DITOPILE AUNGANA NA WANA MPWAPWA KWA IFTAR, WAMUOMBEA DUA RAIS SAMIA


Katika Muendelezo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Dodoma Mhe. Mariam Ditopile ameungana na Waumini Mbalimbali katika Msikiti Mkuu wa Mpwapwa Mjini Mkoani Dodoma katika Iftari na Dua Maalum ya kuiombea Nchi na kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Kabla ya Dua hiyo Mhe. Mbunge alitembelea Gereza Kuu la Mpwapwa na kuwapelekea Wafungwa sadaka ya Futari na mahitaji mbalimbali.

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Dodoma Mhe Mariam Ditopile anaendelea kuwatakia Waislamu wote nchini Ramadhani njema.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments