya mawe - STAMICO; na kuendelea na ujenzi wa jengo la kuhifadhia sampuli za miamba choronge eneo la Kizota - Dodoma ambapo utekelezaji wake umefikia asilimia 75. Shughuli nyingine iliyotekelezwa ni kununuliwa kwa mawe mawili (2) makubwa ya madini ya Tanzanite yenye jumla ya uzito wa kilo 5.22 kutoka kwa mchimbaji mdogo. Jumla ya shilingi bilioni 3.5 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(ii) Mradi Na. 1120: Kituo cha Jemolojia Tanzania (Tanzania Geomological Centre)
Hatua iliyofikiwa ni: Kuwawezesha watumishi tisa (9) wa Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) kupata mafunzo ya muda mfupi na mrefu ndani na nje ya nchi (Thailand, China na India) kuhusu masuala ya uongezaji wa thamani madini. Jumla ya shilingi milioni 716.34 zimetumika zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
2.3.3.4. Huduma
A. Maliasili na Utalii
Hatua iliyofikiwa ni: kuongezeka kwa idadi ya watalii kutoka watalii 922,692 mwaka 2021 hadi kufikia watalii 1,454,920 mwaka 2022 sawa na ongezeko la asimilia 57.7; kuongezeka kwa idadi ya watalii wa ndani kutoka watalii 788,933 mwaka 2021 hadi 2,363,260 mwaka 2022 sawa na ongezeko la asilimia 199.5; Tanzania Kuendelea Kutambulika Kimataifa; Kupandishwa Hadhi Maeneo ya Hifadhi na Misitu; Kuimarika kwa Ulinzi wa Rasilimali za Wanyamapori na Misitu; kuimarika kwa utalii wa urithi wa utamaduni na malikale; kuendeleza Programu za Upandaji Miti na Mashamba ya Miti; na kuongezeka kwa masoko na kiwango cha mazao ya nyuki yanayouzwa nje ya nchi.
(a) Mradi Na. 5203: Mradi wa Usimamizi wa Maliasili na Kuendeleza Utalii Kanda ya Kusini (Resilient Natural Resources Management for Tourism and Growth Project - REGROW)
Hatua iliyofikiwa ni: ukamilishaji na utiaji saini mikataba nane (8) ya ujenzi wa miundombinu mbalimbali ikiwemo ujenzi wa viwanja vya ndege sita (6) katika hifadhi za Taifa za Ruaha (3), Nyerere (2) na Mikumi (1) na ujenzi wa malango (3), vituo vya kutolea taarifa (2), umeme, kambi (4) za utalii, vituo vitatu (3) vya askari, kituo cha ikolojia (1), hosteli ya wanafunzi (1), malazi ya madereva wa utalii (1), mfumo wa maji safi, na canopy walkway katika hifadhi za Taifa za Nyerere, Ruaha, Udzungwa na Hifadhi ya Mazingira Asilia ya Kilombero. Vilevile, ununuzi wa matrekta saba (7) pamoja na viambata vyake 23 kwa lengo la kuimarisha miundombinu ya barabara katika maeneo ya hifadhi; kuwezesha vijana 120 kutoka wilaya za Kilolo, Iringa, Mvomero, Chamwino na Rufiji kupata mafunzo ya mbinu za kudhibiti wanyamapori wakali na waharibifu; kuwezesha vikundi 159 vyenye jumla ya wanachama 3,816 kwa kuwapatia fedha mbegu jumla ya Shilingi 1,453,272,934 katika vijiji 15 vya awamu ya kwanza vinavyopakana na hifadhi za Taifa Ruaha, Nyerere, Mikumi na Udzungwa; na kuwezesha ufadhili wa masomo ya fani mbalimbali kwa vijana 582 kutoka vijiji 15 katika Wilaya saba (7) za Kilombero, Kilosa, Morogoro, Iringa, Kilolo, Mvomero na Chamwino. Jumla ya shilingi bilioni 29.99 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(b) Mradi Na. 4812: Mradi wa Kupambana na Ujangili na Biashara Haramu ya Nyara
Hatua iliyofikiwa ni: kuandaa Mkakati wa Kitaifa wa Usimamizi wa Maeneo ya Jumuiya za Hifadhi za Wanyamapori 2023-2033; kuwezesha kufanyika kwa doria za ki-intelijensia na ushirikiano na nchi jirani katika kanda 10 zilizowezesha kukamatwa kwa vipande 52 vya meno ya tembo, nyamapori aina 101 mbalimbali na majangili 70 ambao wamechukuliwa hatua za kisheria; kuwezesha watumishi 319 kupata mafunzo katika masuala ya intelijensia, operesheni na uendeshaji mashtaka; kufanya tathmini kwa vikundi 155 vyenye wajumbe 2,726 vilivyopo katika mfumo ikolojia wa Ruaha-Rungwa ili kubaini vikundi vinavyokidhi vigezo vya kuwezeshwa na vikundi 45 vilikidhi vigezo na kupewa mafunzo ya ujasiriamali na kuwawezesha kuanzisha umoja wa wafugaji nyuki Manyoni na kuwezesha kuandaliwa kwa Mwongozo wa pamoja wa kubadilishana taarifa za kiintelijensia, uendeshaji wa operesheni za kupambana na ujangili na usimamizi wa wasiri na kuandaa mpango wa kujenga uwezo wa kitaasisi wa kupambana na ujangili na biashara haramu ya nyara. Jumla ya shilingi bilioni 12 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(c) Mradi Na. 4647: Panda Miti Kibiashara (Private Plantation and Value Chain in Tanzania)
Hatua iliyofikiwa ni: kuwezesha kutoa mafunzo kwa viongozi 296 wa Vikundi vya Upandaji miti ya namna ya kusimamia na kuendesha vikundi; kutoa mafunzo kwa wakulima wa miti 5,689; kutoa misumeno 335 ya kupogolea miti kwa Vikundi 80 vya Upandaji miti ; utambuzi wa wawekezaji 1,335; kuwezesha matukio 768 ya huduma za ugani ambapo wakulima 12,354 walishiriki; kuandaa Mipango ya Usimamizi wa Mashamba ya wakulima 603; kutoa vifaa vya kupambana na majanga ya moto (fire beaters 393 na knapsack fire sprayers 36); uanzishwaji wa Kamati za usimamizi wa moto za vijiji 80 zenye jumla ya watu 2,612; kuanzisha vikosi vya kupambana na moto vyenye jumla ya watu 1,284; kutoa pikipiki 14 katika kongani za Njombe (7), Mafinga (4) na Makete (3) kwa ajili ya kuwezesha utoaji wa huduma za ugani kwenye vijiji 80; na kuwezesha vikundi 39 kuandaa maandiko ya biashara kwa ajili ya kuomba mikopo yenye thamani ya Shilingi 726,335,500. Jumla ya shilingi milioni 959.5 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(d) Mradi Na. 4651: Mradi wa Kuwezesha Mnyororo wa Thamani wa Mazao ya Nyuki - BEVAC
Hatua iliyofikiwa ni: kukarabati ofisi ya mradi iliyopo Pemba; kununua magari matatu (3) na pikipiki 20 kwa ajili ya maafisa; kutoa mafunzo ya mbinu za ufugaji bora wa nyuki kwa vyama vya ushirika 19 vyenye jumla ya wafugaji nyuki 1,204; kukamilisha taratibu za maandalizi ya ujenzi wa bweni la wasichana lenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 350 katika Chuo cha Mafunzo ya Ufugaji Nyuki; kuwajengea uwezo viongozi wa vyama vya ushirika 19 vya ufugaji nyuki; kuwezesha ufanyikaji wa mikutano katika vijiji 297 kwa lengo la kuhamasisha jamii kutenga maeneo kwa ajili ya kufugia nyuki; kuwaunganisha wafanyabiashara sita (6) wanaouza asali nje ya nchi na wafugaji nyuki 296 na vikundi 29; kutoa mafunzo kwa makampuni 30 kuhusu utayari wa usafirishaji wa mazao ya nyuki nje ya nchi; kuwezesha kampuni 10 za uuzaji na usafirishaji wa asali nje ya nchi kupata cheti cha ubora kitakachowezesha kampuni hizo kuuza asali katika masoko mbalimbali duniani. Jumla ya shilingi bilioni 6.21zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
B. Utamaduni, Sanaa na Michezo
(i) Mradi Na. 6293: Programu ya Urithi wa Ukombozi wa Bara la Afrika
Hatua iliyofikiwa ni: Kukarabatiwa kwa jengo lililokuwa Makao Makuu ya Ofisi ya Kamati ya Ukombozi ya OAU ambapo utekelezaji umefikia asilimia 95; na kutoa elimu ya uzalendo wa kuenzi na kuhifadhi kumbukumbu za harakati za ukombozi wa Bara la Afrika kwa kuwafikia zaidi ya watu 2,000,000 Afrika kupitia mitandao ya kijamii, makongamano, matamasha, Makala jongefu na mijadala bayana. Jumla ya shilingi milioni 515 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(ii) Mradi Na. 4353: Ukarabati wa Chuo cha Sanaa Bagamoyo (TaSUBa) Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na hatua za ununuzi wa wakandarasi kwa ajili ya kuanzisha kituo cha redio na televisheni; kununuliwa kwa vifaa vya kufundishia na kujifunzia; kuendelea na ukarabati wa majengo; na kufanyika kwa Tamasha la 41 la Kimataifa la Utamaduni na Sanaa Bagamoyo. Jumla ya shilingi milioni 550 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(iii) Mradi Na. 6502: Mfuko wa Utamaduni na Sanaa Tanzania
Hatua iliyofikiwa ni: Kutolewa mikopo kwa awamu mbili (2) yenye thamani ya shilingi bilioni 1.07 kwa wasanii na wadau 45 waliokidhi vigezo. Jumla ya shilingi bilioni 1.07 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(iv) Mradi Na. 6385: Ujenzi wa Chuo cha Michezo cha Malya
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa hosteli ya wanafunzi ambapo utekelezaji umefikia asilimia 27; na kukamilika kwa michoro na kutangazwa kwa zabuni ya ujenzi wa Kituo cha Kukuza na Kuendeleza Vipaji (Sports Academy). Jumla ya shilingi bilioni 1.3 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(v) Mradi Na. 6523: Ujenzi wa Eneo Changamani la Michezo Dar es Salaam
Hatua iliyofikiwa ni: Kupatikana kwa Mshauri Elekezi wa ukarabati wa viwanja vya Benjamini na Uhuru na kuandaliwa kwa makadirio ya majenzi (BOQ) na michoro; na kukamilika kwa ukarabati mdogo wa miundombinu ya eneo changamani la michezo. Jumla ya shilingi milioni 687 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(vi) Mradi Na. 6521 - Kuimarisha Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) na Kukiuza Kiswahili Kikanda na Kimataifa
Hatua iliyofikiwa ni: Kushiriki na kutoa mada ya ubidhaishaji wa Kiswahili katika Kongamano la Jumuiya ya Afrika Mashariki (JAMAFEST) lililofanyika nchini Burundi na Kongamano la Chama cha ukuzaji wa Kiswahili Duniani (CHAUKIDU) lililofanyika Chuo Kikuu cha HOWARD nchini Marekani; kufanyika kwa maadhimisho ya kwanza ya Siku ya Kiswahili Duniani; kuanzishwa kwa vituo 30 vya kufundisha Kiswahili katika Balozi za Tanzania Abu Dhabi, Uholanzi, Zimbabwe, Cuba, Ufaransa na Saudi Arabia na ndani ya nchi; na kuendesha darasa la kwanza la Kiswahili nchini Malawi katika Chuo Kikuu cha Hebron. Jumla ya shilingi milioni 300 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(vii) Mradi Na. 6527 - Ujenzi na Uimarishaji wa Miundombinu ya Michezo katika Shule Maalumu za Michezo
Hatua iliyofikiwa ni: Kufanyika kwa tathmini ya shule 56 za sekondari zilizoteuliwa kuwa shule maalum za michezo; kuanza kwa maboresho ya miundombinu ya michezo katika shule 56 za Sekondari katika mikoa ya Tabora, Tanga, Arusha, Pwani, Dodoma na Mtwara; na kuendelea na maandalizi ya makadirio ya majenzi (BOQ) ili kutangaza zabuni na kumpata Mkandarasi.
(viii) Mradi Na. 6504 - Ujenzi wa Vituo vya Mazoezi na Kupumzikia Wananchi Pamoja na Mradi wa Ujenzi wa Sports Arena (Dar es Salaam na Dodoma)
Hatua iliyofikiwa ni: Kupatikana kwa mkandarasi wa ujenzi wa vituo vya mazoezi na kupumzikia wananchi katika mikoa ya Dar es Salaam na Dodoma ambapo mkandarasi yupo katika hatua za awali za kuandaa vifaa (Mobilization Stage); na kupatikana kwa eneo la ekari 12 kwa ajili ya ujenzi wa Arena ya Michezo Dar es Salaam lililopo Kawe, Tanganyika Packers. Jumla ya shilingi bilioni 5.8 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
C. Sekta ya Fedha, Biashara na Masoko
(i) Benki ya Maendeleo TIB
Hadi kufikia Aprili 2023, Benki ya Maendeleo TIB ilikuwa imetoa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 370.60 ambayo ipo kwenye sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii zikiwemo kilimo miradi sita (shilingi bilioni 90.85), ujenzi miradi minne (shilingi bilioni 28), elimu miradi miwili (shilingi bilioni 5.19), umeme miradi miwili (shilingi bilioni 6.64), Taasisi za fedha mradi mmoja (shilingi bilioni 0.32), uzalishaji miradi minne (shilingi bilioni 41.38), Madini miradi miwili (shilingi bilioni 97.3), Utalii miradi minne (shilingi bilioni 77.78), Mawasiliano na Usafirishaji mradi mmoja (shilingi bilioni 1.86), Mikopo binafsi mia moja na thelathini na nane (shilingi bilioni 7.02), maji mijini miradi 6 (shilingi bilioni 14.25) na programu ya maji vijijini (shilingi bilioni 4.18). Kati ya miradi hiyo, asilimia 91.32 ni miradi ya sekta binafsi na asilimia 8.68 ni miradi ya sekta ya Umma.
(ii) Benki ya Maendeleo ya Kilimo – TADB
Hadi kufikia Disemba 2022 TADB ilikuwa na mtaji (total assets) wa shilingi bilioni 454.351 ikiwa ni ongezeko la asilimia 26 kutoka shilingi bilioni 360.502 zilizokuwepo katika kipindi kama hicho mwaka 2021 kwa hesabu zilizokaguliwa. Hata hivyo, katika kipindi kilichoishia Machi, 2023 mtaji ulipungua kutoka shilingi bilioni 454.351 uliokuwepo Disemba, 2022 hadi kufikia shilingi bilioni 441.039 Machi, 2023. Aidha, katika robo ya kwanza iliyoishia Machi, 2023 TADB ilitoa mikopo ya jumla ya shilingi bilioni 182.87 kwenye mnyororo wa thamani wa mazao ya viwandani (Kahawa, Pamba na Mkonge); mazao ya mbogamboga na matunda (Parachichi, Vanilla, na Zabibu); uzalishaji wa mbegu za mafuta ya chakula (Alizeti na Chikichi); uzalishaji wa nafaka mbalimbali (Mahindi, Mpunga na Maharage) pamoja na ufugaji wa ng’ombe wa maziwa, ng’ombe wa nyama, kuku na samaki. Vilevile, kufikia Machi, 2023 TADB kupitia mfuko wa dhamana kwa wakulima wadogo (SCGS), ulitoa dhamana za jumla ya shilingi bilioni 56.548 kupitia benki kumi na tano (15) washirika katika mnyororo wa thamani wa mazao mbalimbali katika mikoa 24 ya Tanzania bara na kufanya kiasi cha dhamana kilichotolewa kwa wakulima wadogo kufikia shilingi bilioni 181.567 tangu mfuko ulipoanza mwaka 2018.
(a) Huduma za Bima
Hatua iliyofikiwa ni: Kuandikishwa na kutolewa kwa leseni 1,196 zikijumuisha Kampuni za bima 32, Kampuni za bima mtawanyo (Reinsurance) 3, madalali wa bima mtawanyo sita (6), madalali wa bima 103, wakala wa bima 1200 na benki wakala (bancansurance) 28, watoa huduma ya bima kidigitali tisa (9) , watakwimu bima wanne (4), Wachunguzi binafsi wa bima (Private Insurance investigators) watatu (3) na wakadiriaji hasara wa bima 56; Kufanya ukaguzi kwa watoa huduma za bima ambao ni makampuni ya bima 18, matawi ya kampuni 18 za bima, madalali wa bima 8; benki wakala 8 na mawakala wa bima 68; kufanya ukaguzi wa bima kwa vyombo vya moto 33,160,000; na kupokea malalamiko 284 ambayo yalishughulikiwa ambapo malalamiko 68 yalipatiwa ufumbuzi na kulipwa, 22 yalikataliwa, 11 yalipelekwa mahakamani, 18 yalipelekwa kwa Msuluhishi wa Migogoro ya Bima na 135 bado yanaendelea katika hatua mbalimbali za uchunguzi. (b) Huduma Ndogo za Fedha
Hadi kufikia Machi, 2023, Benki Kuu ya Tanzania ilitoa jumla ya leseni 1,187 kwa Watoa huduma Daraja la Pili, na leseni 780 kwa Vyama vya Ushirika wa Akiba na Mikopo, kusajili Vikundi 37,937 vya Kijamii vya Huduma Ndogo za Fedha. Aidha, Wizara ya Fedha na Mipango imetoa mafunzo kwa waratibu wa biashara ya huduma ndogo za fedha 115 kutoka katika mikoa 13 mwezi Mei, 2023. Vilevile, hadi kufikia Machi, 2023 Watoa huduma ndogo za fedha Daraja la Pili wamekopesha mikopo yenye thamani ya shilingi billioni 870 kwa wajasiriamali wadogo na wa kati nchini.
(c) Huduma Jumuishi za Fedha
Hatua iliyofikiwa ni: kuanzishwa kwa idara ya huduma jumuishi za fedha ndani ya Benki Kuu ili kuchochea mikakati itakayoongeza ujumuishaji wa kifedha nchini na kutoa elimu ya fedha kwa umma kwa kushirikiana na wadau wa sekta binafsi na Serikali ikiwemo kujumisha elimu ya fedha katika sera na mitaala ya elimu ya awali, sekondari, vyuo vya kati na vyuo vikuu nchini. Aidha, katika kuimarisha ulinzi kwa mlaji wa huduma za fedha, Benki Kuu imeandaa rasimu ya Mpango wa Kumlinda Mlaji wa Huduma za Fedha (Bank of Tanzania Financial Consumer Protection Framework). Vilevile, utaratibu wa kuweka mazingira ya kufanya majaribio ya teknolojia za fedha (regulatory sandbox) ili kutambua na kuchochea ubunifu wa aina mbalimbali katika masuala ya fedha unaandaliwa.
(d) Mradi Na. 6251: Programu ya Maboresho ya Usimamizi wa Fedha za Umma (PFMRP)
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa uandaaji wa Mwongozo wa Ufuatiliaji na Tathmini (Monitoring and Evaluation Guideline) kwa Ofisi ya Msajili wa Hazina pamoja na taasisi anazozisimamia; kufunga na kuunganishwa kwa mfumo wa MUSE na mifumo sita (6) ambayo ni GePG, PlanRep–TR, PlanRep – LGA, ERMS na mifumo ya benki za biashara (CRDB na NMB); kuunganishwa na kufungamanishwa kwa Mfumo wa Ufuatiliaji na Uchambuzi wa Taarifa za Fedha na mifumo ya PlanRep - TR na MUSE; kuendelea na uundaji wa mfumo wa ukusanyaji wa gawio na fedha taslim kutoka Taasisi na Mashirika ya Umma; kuendelea na ujenzi wa Mfumo wa Usimamizi wa Ununuzi wa Umma kwa njia ya mtandao (NeST); Kuandaa Mpango Mkakati wa Utekelezaji wa Programu ya Maboresho ya usimamizi wa Fedha za Umma Awamu ya Sita (PFMRP VI); Kuhuisha Mfumo wa Ukusanyaji wa Mapato katika Serikali za Mitaa (TAUSI) na kuhuishwa kwa Mfumo wa Kihasibu wa Kuripoti Mapato na Matumizi katika Vituo vya Kutolea Huduma (FFARS); Kuandaa Mfumo wa Kusimamia Viashiria Hatarishi (GERMIS); Kuandaa mahitaji ya Mfumo wa Huduma Ndogo za Kifedha; kukamilika kwa ukarabati wa Ofisi za Hazina Ndogo katika mikoa Kigoma, Kagera na Ruvuma. Jumla ya shilingi bilioni 14.8 zimetumika katika kipindi Julai, 2022 na Aprili, 2023.
(e) Mradi Na. 6244: Miradi ya Kimkakati ya Kuongeza Mapato katika Halmashauri
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na miradi 26 katika Halmashauri 23 ambapo miradi 19 imefikia hatua ya ukamilishaji (miradi 12 imeanza kutoa huduma) na miradi saba (7) ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Jumla ya shilingi bilioni 16.94 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili 2023.
D. Masoko
(a) Soko la Bidhaa Tanzania – TMX
Hatua iliyofikiwa ni: kutoa elimu, kuhamasisha wadau mbalimbali juu ya manufaa ya Soko la Bidhaa na kuuza Mazao. Soko liliuza Kahawa (Kagera) ambapo jumla ya tani 49,677 ziliuzwa kwa thamani ya shilingi bilioni 110.69. Ufuta uliuzwa tani 136.650 kwa shilingi bilioni 0.44, Kakao tani 909.580 kwa shilingi bilioni 4.31. Maandalizi ya kuuza Mifugo hai (ngómbe, mbuzi na kondoo) na ngozi zinazotokana na Wanyama hao yanaendelea. Aidha, timu ya wataalam ikijumuisha Soko la Bidhaa, Wizara ya Fedha na Mipango, Tume ya madini na Benki Kuu ya Tanzania ilikutana na kujadili namna Soko la Bidhaa litakavyoshiriki kuuza madini. Tume ya Madini kwa kushirikiana na Soko la Bidhaa Tanzania itafanya utafiti wa aina ya madini yanayoweza kuuzwa kupitia Soko la Bidhaa na kuandaa mkataba wa makubaliano (MOU) kwa maeneo yote ya ushirikiano. Aidha, Soko la Bidhaa kwa kushirikiana na Bodi ya Pamba, Bodi ya Usimamizi Stakabadhi za Ghala na Tume ya Maendeleo ya Ushirika limeanza maandalizi ya kufanya mauzo ya Pamba katika msimu wa mwaka 2023/24. Hatua za awali ni pamoja na kutoa elimu kwa wadau wa pamba na kuwapitisha katika mfumo wa kielektroniki wa Soko la Bidhaa.
2.3.4. Kukuza Biashara na Uwekezaji
2.3.4.1. Huduma za Biashara na Masoko
(a) Uendelezaji wa Masoko ya Bidhaa
Hatua iliyofikiwa ni: Kujengea uwezo wadau wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala na Soko la Bidhaa katika mikoa 12; na kuendelea na taratibu wa kuwa na jengo la Ofisi. Tayari mshauri elekezi amepatikana ambaye ni DIT (Dar es salaam Insitute of Technology) na hatua za awali zinaendelea katika utekelezaji wa kuwa na jengo la ofisi eneo lililotengwa.
(b) Kuimarisha Maendeleo ya Soko la Ndani na Nje - TANTRADE
Hatua iliyofikiwa ni: Kuratibiwa kwa Maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF) yaliyohusisha washiriki 3,200 (kampuni za ndani 2,975 na kampuni za nje 225 kutoka Nchi 23); kuandaa na kuzinduliwa kwa Mfumo wa TanTrade
Biashara Mobile App unaowezesha wafanyabiashara kupata taarifa za masoko na kubaini fursa za kuweza kuuza bidhaa zao; kuandaliwa kwa Mwongozo wa fursa za Uwekezaji baina ya Tanzania na Marekani; na Kuuzwa kwa tani 147,061 za mazao mbalimbali ikiwemo zabibu, muhogo, mchele, asali, nyama za thamani ya shilingi bilioni 208.2 kwa wanunuzi ndani na nje ya nchi. Jumla ya shilingi milioni 400.00 zimetumika katika kipindi Julai, 2022 na Aprili, 2023.
(c) Kuendeleza Biashara Kupitia Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE)
Hatua iliyofikiwa ni: Kupatikana kwa mkandarasi wa mradi wa ujenzi wa jengo la ghorofa 10 la Vipimo na Viwango katika kampasi kuu ya Dar es salaam; na kukamilika kwa ukarabati wa Kampasi ya Dodoma. Jumla ya shilingi milioni 458.16 zimetumika katika kipindi Julai, 2022 na Aprili, 2023.
Kukuza Ushiriki wa Watanzania kwenye Miradi ya Kimkakati na Uwekezaji Hatua iliyofikiwa ni: Kufanyika kwa tathmini ya ushiriki katika miradi ya kimkakati, ambayo ilibainika kuwa kampuni 2,827 za watanzania ziliingia mikataba kwa ajili ya kutoa huduma za ukandarasi ambapo kati ya hizo kampuni 848 ni za ukandarasi, kampuni 83 za ushauri elekezi na kampuni 1,896 za kutoa huduma ya chakula, ulinzi, usafiri, bima na bidhaa za ujenzi. Aidha, miradi hiyo ilizalisha fursa za ajira 72,395.
Kukuza Sekta Binafsi
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na majadiliano kati ya sekta ya umma na binafsi kupitia mabaraza ya biashara ya ngazi ya Wilaya, Mkoa na Taifa kwa lengo la kutatua chnagamoto zinazokwamisha biashar ana uwekezaji ambapo jumla ya mikutano 10 imefanyika katika ngazi ya mikoa; na kufanyika kwa utambuzi wa muundo wa Sekta Binafsi nchini ambapo jumla ya Kampuni 488 zenye ukomo wa ahadi (Limited by Guarantee) za Sekta Binafsi zimesajiliwa na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) na Jumuiya za Biashara 22 zimesajiliwa na Ofisi ya Msajili wa Jumuiya nchini.
2.3.4.2. Kuboresha Mazingira ya Kufanya Biashara na Uwekezaji
A. Kuboresha Mazingira ya Uwekezaji
Hatua iliyofikiwa ni: Kutungwa kwa Sheria ya Uwekezaji namba 10 ya mwaka 2022; kuendelea kuandaa kanuni za utelekezaji wa Sheria ya Uwekezaji ya mwaka 2022; na kuandaliwa kwa mapendekezo ya maboresho ya sheria na kanuni zenye muingiliano ikiwemo tozo kero, adhabu, leseni na vibali kwenye sekta mbalimbali za biashara na uwekezaji; kuandaa na kushiriki makongamano 10 ndani na nje ya nchi kwa ajili ya kutangaza kwa fursa mbalimbali za uwekezaji kwa ajili ya kuvutia uwekezaji wa mitaji kutoka nje (FDI); kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa Hati za Makubaliano 50 zilizosainiwa; na kuendelea kuratibu maandalizi ya Kongani za Viwanda.
B. Kuimarisha Ushiriki wa Sekta Binafsi
(a) Huduma za Uwekezaji Mahala Pamoja (One Stop Facilitation Centre - OSC)
Hatua iliyofikiwa ni: Kutolewa kwa huduma kwa wateja 13,836 katika kituo cha Huduma za Uwekezaji Mahala Pamoja (OSC) katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023; Kusajiliwa kwa miradi mipya 240 (wazawa - 89, wageni - 94 na ubia - 57) inayotarajiwa kutengeneza ajira 39,245; kutolewa kwa elimu kwa umma kuhusu huduma zitolewazo na OSC kwa njia ya makala (Documentary) na vyombo vya habari; na kutengenezwa kwa Mfumo wa Kielektroniki wa Kuhudumia Wawekezaji Mahali Pamoja (Tanzania Electronic Investment Window - TeIW) ambapo awamu ya kwanza inahusisha kuunganisha Mifumo kutoka Taasisi za NIDA, TRA, BRELA, TIC, Kazi, Uhamiaji na Ardhi.
C. Mahusiano na Nchi za Nje na Uchumi wa Kidiplomasia
(a) Mradi Na. 6391: Ujenzi na Ukarabati wa Majengo ya Vitega Uchumi, Ofisi na Makazi ya Watumishi Balozini
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ukarabati wa makazi ya balozi wa Tanzania
Brussels (Ubelgiji) na nyumba ya mkuu wa utawala Ubalozi wa Tanzania Stockholm (Sweden); kukamilika kwa ukarabati wa jengo linalotumika kama kitega uchumi na jengo la makazi ya watumishi katika Ubalozi wa Tanzania Harare (Zimbabwe); kukamilika kwa ukarabati wa majengo matatu (3) ya makazi ya watumishi katika Ubalozi wa Tanzania Lilongwe (Malawi); kuendelea na ukarabati wa jengo la ofisi za ubalozi wa Tanzania Brussels (Ubelgiji); kuendelea na ukarabati wa makazi ya balozi wa Tanzania Stockholm (Sweden); na kuendelea na ukarabati wa jengo la zamani la ofisi za Ubalozi wa Tanzania Washington D.C (Marekani). Shughuli nyingine zilizotekelezwa ni pamoja na ununuzi wa jengo la Mkuu wa Utawala na Fedha katika Ubalozi wa Tanzania, Berlin (Ujerumani). Jumla ya shilingi bilioni 6.08 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(b) Mradi Na. 6389: Ujenzi wa Majengo ya Ofisi
Upanuzi wa Uboreshaji wa Miundombinu ya Chuo cha Diplomasia
Hatua iliyofikiwa ni kuendelea na ujenzi wa vyumba tisa (9) vya mihadhara katika Chuo cha Diplomasia, Kurasini, Dar es Salaam. Jumla ya shilingi milioni 663.0 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
2.3.5. Kuchochea Maendeleo ya Watu
2.3.5.1. Afya
(a) Mradi Na. 5487: Hospitali ya Taifa ya Muhimbili
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa Jengo la Wodi Maalum (Private wards) ambao umefikia asilimia 75; kukamilika kwa utengenezaji wa mfumo mpya wa utoaji huduma kupitia TEHAMA (Health Management Infomation System); kukamilika kwa ukarabati wa vyumba vitano (5) vya ICU na vyumba vya radiolojia (MRI 1, CT SCAN 1 na X-Ray 2); na kukamilika kwa upanuzi wa jengo la OPD na ukarabati wa Hospitali ya watoto. Jumla ya shilingi bilioni 1.9 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(b) Mradi Na. 6364: Hospitali ya Taifa Muhimbili - Mloganzila
Hatua iliyofikiwa ni: Kuwezesha mafunzo ndani na nje ya nchi kwa watumishi 82 katika fani mbalimbali za kibingwa katika masomo ya uzamili; kukamilika kwa ujenzi wa kituo cha upandikizaji viungo na sehemu ya kufulia nguo; na kukamilika kwa ukarabati wa wodi za watoto wachanga mahututi (NICU).
Shughuli nyingine zilizotekelezwa ni: Kukamilika kwa ujenzi wa wodi ya kawaida ya watoto, wodi ya mama wajawazito mahututi, wodi ya uangalizi maalumu wa mama wajawazito (HDU) na chumba maalumu kwa ajili ya kufanya matengenezo ya vifaa tiba (biomedical workshop); na kutolewa kwa huduma za uchunguzi za kibingwa ambapo jumla ya vipimo vya maabara 11,096 (Plain X-Ray 3,070, CT Scan 2,601, USS 4,055, MRI 720, Floroscopy 507 na mammography 223) vilifanyika. Aidha, hospitali imetoa huduma mpya za kupunguza uzito kwa kuwekewa Puto (Intragastric balloon) ambapo jumla ya wagonjwa 87 na upandikizaji wa uloto (bone marrow transplant) kwa wagonjwa 11 wamehudumiwa. Jumla ya shilingi bilioni 1.5 zimetumika hadi Aprili 2023.
(c) Mradi Na. 5491: Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI)
Hatua iliyofikiwa ni: kuendelea ununuzi wa vifaa tiba na utoaji wa huduma za Tiba kwa njia ya mkoba (Outreach Program) ambapo jumla ya wateja 4,528 walipatiwa huduma hiyo katika Hospitali za Mikoa ya Mtwara, Lindi na Dar es Salaam. Jumla ya shilingi milioni 500 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(d) Mradi Na. 5419: Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI)
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ukarabati na upanuzi wa jengo la Wagonjwa mahututi (ICU). Jumla ya shilingi bilioni 2 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(e) Mradi Na. 5412: Taasisi ya Saratani Ocean Road
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ukarabati na upanuzi wa jengo la wagonjwa mahututi; kukamilika kwa ukarabati mkubwa wa chumba cha MRI; kukamilika kwa ukarabati wa chumba cha tiba mtandao; kufungwa kwa mashine ya PET/CT SCAN; na kununuliwa na kusimikwa kwa mashine mbili (2) za LINAC na mbili (2) za COBALT. Jumla ya shilingi bilioni 4 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(f) Mradi Na. 5424: Hospitali ya Rufaa ya Magonjwa Ambukizi – Kibong’oto (Kilimanjaro)
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD) na jengo la utawala; kuendelea na ujenzi wa maabara ya Kisasa (BSL 3) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 96; na kuendelea na ujenzi na ukarabati Mkubwa wa jengo la Radiolojia kwa ajili ya kusimika CT Scan ambapo utekelezaji umefikia asilimia 21. Jumla ya shilingi bilioni 1.3 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(g) Mradi Na 5425: Hospitali ya Rufaa ya Afya ya Akili Mirembe
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ujenzi wa nyumba ya Mtumishi - Hombolo; kuendelea na ujenzi wa jengo la wagonjwa mahututi (ICU) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 99 na jengo la huduma za dharura (EMD) asilimia 98; na kutoa mafunzo ya muda mrefu na mfupi kwa watumishi 14 katika fani mbalimbali za kibingwa katika vyuo vya ndani na nje. Jumla ya shilingi bilioni 4 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(h) Mradi Na. 5426: Hospitali ya Rufaa Kanda ya Ziwa, Bugando
Hatua iliyofikiwa ni kukamilika kwa ukarabati na upanuzi wa majengo ya wagonjwa mahututi - Medical ICU, Surgical ICU, na Neonatal ICU. Jumla ya shilingi milioni 997 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(i) Mradi Na. 5427: Hospitali ya Kanda ya Kaskazini (KCMC)
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ukarabati na upanuzi wa jengo la wagonjwa mahututi (Medical ICU na Surgical ICU); na kuendelea na ujenzi wa jengo la huduma za tiba - mionzi kwa matibabu ya magonjwa ya kansa (Radiotherapy) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 53. Jumla ya shilingi bilioni 1.0 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(j) Mradi Na. 5422: Hospitali ya Rufaa ya Nyanda za Juu Kusini Mbeya Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ukarabati na upanuzi wa jengo la wagonjwa mahututi (ICU), jengo la huduma za dharura (EMD) na chumba cha tiba mtandao; kununuliwa kwa vifaa tiba ikiwemo patient monitors 18, Vitanda, na Bed Lockers; na kuendelea na ujenzi wa jengo kwa ajili ya huduma za uzazi unaofanyika eneo la Meta ambapo utekelezaji umefikia asilimia 99. Jumla ya shilingi bilioni 1.1 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(k) Mradi Na. 5428: Hospitali ya Benjamini Mkapa
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ukarabati wa chumba cha kutolea tiba mtandao na jengo la huduma za CT - Scan; kuanza kutolewa kwa huduma ya upandikizaji wa Uloto (Bone marrow Transplant) ambapo wagonjwa watatu (3) wamehudumiwa; kukamilika kwa upanuzi wa jengo la wagonjwa mahututi (ICU); na na kuendelea na ujenzi wa jengo la Tiba Mionzi (Radiotherapy) ambao umefikia asilimia 15.5. Jumla ya shilingi bilioni 3.1 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(l) Mradi Na. 5408: Ujenzi wa Hospitali ya Kanda ya Ziwa - Burigi
Hatua iliyofikiwa ni: kukamilika kwa awamu ya tatu ya ujenzi wa nyumba 20 za watumishi; kuendelea na ujenzi wa uzio ambao umefikia asilimia 85; kukamilika kwa ujenzi wa njia za kupita wagonjwa na barabara za ndani ya eneo la Hospitali; na kukamilika kwa ujenzi wa jengo la huduma za uchunguzi kwa njia ya mionzi (Radiolojia). Shughuli nyingine zilizotekelezwa ni kukamilika kwa ujenzi wa jengo la nyumba ya mashine ya kufua umeme (power house) na kukamilika kwa ujenzi wa jengo la ghorofa mbili (2) la wodi ya wagonjwa. Jumla ya shilingi milioni 461 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(m) Mradi Na. 5423 Hospital ya Rufaa ya Kanda ya Kusini - Mtwara
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ujenzi wa jengo la wagonjwa mahututi (ICU), ujenzi wa nyumba ya mtumishi na ukarabati wa chumba cha tiba mtandao; na kuendelea na ujenzi wa Jengo la Huduma za Dharura (EMD) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 80 na ujenzi wa jengo la OPD umefikia asilimia 61. Jumla ya shilingi bilioni 3.9 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(n) Mradi Na. 5411: Mradi wa Kuboresha Hospitali za Rufaa za Mikoa
Hatua iliyofikiwa ni:
(i) Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Njombe: Kukamilika kwa nyumba ya mtumishi na ukarabati wa jengo la huduma za CT-Scan. Jumla ya shilingi bilioni 2.2 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(ii) Hospitali ya Mkoa Simiyu: Kuendelea na ujenzi wa jengo la huduma za afya ya uzazi ambapo utekelezaji umefikia asilimia 88; kuendelea na ujenzi wa jengo la wagonjwa mahututi (asilimia 94), jengo la huduma za dharura (asilimia 94) na nyumba ya mtumishi (asilimia 98). Jumla ya shilingi milioni 337 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(iii) Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita: Kuendelea na ujenzi wa Jengo la Afya ya Uzazi ambao umefikia asilimia 29, jengo la wagonjwa wa nje (OPD) asilimia 99.5, jengo la wagonjwa mahututi (asilimia 98) na jengo la huduma za dharura (asilimia 98); na kukamilika kwa nyumba ya mtumishi. Jumla ya shilingi bilioni 1.8 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(iv) Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Songwe: Kukamilika kwa ujenzi wa jengo la OPD; na kuendelea na ujenzi wa jengo la wagonjwa mahututi ambapo utekelezaji umefikia asilimia 90, jengo la huduma za dharura (asilimia 89) na na jengo la huduma za afya ya uzazi umefikia asilimia 55. Jumla ya shilingi
bilioni 2.6 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(v) Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Katavi: Kukamilika kwa ujenzi wa nyumba ya mtumishi; kuendelea na ujenzi wa majengo ya uchunguzi na afya ya uzazi, miundombinu ya ICT, HVAC, Lift, Hewa Tiba, chumba cha tiba mtandao na jengo la OPD na Ujenzi jengo la huduma za CT-Scan ambao umefikia asilimia 97; na ujenzi wa jengo la huduma za dharura na jengo la wagonjwa mahututi umefikia asilimia 84. Jumla ya shilingi bilioni 12.9 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(vi) Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Singida (RRH): Kukamilika kwa ujenzi wa nyumba ya mtumishi, ukarabati wa jengo la huduma za CT - Scan na chumba cha tiba mtandao; na kuendelea na ujenzi wa jengo la huduma za dharura na Jengo la wagonjwa mahututi ambapo utekelezaji umefikia asilimia 90. Jumla ya shilingi bilioni 7.4 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(vii) Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Shinyanga: Kukamilika kwa ujenzi ya nyumba ya mtumishi na jengo la huduma za CT-Scan; na kuendelea na ujenzi wa jengo la wagonjwa mahututi ambapo utekelezaji umefikia asilimia 97 na jengo la huduma za dharura asilimia 99. Jumla ya shilingi bilioni 3.4 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(viii) Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mara: Kukamilika kwa ujenzi wa nyumba mbili (2) za watumishi; kuendelea na ujenzi wa jengo la wagonjwa mahututi ambapo utekelezaji umefikia asilimia 90 na jengo la huduma za dharura asilimia 40. Jumla ya shilingi bilioni 1.0 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(ix) Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Arusha (Mount Meru): Kukamilika kwa ujenzi wa nyumba ya mtumishi, ukarabati na upanuzi wa jengo la wagonjwa mahututi, chumba cha tiba mtandao na jengo la huduma za CT - Scan. Jumla ya shilingi bilioni 3.2 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(x) Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwanza (Sekou Toure): Kukamilika kwa ukarabati wa jengo la huduma za CT-Scan, chumba cha tiba mtandao na nyumba ya mtumishi. Jumla ya shilingi milioni 537 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(xi) Hospitali ya Rufaa ya Mkoa (Mwananyamala): Kuendelea na ujenzi wa jengo la Huduma za dharura ambapo utekelezaji umefikia asilimia 98 na jengo la wagonjwa mahututi (asilimia 90) na ukarabati wa jengo la huduma za CT-
Scan (asilimia 99). Jumla ya shilingi bilioni 3.2 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(xii) Hospitali ya Rufaa ya Mkoa (Temeke): Kukamilika kwa ukarabati na upanuzi wa jengo la huduma za dharura; kuendelea na ujenzi wa jengo la huduma za CT - Scan ambapo utekelezaji umefikia asilimia 95; ukarabati na upanuzi wa jengo la wagonjwa mahututi umefikia asilimia 96. Jumla ya shilingi bilioni 2.9 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(xiii) Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Pwani (Tumbi): Kukamilika kwa ujenzi wa nyumba ya mtumishi; kukamilika kwa ukarabati na upanuzi wa jengo la wagonjwa mahututi, jengo la huduma za dharura na jengo la huduma za CT - Scan. Jumla ya shilingi bilioni 2.9 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(xiv) Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Kigoma (Maweni): Kukamilika kwa ujenzi wa jengo la kuhifadhi maiti, nyumba ya mtumishi na ukarabati wa chumba cha tiba mtandao; na kuendelea na ujenzi wa jengo la wagonjwa mahututi, jengo la huduma za CT-Scan na huduma za dharura ambapo utekelezaji umefikia asilimia 99 na jengo la OPD asilimia 95. Jumla ya shilingi milioni 400 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(xv) Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Kilimanjaro (Mawenzi): Kukamilika kwa ukarabati na upanuzi wa jengo la wagonjwa mahututi, jengo la huduma za dharura na ujenzi wa nyumba ya mtumishi; na kuendelea na ujenzi wa jengo la huduma za afya ya uzazi ambapo utekelezaji umefikia asilimia 85. Jumla ya shilingi bilioni 2.9 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(xvi) Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Manyara: Kukamilika kwa ukarabati wa chumba cha tiba mtandao na nyumba ya mtumishi na ujenzi wa jengo la wagonjwa wa Nje (OPD) umefikia asilimia 99 na kuendelea na ujenzi wa majengo ya huduma za CT - Scan (asilimia 92), Jengo la Damu Salama (asilimia 72), wagonjwa mahututi (asilimia 82) na huduma za dharura (asilimia 70). Jumla ya shilingi bilioni 3.5 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(xvii) Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mbeya: Kukamilika kwa ukarabati na upanuzi wa jengo la wagonjwa mahututi na ujenzi wa nyumba ya mtumishi; na kuendelea na ujenzi wa jengo la huduma za CT-Sca ambapo utekelezaji umefikia asilimia 87 na jengo la upasuaji (theatre, ICU & CSSD) umefikia asilimia 98. Jumla ya shilingi bilioni 2.0 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(xviii)Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mtwara: Kukamilika kwa ukarabati wa jengo la huduma za CT - Scan. Jumla ya shilingi bilioni 2.2 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(xix) Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Dodoma: Kukamilika kwa ukarabati na upanuzi wa jengo la huduma za dharura, ujenzi wa nyumba ya mtumishi, ujenzi wa jengo la huduma za CT - Scan na ujenzi wa jengo la wagonjwa mahututi. Jumla ya shilingi bilioni 2.9 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(xx) Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Tanga: Kukamilika kwa ujenzi wa jengo la huduma za CT-Scan, ukarabati na upanuzi wa jengo la wagonjwa mahututi na ukarabati wa chumba cha tiba mtandao. Aidha, ukarabati na upanuzi wa jengo la huduma za dharura umefikia asilimia 99.4 na ujenzi wa nyumba ya mtumishi umefikia asilimia 99. Jumla ya shilingi bilioni 2.6 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(xxi) Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Kagera: Kukamilika kwa ujenzi wa nyumba ya Mtumishi na jengo la wagonjwa mahututi; na kuendelea na ujenzi wa jengo la huduma za dharura (asilimia 99) na jengo la huduma za CT-Scan (asilimia 98). Jumla ya shilingi bilioni 3.4 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(o) Mradi Na 2208: Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu ya Taifa (NIMR)
Hatua iliyofikiwa ni: Kufanyika kwa tafiti za afya za magonjwa 113 ya binadamu; kufanyika kwa utafiti wa kufuatilia hali ya maambukizi ya malaria nchini kwa kutumia mbinu za vinasaba katika mikoa 13 ya Tanzania Bara; kufanyika kwa utafiti kuhusu kutathmini usugu wa vimelea vya ugonjwa wa malaria dhidi ya dawa ya mseto barani Afrika; uimarishaji uwezo wa mfumo wa afya na kupeleka afua ya Praziquantel ya watoto (Pediatric Praziquantel) kwa ajili ya kudhibiti ugonjwa wa kichocho kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano, utafiti wa usalama na ufanisi wa chanjo ya TANCoV 1.3.20 SARS-CoV-2; kufanyika kwa utafiti unaojumuisha uchunguzi wa Kifua Kikuu ili kukomesha Kifua Kikuu katika ukanda wa Afrika Mashariki kwa nia ya kutafsiri shahidi za kitafiti kuwa sera na utendaji (EXITTB); kufanyika kwa utafiti wa kuzuia ugonjwa wa kisukari Afrika; kufanyika kwa jaribio nasibu la awamu ya tatu ya dawa ya Metformin kwa watu walioambukizwa VVU wanaokaribia kupata ugonjwa wa kisukari; na kufanyika kwa utafiti wa vyakula tiba kwa ajili ya afya ya uzazi na kutatua mahitaji muhimu ya virutubisho na madini kabla na wakati wa ujauzito. Jumla ya shilingi bilioni 1.0 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(p) Mradi Na. 5411: Mradi wa Kuboresha Upatikanaji wa Dawa, Vifaa Tiba na Vitendanishi
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na usambazaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi ambapo kwa zahanati na vituo vya afya umefikia asilimia 45, hospitali za wilaya (asilimia 52), hospitali za rufaa za mikoa (asilimia 87) na Hospitali ya Taifa (asilimia 66); Kuendelea na ununuzi wa vifaa tiba vya afya ya kinywa na macho kwa ajili ya Hospitali za Halmashauri 71 zilizokamilika; na ununuzi wa vifaa tiba vya zahanati 300; na ununuzi wa vifaa tiba katika vituo vya Afya 159 vya tozo. Jumla ya shilingi bilioni 164.0 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(q) Mradi Na. 5432: Uimarishaji wa Huduma za Chanjo
Hatua iliyofikiwa ni: Kutoa chanjo kwa watoto wa chini ya umri wa mwaka mmoja ambapo chanjo ya Penta3 kwa watoto 397,700 sawa na asilimia 107, chanjo ya Polio ya matone OPV3 asilimia 103, sindano (IPV) asilimia 107, Surua rubella 1 asilimia 109, Surua Rubella 2 asilimia 96, HPV1 asilimia 83 na HPV2 asilimia 62. Jumla ya shilingi bilioni 41.3 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(r) Mradi Na. 5492: Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI (NACP)
Hatua iliyofikiwa ni: Kutoa huduma ya tiba na matunzo kwa watu wapatao 1,582,109; kutolewa kwa huduma za PMTCT, ambapo vituo 7,120 sawa na asilimia 95 ya vituo vinavyotoa huduma ya afya ya uzazi na mtoto vinatoa huduma za PMTCT; kutolewa kwa huduma za upimaji VVU kwa wajawazito 1,793,204 kati ya 1,818,147 ya wajawazito wote waliohudhuria hudhurio la kwanza kliniki. Kati yao, wajawazito 52,012 sawa na asilimia 2.9 walibainika kuwa wanaishi na maambukizo ya VVU. Wajawazito 49,953 sawa na asilimia 96 walianzishiwa dawa za ARV na kuzuia maambukizi kwenda kwa mtoto. Watoto 34,364 sawa na asilimia 88 ya Watoto waliozaliwa na akina mama wanaoishi na VVU walipimwa kipimo cha kwanza cha uchunguzi wa maambukizi ya VVU katika umri wa miezi miwili na asilimia 0.7 walibainika kuwa na maambukizi. Jumla ya shilingi bilioni 1.6 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(s) Mradi Na.5498: Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma
Hatua iliyofikiwa ni: Kununuliwa na kusimikwa kwa mashine za kisasa aina ya Truenut 30 kwenye vituo vya kutolea huduma za Kifua Kikuu; kutolewa kwa huduma za mkoba kliniki tembezi (Mobile Vans outreach services) ambapo jumla ya watu 8,298 walichunguzwa na kupimwa Kifua Kikuu; na kutekeleza shughuli ya tambua TB ambapo jumla ya wagonjwa 155 sawa na asilimia 35 wa Kifua Kikuu Sugu waliogundulika walianzishiwa matibabu. Jumla ya shilingi bilioni 9.0 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(t) Mradi Na. 5406: Kudhibiti Magonjwa ya Kuambukiza na Yasiyo ya Kuambukiza
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa wodi mbili (2) kwa ajili ya matibabu ya magonjwa hatarishi na milipuko katika Hospitali ya Kisopwa ambapo utekelezaji wa umefikia asilimia 60; na kufanya tathmini ya huduma za mionzi nchini katika hospitali tano (5) - BMH, MBEYA, ORCI, KCMC na BUGANDO ili kuangalia huduma zinazotolewa. Jumla ya shilingi bilioni 4.1 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(u) Mradi Na. 2204: Mafunzo na Maendeleo ya Wataalamu
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ujenzi na ukarabati wa wa jengo la wodi maalum (Private wards) katika Chuo cha Tabora Clinical Officers Training Centre; kukamilika kwa ukarabati wa majengo ya vyuo vya Ngudu School of Environmental Health Science, Kilosa Clinical Officers Training Centre, Kagemu Environmental
Health Science, na Tabora Clinical Officers Training Centre. Aidha, ujenzi katika Chuo cha Korogwe SON umefikia asilimia 95, Mtwara COTC asilimia 95 na Nachingwea SON asilimia 48; na kutolewa kwa ufadhili wa masomo ya uzamili katika fani mbalimbali za afya kwa watumishi 373 ambapo kati ya hao 318 ni masomo ya kimkakati na 55 ni mafunzo kwa njia ya mafungu. Jumla ya shilingi bilioni 45.5 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(v) Mradi Na. 5416: Mipango ya Afya na Uendeshaji
Hatua iliyofikiwa ni: Kuwekwa kwa mfumo wa tiba mtandao katika hospitali nne (4); na kununuliwa na kuanza kutumika kwa vifaa vya TEHAMA katika hospitali za kanda za Bugando na Benjamin Mkapa na hospitali tatu (3) za kibingwa (Muhimbili, MOI na JKCI) na hospitali maalum moja (1) (Ocean Road Cancer Institute). Jumla ya shilingi bilioni 2.0 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(w) Mradi Na. 5401: Ujenzi wa Hospitali za Halmashauri
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa Hospitali 59 za halmashauri na ukarabati wa hospitali kongwe 19 za halmashauri ambapo utekelezaji wa miradi hiyo ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Jumla ya shilingi bilioni 233.4 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(x) Mradi Na. 5429: Huduma ya Afya ya Msingi
Hatua iliyofikiwa ni: kuendelea na ukamilishaji wa ujenzi wa zahanati 300 katika Halmashauri 184 ambapo utekelezaji upo katika hatua mbalimbali; na ununuzi wa vifaa na vifaa tiba kwa vituo vya afya 150, zahanati 300 na hospitali za Halmashauri 71. Jumla ya shilingi bilioni 69.15 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
2.3.5.2. Ustawi na Maendeleo ya Jamii
(i) Mradi Na. 6330: Ukarabati wa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ujenzi wa kumbi pacha za mihadhara (lecture theatre two in one) zenye uwezo wa kuhudumia wanafunzi 1,008; kukamilika kwa ujenzi wa bweni la wasichana la ghorofa nne (4) na ununuzi wa samani (viti, vitanda na magodoro) kwa ajili ya kumbi pacha za mihadhara na hosteli iliyojengwa katika Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru; kukamilika kwa ukarabati wa jengo la utawala katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii Rungemba; kukamilika kwa ukarabati wa maktaba yenye uwezo wa kuhudumia wanafunzi 120, ukumbi wa mihadhara wenye uwezo wa kuhudumia wanafunzi 260 na mabweni mawili yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 64 kila moja na kuendelea na ujenzi wa Bwalo la Chakula lenye uwezo wa kubeba wanafunzi 400 ambapo utekelezaji umefikia asilimia 15 katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii Ruaha; kukamilika kwa ujenzi wa Jengo la Utawala lenye vyumba vya ofisi 17 na kumbi mbili (2) ndogo za mikutano zenye uwezo wa kuhudumia watu 40 kwa wakati mmoja katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii Mlale; na kuendelea na ujenzi wa hosteli ya ghorofa mbili (2) yenye uwezo wa kuhudumia wanafunzi 600 katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii Uyole ambao umefikia asilimia 48; na kuendelea na ukarabati wa nyumba moja ya mtumishi, ufungaji wa mifumo ya TEHAMA na ununuzi wa Lori, gari (pick up) na mashine za kiuhandisi (Poker Machines na Mobile Block Machines) katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii Ufundi Mabughai. Jumla ya shilingi bilioni 3.97 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(ii) Mradi Na. 6259: Ujumuishaji wa Masuala ya Jinsia katika Mipango ya Maendeleo
Hatua iliyofikiwa ni: kuendelea kufanya mapitio ya Sera ya Maendeleo ya Wanawake na Jinsia (2000) na Mkakati wa utekelezaji wake (2005) ambayo ipo katika hatua ya uidhinishaji; kukamilika kwa tathmini ya utekelezaji wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA) na kuandaliwa kwa MTAKUWWA Awamu ya Pili; kukamilika kwa maandalizi ya Programu ya miaka mitano (2022 – 2026) ya Utekelezaji wa Ahadi za Nchi kwenye Jukwaa la Kimataifa la Kizazi chenye Usawa; kuanzishwa kwa Dawati la Jinsia katika Chuo Kikuu cha Dodoma na Chuo Kikuu cha Mtakatifu Yohana (Saint John University) na hivyo kufikisha idadi ya madawati 87 ya Jinsia yaliyoanzishwa mpaka sasa katika Vyuo Vya Elimu ya Juu na Kati; kufanyika kwa kampeni maalum ya kupinga ukatili dhidi ya watoto hususan ukeketaji katika mikoa yenye matukio mengi ya ukeketaji ya Manyara ambapo ukeketaji umefikia asilimia 58 na Mara (asilimia 31); kuanzishwa kwa mfumo wa huduma kwa mteja ambao utatumika kutoa huduma zote za Wizara; kuandaliwa kwa Mwongozo wa Uanzishwaji na Uendeshaji wa Dawati la Jinsia Katika Maeneo ya Umma na kutolewa mafunzo kwa waratibu 216 wa Dawati hilo. Jumla ya shilingi bilioni 2.07 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(iii) Mradi Na. 5414: Uhai na Maendeleo ya Mtoto
Hatua iliyofikiwa ni: Kuundwa kwa Madawati ya Ulinzi na Usalama wa Mtoto 1,393 katika shule za msingi na sekondari na Mabaraza ya Watoto 560 katika mikoa 8 (Rukwa, Arusha, Tanga, Dar es salaam, Pwani, Shinyanga, Dodoma na Geita); kutolewa kwa elimu ya uelewa katika jamii kuhusu Programu Jumuishi ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (2021/22 - 2024/25) kwa Waheshimiwa Wabunge 124 na kwenye mikoa 10 ya Tabora, Lindi, Dar es saalam, Morogoro, Arusha, Manyara, Mbeya, Rukwa, Kagera na Dodoma; kuunganisha viashiria vya Mpango wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto kutoka kwenye mifumo iliyopo katika Wizara za Kisekta; kutolewa mafunzo kwa wazazi 104 na vijana balehe 94 katika Halmashauri ya Wilaya Mbarali mkoani Mbeya kuhusu Programu ya Malezi Jumuishi kwa Kundi la Vijana Balehe; na kuendelea na maandalizi ya video fupi zenye ujumbe maalum ambazo zitatumika kwenye vyombo vya habari ikiwemo redio na Runinga kwa ajili ya kutoa tahadhari ya matumizi yasiyofaa ya mitandao ya kijamii kwa watoto, wazazi na jamii kwa ujumla. Jumla ya shilingi milioni 662.8 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(iv) Mradi Na. 6290: Uchakataji wa Taarifa na Uandaaji Programu Programming and Data Processing)
Hatua iliyofikiwa ni: Kufanyika kwa ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii Monduli, Mlale, Ruaha, Uyole, Taasisi ya Ustawi wa Jamii (Kampasi ya Kisangara) na Makazi ya Wazee Kibirizi (Kigoma), Kilima (Kagera) na Nandanga (Lindi). Jumla ya shilingi milioni 200 zimetumika hadi Aprili 2023.
2.3.5.3. Elimu
(a) Mradi Na. 4312: Programu ya Lipa Kulingana na Matokeo katika Elimu (EP4R)
Hatua iliyofikiwa ni: Kukarabatiwa kwa majengo yaliyoungua katika Chuo Kikuu Cha Dar es salaam Kampasi ya Zanzibar na ununuzi wa vifaa vya maabara; kuendelea na ujenzi wa Vyuo vitatu (3) vya Ualimu ambavyo ni Sumbawanga (asilimia 80), Dakawa (asilimia 80) na Mhonda (asilimia 80) na shule ya Mfano ya Sekondari Dodoma (asilimia 90); ujenzi wa shule mpya 40, madarasa 96, mabweni 4, nyumba za walimu 7 katika shule za msingi; ujenzi wa mabweni 62, madarasa 46, maabara 16, maktaba 4, nyumba za walimu 13, mabwalo 22 katika shule za sekondari; ujenzi wa ofisi tano (5) za wathibiti ubora wa shule katika halmashauri za Njombe, Tarime, Pangani, Bunda na Ubungo; kuendelea na ujenzi na ukarabati wa miundombinu mbalimbali katika vyuo vya ualimu Mamire (asilimia 90), Vikindu (asilimia 70), Songea (asilimia 5), Singachini (asilimia 5) na Katoke (asilimia 5); kuendelea na ukarabati wa Shule Kongwe 61 (msingi 45, Sekondari 16) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 80; na kununuliwa kwa mashine za uchapaji katika kiwanda cha Press A. Jumla ya shilingi bilioni 51.48 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(b) Mradi Na. 4321: Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Elimu ya Msingi (MMEM) LANES II
Hatua iliyofikiwa ni: Kufanyika kwa asilimia 40 ya tathmini ya ubora wa shule kwa shule 5812 Tanzania Bara; kuendelea kwa MEWAKA katika Halmashauri 144 zilizopo katika mikoa 26; kuchapishwa kwa nakala 372,773 ya vitabu vya uchambuzi wa mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi – CIRA – PSLE 2021; kuendelea na uchapaji wa nakala 53,510 za vitabu vya uchambuzi wa upimaji wa stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu - PIRA – SFNA na nakala 314,700 za vitabu vya uchambuzi wa upimaji wa darasa la IV – PIRA – SFNA ambapo utekelezaji umefikia asilimia 50; kuendelea na ukamilishaji wa ujenzi wa madarasa 128 ya mfano ambapo utekelezaji umefikia asilimia 50. Jumla ya shilingi bilioni 17.64 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(c) Mradi Na. 4319: Mradi wa Kuboresha Elimu ya Awali na Msingi (Boost Primary Student Learning)
Hatua iliyofikiwa ni: Kufanya tathmini ya mahitaji ya miundombinu kwenye Shule za Msingi 17,182 zilizopo katika Halmashauri zote; Mafunzo kwa Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakurugenzi wa Halmashauri, Maafisa Elimu wa Mikoa, timu za utekelezaji wa mradi ngazi za Mkoa na Halmashauri ambapo jumla ya watendaji 2,888 wamepatiwa mafunzo; kutoa Mafunzo ya Walimu Kazini (MEWAKA) kwenye shule za Msingi 2,952 kwenye Halmashauri 26 (Halmashauri 1 kila Mkoa) za majaribio; na kukamilika kwa uaandaji wa miongozo ya utawala bora na kiongozi cha usimamizi wa shule pamoja na moduli 12 za mafunzo endelevu ya walimu kazini. Jumla ya shilingi bilioni 265.08 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(d) Mradi Na. 3280: Programu ya Huduma ya Maji, Elimu ya Afya na Usafi wa Mazingira Shuleni – SWASH
Hatua iliyofikiwa ni: Kufanya ufuatiliaji wa awamu ya pili ya ujenzi wa matundu ya vyoo 6,096, vifaa 1,655 vya kunawia mikono na matenki 238 ya kuhifadhia maji katika Shule za Msingi 235 zilizo katika Halmashauri 86; na kuandaa rasimu ya Mpango wa Kitaifa wa Ugharimiaji na Uwekezaji katika Huduma za Maji na Usafi na Mazingira Shuleni (National School WASH Costed Plan and Investment Case). Jumla ya shilingi bilioni 19.02 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(e) Mradi Na. 4390: Mradi wa Kuboresha Elimu ya Sekondari (SEQUIP) Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa shule mpya 232 za Sekondari za kata zenye uwezo wa kuhudumia wanafunzi 400 kila moja katika kata zisizokuwa na shule za Sekondari ambapo utekelezaji umefikia asilimia 75; ujenzi wa shule 10 maalumu za bweni (kidato cha 5 & 6) za wasichana kwa masomo ya Sayansi na upanuzi wa shule 11 umefikia asilimia 50; kukamilika kwa upanuzi wa shule kongwe 18 za sekondari na vituo nane (8) vya Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima ili vitumike kutoa elimu kwa njia mbadala kwa wasichana walio nje ya mfumo rasmi; na kuwezesha na kutoa mafunzo kazini kwa walimu wapatao 736 wa masomo ya Sayansi na Hisabati kama wawezeshaji wa kitaifa. Jumla ya shilingi bilioni 39.72 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(f) Mradi Na. 6390: Mamlaka ya Elimu Tanzania – TEA
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa ofisi za walimu katika shule saba(7) za sekondari, madarasa 78, (asilimia 28), nyumba 40 za walimu (asilimia 11)na matundu 1,008 (asilimia 13) ya vyoo katika shule 80 za msingi na 22 za sekondari; mabweni 10 ya wasichana katika shule 10 za sekondari (asilimia 10); kutolewa kwa mafunzo kwa wanufaika 5,981 kuhusu ujuzi katika nyanja za Kilimo, Kilimo uchumi, utalii na huduma za utalii, usafirishaji, Nishati na Teknolojia ya habari na mawasiliano; kutolewa kwa mafunzo ya ufundi stadi kwa wananchi 1,627 wanaotoka katika kaya maskini ikiwemo vijana, wanawake na walemavu; na kufikia asilimia 89 ya ununuzi wa vifaa vya kujifunzia na kuboresha miundombinu kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika shule tisa (9) za msingi na shule moja (1) ya sekondari. Jumla ya shilingi bilioni 7.0 fedha zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(g) Mradi Na. 6363: Ukarabati wa Chuo cha Ufundi Arusha - ATC
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ujenzi wa bweni la wanafunzi wa kike lenye uwezo wa kuhudumia wanafunzi 428 ambapo utekelezaji umefikia asilimia 99.46; kuendelea na ukamilishaji wa ujenzi wa madarasa nane (8) yenye uwezo wa kuhudumia wanafunzi 880 kwa wakati mmoja, maabara sita (6) zenye uwezo wa kuhudumia wanafunzi 270 kwa wakati mmoja na ofisi 26 zenye uwezo wa kuhudumia watumishi 104 ambapo utekelezaji umefikia asilimia 99.4; kuendelea na ukamilishaji wa ujenzi wa hospitali ya taaluma na tiba (polyclinic) ambapo utekelezaji umefikia asilimia 95; na kuendelea na ujenzi wa kliniki itakayohudumia wanafunzi, wafanyakazi na wananchi wa maeneo jirani ambapo utekelezaji umefikia asilimia 24.43. Jumla ya shilingi bilioni 1.0 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(h) Mradi Na. 4397: Ujenzi na Ukarabati wa Vyuo vya Ufundi Stadi
Hatua iliyofikiwa ni: kuendelea na ujenzi na ukarabati wa Vyuo vya Ufundi stadi vya mikoa ya Dodoma (asilimia 90), Mtwara (asilimia 94); ujenzi wa Vyuo vya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi katika Wilaya 25 (asilimia 98). Aidha, Chuo cha Wilaya ya Mbarali na Chuo cha Wilaya ya Kishapu vimeanza kutoa mafunzo. Jumla ya shilingi bilioni 31.0 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(i) Mradi Na. 4323: Kuendeleza Elimu ya Ualimu - TESP
Hatua iliyofikiwa ni: Kukamilika kwa ujenzi wa Chuo cha Ualimu Kabanga; kuendelea na ujenzi na ukarabati wa maabara za sayansi, maktaba na vyumba vya TEHAMA katika Vyuo saba (7) vya Butimba (asilimia 100), Morogoro (asilimia 90), Tukuyu (asilimia 92), Kasulu (asilimia 90), Patandi (asilimia 91), Mpwapwa (asilimia 70) na Dakawa (asilimia 70); kuendelea na ununuzi wa vifaa vya TEHAMA ambapo kazi ya uunganishaji wa vyuo 35 vya ualimu katika Mkongo wa Taifa umefikia asilimia 40; ununuzi wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia kwa vyuo vya ualimu 35; ununuzi wa vifaa na madawa ya maabara katika vyuo 10 vya ualimu vya sayansi; na kuendelea na uundaji wa mfumo wa usahihishaji wa kielektroniki ambapo utekelezaji umefikia asilimia 85. Jumla ya shilingi bilioni 12.35 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023
(j) Mradi Na. 4340: Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu
Hatua iliyofikiwa ni: Kutolewa kwa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 652.1 kwa wanafunzi 202,877 (wanafunzi 72,973 ni wa mwaka wa kwanza na wanafunzi 129,904 ni wanaoendelea na masomo); kuwezesha ukusanyaji wa mikopo iliyoiva ya shilingi bilioni 141.3 sawa na asilimia 61 ya lengo mwaka mzima wa bajeti; kutolewa kwa shilingi bilioni 2.75 kwa ajili ya kudhamini wanafunzi 593 wenye ufaulu wa juu zaidi katika programu za Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati (STEM) kupitia Samia Scholarship; na kuanzishwa kwa Kituo Mahsusi cha Wateja. Jumla ya shilingi bilioni 655.51 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(k) Mradi Na. 4392: Mradi wa Elimu wa Kukuza Stadi za Kazi na Ujuzi ya ESPJ
Hatua iliyofikiwa ni: Kuendelea na ukarabati na ujenzi wa vyuo 14 vya maendeleo ya wananchi (FDCs) ambapo ujenzi umefikia asilimia 95, vyuo 25 vya Ufundi Stadi vya Wilaya (asilimia 96) na Chuo cha Ufundi cha Dodoma (asilimia 78); kutoa mafunzo ya ujuzi kwa vijana 2,373 walio katika mazingira magumu kupitia mpango wa Bursary Scheme na mafunzo kwa watanzania 5,030 kupitia programu ya mafunzo ya Utarajali na Uanagenzi; na kuwajengea uwezo watumishi 2,400 wa VETA na FDCs kwa lengo la kuimarisha stadi za ujuzi. Jumla ya shilingi bilioni 27.7 zimetumika katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Aprili, 2023.
(l) Mradi Na. 4315: Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (Higher Education for Economic Transformation Project - HEET)
Hatua iliyofikiwa ni: kuendelea na taratibu za manunuzi ya kuwapa wakandarasi na washauri elekezi kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu katika vyuo 22 vya elimu ya juu vinavyonufaika na mradi; kuendelelea na taratibu za kuhuisha na kuandaa mitaala mipya ili iendane na mahitaji ya soko la ajira ikiwemo kutoa mafunzo, kuandaa vigezo vya ulinganifu wa progamu; kutoa mafunzo ya kushughulikia malalamiko (washiriki ), kuimarisha ushirikiano na sekta binasi (Industrial linkages) (washiriki 66); kuendelea kutoa mafunzo ya muda mrefu kwa watumishi 327 (ndani na nje ya nchi) ambapo 220 ni uzamivu (Phd) na 107 ni uzamili (masters); kuanza maboresho ya miundombinu ya TEHAMA kwa kutoa mafunzo ya ufundishaji na ujifunzaji kwa njia ya masafa na kuongeza kasi ya Interneti, kuanzisha madawati ya jinsia 21 katika vyuo vya elimu ya juu 21 vinavyonufaika na mradi. Jumla ya shilingi bilioni 32.3 zimetumika katika kipindi cha nusu mwaka.
(m)