BIBI BIKRA WA MIAKA 123 AOMBA 'CONNECTION' YA MWANAUME WA KUMUOA... "SIJAWAHI KABISA KUFANYA"




Bikizee Theresa Nyirakajumba ametoa wito kwa watu kumuunganisha na mwanaume atakayemuoa.

Katika video iliyosambazwa kupitia YouTube, ajuza huyo alifichua kuwa hajawahi kuwa na uhusiano na mwanamume yeyote tangu kuzaliwa.

Akizungumza na Afrimax English, alisimulia jinsi alivyokataa wachumba kwa sababu alikuwa akimngoja mwanaume kamili ambaye angehisi uhusiano naye. Cha kusikitisha ni kwamba hilo halijawahi kutokea, na sasa, akiwa na umri wa miaka 123, anaomba msaada wa kujipatia mume.

Alisema kwenye video hiyo: "Naitwa Theresa Nyirakajumba, sijawahi kuona uchi wa mwanaume. Kwa miaka 123, ninaishi kwa tamaa isiyotimizwa, tumaini potovu na moyo wa ujasiri wa kusubiri kwamba siku moja ataibuka mwanaume na kuikumbatia nafsi yangu.”

Maoni ya wanamtandao

@chesterphiri7523 aliandika: "Ikiwa "Ubikra" ni mtu, basi Mama huyu ni mmoja. Urefu wa maisha pekee ni zaidi ya furaha ambayo angeweza kupata kutoka kwa mwanadamu. Utukufu kwa Mungu."

@francine8905 alitoa maoni: "Ameishi kwa muda mrefu bila maumivu ya moyo. Bahati iliyoje. Sababu ya kuwa na miaka 123 ni kwa sababu amejipenda mwenyewe. Anahitaji tu mahali pazuri pa kuishi, kwa kweli na labda hana hisia ya wanaume."

@gillianwalcott1857 aliongeza: "Umri wa miaka 123 na ninataka mwanamume. Bado alipata hisia za aina hiyo kwa mwanamume. Afadhali aende kumtumikia bwana."

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments