MILEMBE AUAWA NA WASIOJULIKANA KISHA KUTUPWA KWENYE NYUMBA YAKE


Milembe Selemani(43)

Milembe Selemani(43), mkazi wa mtaa wa Mseto halmashauri ya mji Geita, aliyekuwa kitengo cha ugavi mgodi wa GGML, ameuawa kwa kukatwa viungo vya mwili wake na watu wasiojulikana na mwili wake kutupwa kwenye moja ya nyumba alizokuwa anajenga zilizopo mtaa wa Mwatulole Kata ya Buhalahala.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la polisi mkoa wa Geita Berthaneema Mlay, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo huku watu wanne wakishikiliwa kwa ajili ya uchunguzi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments