LORI LAUA WAENDESHA BODABODA ZAIDI YA 10 KIJIWENI


Watu kadhaa wamepoteza maisha baada ya lori lililokuwa likisafirisha changarawe kupoteza mwelekeo na kugonga kundi la bodaboda waliokuwa wameegesha eneo lao (kijiweni) mjini Migori nchini Kenya.

Tukio hilo la asubuhi ya Jumamosi - Aprili 8,2023 limeshuhudia umati mkubwa wa watu ukimiminika eneo la tukio ili kuwanusuru majeruhi na kuwakimbiza hospitalini kwa matibabu. 

Kwa mujibu wa raia mmoja aliyeshuhudia na kuzungumza na runinga ya TV47, breki za lori hilo zilifeli na kuingia katika kundi hilo la bodaboda ambao walikuwa wanasubiri abiria. 

Ajali hiyo imefanyika karibu na shule ya msingi ya Migori. Eneo la tukio lilikuwa limejaa damu na miili. 

Vyuma pia vilikuwa vimetapakaa eneo hilo.

Eneo la tukio linaripotiwa kuwa na zaidi ya miili kumi huku ambulansi na wazima moto kutoka kwa serikali ya kaunti ya Migori wakifika eneo la ajali hiyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments