WAHITIMU 22 KUTOKA NCHINI KENYA WATUNUKIWA VYETI NIT

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Bw. Abdi Mkeyenge akiwatunuku vyeti Wahitimu 22 kutoka nchini Kenya wa kozi ya muda mfupi ya Cargo tallyingi for international shipping inayohusika na kuhudumia shehena ndani na nje ya nchi kwenye Mahafali ambayo yamefanyika katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) leo Aprili 6,2023 Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Bw. Abdi Mkeyenge akiwatunuku vyeti Wahitimu 22 kutoka nchini Kenya wa kozi ya muda mfupi ya Cargo tallyingi for international shipping inayohusika na kuhudumia shehena ndani na nje ya nchi kwenye Mahafali ambayo yamefanyika katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) leo Aprili 6,2023 Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Bw. Abdi Mkeyenge akiwatunuku vyeti Wahitimu 22 kutoka nchini Kenya wa kozi ya muda mfupi ya Cargo tallyingi for international shipping inayohusika na kuhudumia shehena ndani na nje ya nchi kwenye Mahafali ambayo yamefanyika katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) leo Aprili 6,2023 Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Bw. Abdi Mkeyenge akizungumza katika Mahafali ya Wahitimu 22 kutoka nchini Kenya wa kozi ya muda mfupi ya Cargo tallyingi for international shipping inayohusika na kuhudumia shehena ndani na nje ya nchi ambayo yamefanyika katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) leo Aprili 6,2023 Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Bw. Abdi Mkeyenge akizungumza katika Mahafali ya Wahitimu 22 kutoka nchini Kenya wa kozi ya muda mfupi ya Cargo tallyingi for international shipping inayohusika na kuhudumia shehena ndani na nje ya nchi ambayo yamefanyika katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) leo Aprili 6,2023 Jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT), Prof. Zacharia Mganilwa akizungumza katika Mahafali ya Wahitimu 22 kutoka nchini Kenya wa kozi ya muda mfupi ya Cargo tallyingi for international shipping inayohusika na kuhudumia shehena ndani na nje ya nchi ambayo yamefanyika katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) leo Aprili 6,2023 Jijini Dar es Salaam
Mkuu wa Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT), Prof. Zacharia Mganilwa akizungumza katika Mahafali ya Wahitimu 22 kutoka nchini Kenya wa kozi ya muda mfupi ya Cargo tallyingi for international shipping inayohusika na kuhudumia shehena ndani na nje ya nchi ambayo yamefanyika katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) leo Aprili 6,2023 Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia Mahafali ya Wahitimu 22 kutoka nchini Kenya wa kozi ya muda mfupi ya Cargo tallyingi for international shipping inayohusika na kuhudumia shehena ndani na nje ya nchi ambayo yamefanyika katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) leo Aprili 6,2023 Jijini Dar es Salaam.
Wahitimu 22 kutoka nchini Kenya wa kozi ya muda mfupi ya Cargo tallyingi for international shipping inayohusika na kuhudumia shehena ndani na nje ya nchi wakiwa kwenye mahafali ya kumaliza kozi hiyo leo Aprili 6,2023 katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Bw. Abdi Mkeyenge akipata picha ya pamoja na wahitimu 22 kutoka nchini Kenya wa kozi ya muda mfupi ya Cargo tallyingi for international shipping inayohusika na kuhudumia shehena ndani na nje ya nchi.. Hafla ya kuwatunuku vyeti wahitimu hao imefanyika leo Aprili 6,2023 NIT Jijini Dar es Salaam.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

**************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

CHUO Cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kimewatunuku vyeti wahitimu 22 kutoka nchini Kenya wa kozi ya muda mfupi ya Cargo tallyingi for international shipping inayohusika na kuhudumia shehena ndani na nje ya nchi.

Akizungumza mara baada ya kuwatunuku vyeti wahitimu hao, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Bw. Abdi Mkeyenge amesema Sekta ya Usafirishaji kwa njia ya Maji umepiga hatua katika Ukanda wa Afrika Mashariki hivyo amewataka vijana kuchangamkia fursa hiyo kwa kusoma kozi za kuhudumia Shehena.

Sekta hii imepiga hatua katika ukanda wa Afrika Mashariki hivyo ni Muhimu kuwa na wataalamu wa kutosha watakaokuwa na uwezo mathubuti wa kuhudumia eneo hilo". Amesema

Nae Mkuu wa Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT), Prof. Zacharia Mganilwa amesema hatua ya wanafunzi hao 22 kutoka nchini Kenya ni matokeo ya ufadhili wa Benki ya Dunia katika vituo vya umahiri kwa nchi tatu ikiwemo Ethiopia Kenya na Tanzania ambao unawezesha wakufunzi na wanafunzi kubadilisha ujuzi na mbinu za ufundishaji kwa vyuo husika katika nchi hizo.

Miongoni mwa wanafunzi waliohitimu mafunzo hayo ya mwezi mmoja kutoka Chuo cha Kenya Coast National Polytechnic (KCNP) Mombasa nchini kenya wamesema ushirikiano huo ni muhimu katika kuendeleza taaluma na ujuzi wa wanafunzi katika vyuo vinavyonufaika na ufadhili wa Bank ya Dunia.

Kuhitimu kwa wanafunzi hao kutoka nchini Kenya ni awamu ya kwanza ambapo pamoja na mambo mengine imebainishwa kuwa hatua hiyo itasaidia sana kukuza uchumi wa kikanda kupitia sekta ya usafirishaji kwa njia ya maji.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments