WEADO WAENDESHA KAMPENI YA CHANJO YA UVIKO-19, KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA KIJIJI CHA ILOBASHI WILAYANI SHNYANGA


Wananchi wa kijiji cha Ilobashi Kata ya Masengwa wilayani Shinyanga wakiwa kwenye Kampeni ya uhamasa ya Chanjo ya UVIKO-19, pamoja na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia zikiwamo mimba na ndoa za utotoni kutoka Shirika la WEADO.

Na Marco Maduhu, SHINYANGA

SHIRIKA la Women Elderly Advocacy And Development Organization (WEADO) limeendesha Kampeni ya kuhamasisha wananchi hasa makundi ya Wanawake, Vijana na Wazee kuchanja Chanjo ya UVIKO-19 katika kijiji cha Ilobashi Kata ya Masengwa wilayani Shinyanga.

Zoezi hilo la Hamasa ya Kampeni ya Chanjo ya UVIKO-19, imefanyika leo Machi 3, 2023 na kutolewa na wataalamu wa Afya na viongozi wa Kata ya Masengwa, kwa ufadhili wa Shirika la watoto Duniani UNICEF kupitia Mdau kiongozi Help Age Tanzania.

Elimu hiyo ya Hamasa ya Chanjo ya UVIKO-19 imeendana pia na Kampeni ya kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia likiwamo tatizo la mimba na ndoa za utotoni, kwa ufadhili wa Shirika la Foundation For Civil Society.

Mganga kutoka Zahanati ya Ilobashi Dk. Victor Thomas, akitoa elimu ya Chanjo ya UVIKO-19 kwa wananchi wa Kijiji cha Ilobashi, amewasihi wajitokeze kwa wingi kuchanja ikiwa Chanjo ni salama na adhina madhara yoyote, na kupuuza upotoshaji ambao umekuwa ukienezwa dhidi ya Chanjo hiyo.

Amesema tangu Chanjo ya UVIKO-19 ianze kutolewa hapa nchini hakuna mtu yoyote ambaye amelalamika kupata madhara ya kiafya, na kuwasihi wananchi wajitokeze kupata Chanjo ili wapate Kinga ambayo itawalinda siku wakipata maambukizi ya virusi vya Corona wasipate madhara makubwa.

“Wananchi Chanjo ya UVIKO-19 ni salama na haina madhara yoyote na inatolewa bure hakuna malipo, jitokezeni kuchanja ili muwe salama siku mkipata maambukizi ya virusi vya Corona,”amesema Dk. Thomas.

Naye Katibu wa Baraza la Wazee mkoani Shinyanga Anderson Lyimo ambaye pia ni Katibu wa Baraza la Wazee Taifa, amewataka Wazee kujitokeza kwa wingi kupata Chanjo ya UVIKO-19, na kupuuza upotoshaji sababu wao kinga zao zimeshashuka ili wajilinde na ugonjwa wa Virusi vya Corona pale watakapopata maambukizi.

Kwa upande wake Ofisa Maendeleo Kata ya Masengwa wilayani Shinyanga Atupokile Maseta, akizungumzia masuala ya kupinga ukatili, amewataka wananchi wapaze sauti pale wanapokuwa wakifanyiwa vitendo vya ukatili, na siyo kunyamaza kimya, pamoja na kutoa ushirikiano mahakamani ili watuhumiwa wafungwe jela na kuacha kumaliza kesi kimya kimya ili kutokomeza tatizo hilo.

Aidha, Shirika la WEADO linatekeleza Mradi wa Kampeni ya kuhamasisha Chanjo ya UVIKO-19 kwa wananchi hasa makundi ya Wazee, Vijana na Wanawake, pamoja na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia zikiwamo mimba na ndoa za utotoni wilayani Shinyanga.

Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Shinyanga Lidya Kwesigabo akitoa elimu ya hamasa ya Chanjo ya UVIKO-19, pamoja na kupinga vitendo vya ukatili zikiwamo mimba na ndoa za utotoni kwa Wananchi wa Kijiji cha Ilobashi Kata ya Masengwa wilayani Shinyanga.

Afisa Maendeleo ya jamii Kata ya Masengwa wilayani Shinyanga Atupokile Maseta akitoa elimu ya hamasa ya Chanjo ya UVIKO-19, pamoja na kupinga vitendo vya ukatili zikiwamo mimba na ndoa za utotoni kwa Wananchi wa Kijiji cha Ilobashi.

Mganga wa Zahanati ya Ilobashi wilayani Shinyanga Dk. Victor Thomasi akitoa elimu ya hamasa ya Chanjo ya UVIKO-19 kwa wananchi wa Kijiji cha Ilobashi Kata ya Masengwa wilayani Shinyanga.

Katibu wa Baraza la Wazee mkoani Shinyanga Anderson Lyimo akitoa elimu ya hamasa ya Chanjo ya UVIKO-19, pamoja na kupinga vitendo vya ukatili kwa wananchi wa Kijiji cha Ilobashi Kata ya Masengwa wilayani Shinyanga.


Mwezeshaji wa masuala ya kupinga vitendo vya ukatili katika Kijiji cha Ilobashi Kata ya Masengwa wiayani Shinyanga Mary Lutinya akitoa elimu ya kupinga vitendo vya ukatili ndani ya jamii zikiwamo mimba na ndoa za utotoni.

Wananchi wa Kijiji cha Ilobashi Kata ya Masengwa wilayani Shinyanga wakiwa kwenye elimu ya hamasa ya kuchanja Chanjo ya UVIKO-19, pamoja na kupinga vitendo ya ukatili wa kijinsia zikiwamo mimba na ndoa za utotoni.

Elimu ya hamasa ya Chanjo ya UVIKO-19 ikiendelea pamoja na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia zikiwamo mimba na ndoa za utotoni.

Elimu ya hamasa ya Chanjo ya UVIKO-19 ikiendelea pamoja na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia zikiwamo mimba na ndoa za utotoni.

Elimu ya hamasa ya Chanjo ya UVIKO-19 ikiendelea pamoja na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia zikiwamo mimba na ndoa za utotoni.

Elimu ya hamasa ya Chanjo ya UVIKO-19 ikiendelea pamoja na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia zikiwamo mimba na ndoa za utotoni.

Elimu ya hamasa ya Chanjo ya UVIKO-19 ikiendelea pamoja na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia zikiwamo mimba na ndoa za utotoni.

Elimu ya hamasa ya Chanjo ya UVIKO-19 ikiendelea pamoja na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia zikiwamo mimba na ndoa za utotoni.

Elimu ya hamasa ya Chanjo ya UVIKO-19 ikiendelea pamoja na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia zikiwamo mimba na ndoa za utotoni.
Elimu ya hamasa ya Chanjo ya UVIKO-19 ikiendelea pamoja na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia zikiwamo mimba na ndoa za utotoni.

Elimu ya hamasa ya Chanjo ya UVIKO-19 ikiendelea pamoja na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia zikiwamo mimba na ndoa za utotoni.

Elimu ya hamasa ya Chanjo ya UVIKO-19 ikiendelea pamoja na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia zikiwamo mimba na ndoa za utotoni.

Elimu ya hamasa ya Chanjo ya UVIKO-19 ikiendelea pamoja na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia zikiwamo mimba na ndoa za utotoni.

Elimu ya hamasa ya Chanjo ya UVIKO-19 ikiendelea pamoja na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia zikiwamo mimba na ndoa za utotoni.

Elimu ya hamasa ya Chanjo ya UVIKO-19 ikiendelea pamoja na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia zikiwamo mimba na ndoa za utotoni.

Elimu ya hamasa ya Chanjo ya UVIKO-19 ikiendelea pamoja na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia zikiwamo mimba na ndoa za utotoni.

Elimu ya hamasa ya Chanjo ya UVIKO-19 ikiendelea pamoja na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia zikiwamo mimba na ndoa za utotoni.

Elimu ya hamasa ya Chanjo ya UVIKO-19 ikiendelea pamoja na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia zikiwamo mimba na ndoa za utotoni.

Mganga wa Zahanti ya Ilobashi Dk. Victor Thomasi (kulia) akichanja Chanjo ya UVIKO-19 kwa wananchi ambao wamehamasika na kupata Chanjo kwenye Kampeni hiyo ya Shirika la WEADO.

Mganga wa Zahanati ya Ilobashi Dk. Victor Thomasi (kulia) akichanja Chanjo ya UVIKO-19 kwa wananchi ambao wamehamasika na kupata Chanjo kwenye Kampeni hiyo ya Shirika la WEADO.

Mganga wa Zahanati ya Ilobashi Dk. Victor Thomasi (kulia) akichanja Chanjo ya UVIKO-19 kwa wananchi ambao wamehamasika na kupata Chanjo kwenye Kampeni hiyo ya Shirika la WEADO.

Hamasa wakitoa burudani kwenye kampeni ya Chanjo ya UVIKO-19, pamoja na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia zikiwamo mimba na ndoa za utotoni katika Kijiji cha Ilobashi Kata ya Masengwa wilayani Shinyanga.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments