POLISI SHINYANGA WAKAMATA WAGANGA WA RAMLI ZA MAUAJI.. RPC MAGOMI AONYA ASKARI WANAOSHIRIKI KUFANYA UHALIFU


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akionesha vifaa vya uganga vilivyokamatwa wakati akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Februari 27,2023 - Picha na Kadama Malunde

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga limewakamata waganga wa jadi watatu wakiwa na vifaa vinavyotumika katika kupiga ramli chonganishi ambayo husababisha mauaji ya kikatili yakiwemo ya kuua kwa mapanga huku likikemea vikali tabia ya baadhi ya askari polisi wasio waadilifu ambao wanavujisha siri na wanaoshirikiana na wahalifu.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Februari 27,2023 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi amesema vifaa hivyo na watuhumiwa hao wamekamatwa kufuatia misako na doria za jeshi la polisi kwa kipindi cha Februari 5 hadi 27,2023.

“Tumekamata waganga wa jadi wakiwa na vifaa vya kufanyia ramli chonganishi zinazopelekea mauaji ya kikatili yakiwemo mauaji ya mapanga. Pia tumefanikiwa kukamata watuhumiwa watatu wakiwa na vifaa tiba vya hospitali ambavyo haviruhusiwi kumilikiwa na mtu pasipo na idhini ya serikali”,ameeleza Kamanda Magomi.


“Pia tumekamata jumla ya lita 780 za mafuta ya diesel katika maeneo tofauti ya mradi wa Reli ya Kisasa (SGR) pamoja na pikipiki tatu zilizokuwa zinatumika katika uhalifu ikiwemo kubeba mafuta ya wizi katika mradi wa SGR. Hali kadhalika tumeokota pikipiki 2”,amesema.

Amevitaja vitu vingine vilivyokamatwa kuwa ni pamoja na milango 9 ya chuma,mabomba matatu ya chuma,bomba moja la alama za barabarani, milango mitano ya mbao, mzani wa kupimia uzito, mashine ya kutobolea miamba, godoro moja,viti vinne vya plastiki, bangi kete 31, ngoma moja ya shule na magitaa mawili,mashine mbili za kuchezea kamali, subwoofer 2,feni 1,mtungi mmoja wa gesi.

“Jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga linakemea vikali tabia ya baadhi ya askari polisi wasio waadilifu ambao wanavujisha siri na ambao wanashirikiana na wahalifu na kusababisha kudhoofika kwa upatikanaji wa taarifa za kihalifu kutoka kwa wananchi. Hatua kali za kinidhamu zitachukuliwa dhidi yao”, ameongeza Kamanda Magomi
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Februari 27,2023. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Februari 27,2023
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Februari 27,2023.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akionesha vifaa vya uganga vilivyokamatwa na Jeshi la polisi kufuatia misako na doria zilizofanyika
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akionesha vifaa vya uganga vilivyokamatwa na Jeshi la polisi
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akionesha vitu  mbalimbali vilivyokamatwa na Jeshi la polisi Shinyanga
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akionesha vitu  mbalimbali vilivyokamatwa na Jeshi la polisi Shinyanga

Vitu  mbalimbali vilivyokamatwa na Jeshi la polisi Shinyanga.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments