LEMBELI ATEMBELEA MAENEO YA KIHISTORIA NEW YORK - MAREKANI..ASEMA TANZANIA INALIPA KIPAUMBELE SUALA LA UHIFADHI NA ULINZI WA MAZINGIRA


Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Jane Goodall Tanzania Bw. James Lembeli ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya Taasisi hiyo nchini Marekani na Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kahama akiwa katika Bustani ya New York City Park.
**
Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Jane Goodall Tanzania Bw. James Lembeli ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya Taasisi hiyo nchini Marekani na Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kahama amesema Tanzania,kama ilivyo kwa nchi nyingine inalipa kipaumbele suala la ulinzi wa mazingira na uhifadhi kuepusha janga linaloweza kutokea kutokana na athari za mabadiliko ya tabia nchi ambazo tayari katika nchi nyingine zimeanza kuleta madhara makubwa.


Ametaja madhara hayo ni mafuriko,vimbunga,joto kali na kuyeyuka kwa theluji huko antaktika na ktk vilele vya milima ikiwemo kilimanjaro kuwa ni mifano halisi.


Lembeli amesema hayo juzi mjini New York wakati akiongea na wadau wa masuala ya mazingira kutoka sehemu mbambali za Dunia wakati wa ghahla ya kumpongeza mwanzilishi taasisi ya Jane Goodall kutimiza miaka 89 na miaka karibu miaka 63 tangu atue Kigoma,Tanzania kuanza kazi ya utafitiwa wa Sokwe na wanyama wengine aina ya Nyani.


Amesema,Kwa kutambua msimamo wa Tanzania ktika sekta za mazingira na uhifadhi,serikali ya Marekani kupitia shirika lake la misaada USAID ilitoa msaada wa Dola milioni 20 kwa ajili ya mradi wa kuimarisha na kuboresha mazingira katika mikoa ya Kigoma na Katavi ulioanza mwaka 2013 na ambao utamalizika novemba mwaka huu.


Mradi huo umejikita hususani katika elimu ya kuhifadhi misitu ya asili katika maeneo hayo,afya na elimu ya kujitegemea hususani Amina mama na vijana vijiji.


Taasisi ya Jane Goodall ambayo chimbuko lake ni Gombe, Kigoma Tanzania ambako muasisi wake (Jane Goodall) alifika kuanza kazi ya utafiti wa Sokwe na wanyama aina ya nyani inafanya kazi ktk nchi zaidi ya 60 ulimwenguni ikiwa imejikita kuhusani katika suala la elimu ya uhifadhi wa mazingira kupitia programu yake ya vijana ya Roots and Shoot-lengo likiwa ni kuiponya Dunia na tatizo la uharibifu wa mazingira hivyo kuwa sehemu Bora ya kuishi wanadamu na viumbe vingine.


Akiwa New York,lembeli licha ya kuhudhuria kikao cha Bodi ya Wakurungenzi ya Jane Goodall-Marekani pia alipata fursa ya kukutana na watu mbalimbali na kutembelea maeneo mbalimbali ya kihistoria ikiwa pamoja na kanisa Kuu katoliki la Mtakatifu Patrick ambapo alipata fursa ya kuingia na kusali, Bustani kubwa ya mjini New York, New York Central Park, Makumbusho ya Brooklyn na Lockfeller Center.


Sherehe ya miaka 89 ya kuzaliwa Jane ilifanyika katika hoteli maarufu ya mjini New York Litz Calton.
Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Jane Goodall Tanzania Bw. James Lembeli ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya Taasisi hiyo nchini Marekani na Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kahama akiwa katika Bustani ya New York City Park
Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Jane Goodall Tanzania Bw. James Lembeli ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya Taasisi hiyo nchini Marekani na Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kahama akiwa katika Bustani ya New York City Park
Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Jane Goodall Tanzania Bw. James Lembeli ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya Taasisi hiyo nchini Marekani na Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kahama akiwa katika  kanisa kuu la Mtakatifu Patrick-New York
Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Jane Goodall Tanzania Bw. James Lembeli ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya Taasisi hiyo nchini Marekani na Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kahama akiwa katika  kanisa kuu la Mtakatifu Patrick-New York
Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Jane Goodall Tanzania Bw. James Lembeli ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya Taasisi hiyo nchini Marekani na Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kahama akiwa katika Rockefeller Center
Studio za radio na NBC tv

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments