YANGA SC YAICHAPA TP MAZEMBE 1-0 UGENINI


**********************

NA EMMANUEL MBATILO

KLABU ya Yanga imefanikiwa kuondoka na ushindi kwenye mechi yake ya mwisho hatua ya makundi Kombe la Shirikisho barani Afrika baada ya kufanikiwa kuichapa TP Mazembe kwa bao 1-0 , mchezo uliopigwa nchini DR Congo.

Yanga SC imefanikiwa kupata bao kipindi cha pili likifungwa na kiungo mshambuliaji Farid Musa ambaye aliingia akitokea benchi akipihwa na Mudathir Yahya mabadiliko ambayoyalizaa matunda.

Yanga sasa inaenda hatua ya Robo Fainali akiwa anaongoza kundi akijikusanyia alama 13 katika michezo sita hatua ya makundi.

Yanga iliwakosa baadhi ya wachezaji kikosi cha kwanza ambapo walimkosa Djidji Diara ambaye ni goli kipa namba moja, Khalid Aucho, Aziz Ki na Morrison .

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments