BABU ACHOMA NYUMBA, APOTEZA MAISHA NA WATOTO WAKE WATATU

 

Watu wanne familia moja wamefariki dunia kwa kuteketea na moto baada ya baba wa familia hiyo Aman Madumba (72), kujifungia chumbani na watoto hao kisha kuchoma nyumba moto.


Familia hiyo ya kijiji cha Malolo B kilichopo Wilayani Kilosa mkoani Morogoro inajumuisha baba huyo na watoto wake watatu ambao ni Habibu Aman (10), Sadick Aman (8) wote wa darasa la tatu na Bahati Aman (5).

 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, ACP Alex Mkama amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa uchunguzi unaendelea ili kubaini chanzo cha tukio hilo.

Mjukuu wa marehemu, Mwanjaa Madumba amesema majira ya saa saba usiku wa kuamkia leo Mei 5, 2023 akiwa amelala aliona moshi mkubwa chumbani kwake na alipotoka aligundua ulikuwa ukitokea upande wa chumba cha babu yake.

“Nilipiga kelele Watu wakafika na kuzima moto huo na walipofungua mlango wa chumbani walikuta wote wanne wameteketea na moto,” alisimulia mjukuu huyo huku ikidaiwa huenda msongo wa mawazo umesababisha hali hiyo kwani marehemu huyo alitengana na mkewe.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments