CHRISTINA MNDEME ATEULIWA KUWA MKUU WA MKOA WA SHINYANGA, FRANCIS MICHAEL SONGWE, KINDAMBA TANGA


 Mhe. Christina Mndeme

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi na uhamisho wa wakuu wa mikoa mitatu ya Shinyanga, Tanga na Songwe.


Wakuu wa mikoa wapya walioteuliwa ni Christina Mndeme ambaye anakwenda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga huku aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Francis Michael ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Songwe.

Christina Mndeme anachukua nafasi ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Sophia Mjema, ambae alichaguliwa kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM.

Aidha aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Waziri Kindamba amehamishiwa Mkoa wa Tanga, huku aliyekuwa mkuu wa mkoa huo, Omary Mgumba uteuzi wake ukitenguliwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments