MWAMBA AFUTA HARUSI BAADA YA MCHUMBA KUMPELEKEA X WAKE KADI YA MUALIKO NA KUPAKULIANA ASALI


Mwanamke mmoja raia wa Nigeria amejawa na machozi baada ya mchumba wake kufuta harusi yao.

Mrembo huyo alianika suala hilo kwenye kundi la Facebook na kuomba ushauri wa wanamtandao.

Alisema alimtembelea tu mpenzi wake wa zamani ili kumpa kadi ya mwaliko kwenye harusi yake, lakini aliishia kurusha roho na jamaa huyo.

Kwa bahati mbaya, mume wake mtarajiwa aligundua kuhusu uzinzi wake baada ya kudukua simu yake.

Baadaye mwanaume huyo aliagiza kwamba matayarisho yote ya harusi yasitishwe mara moja. 

Mrembo huyo alilalama kuwa: "Mbele yangu, aliwaita wazazi wote wawili na kuwataka wasitishe maandalizi yote ya harusi. Walipouliza kwanini, aliwaambia nitaeleza vizuri zaidi. Aliniacha nyumbani kwake na kwenda hotelini na hakurudi" 

Maoni ya wanamtandao 

Kingsley Uchenna alisema: "Upuuzi. Kwa nini ulikubali mtoto wa mtu wakati bado unampenda ex wako? Maisha haya EEE. Mwanaume amefanya vizuri. Anaamini unaweza kufanya zaidi atakapokuoa!"

@Adeoye Augustine Okusanya alitoa maoni: "Kwa nini ulishuka chini namna hii? Ni kama bado una hisia ya kimapenzi na mpenzi wako wa zamani."

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments