SIMBA SC YAONDOKA NA ALAMA TATU MBELE YA VIPERS, YAICHAPA 1-0




NA EMMANUEL MBATILO

KLABU ya Simba imefanikiwa kuondoka na alama tatu ugenini baada ya kufanikiwa kuichapa Vipers ya nchini Uganda 1-0, na kufanikiwa kushika nafasi ya tatu kwenye kundi akiwa amecheza mechi tatu.

Katika mchezo huo muhimu ambao Simba Sc alihitaji kupata ushindi ili aweze kupata matumaini katika kuwania nafasi mbili za juu na kuweza kutinga robo fainali kwenye michuano hiyo ya Klabu Bingwa Afrika inayoendelea.

Simba Sc ilifanikiwa kupata bao la mapema kipindi cha kwanza kupitia kwa beki wao kisiki Inonga Baka na kuiwezesha timu yake kuibuka na ushindi wa bao 1-0.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments