RC NAWANDA AKABIDHI PIKIPIKI KWA MAAFISA UGANI MKOA WA SHINYANGA...."MSITUMIE KWA ANASA, ZIKASAIDIE WAKULIMA"




Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Yahaya Nawanda amekabidhi pikipiki 224 zilizotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maafisa ugani kilimo mkoa wa Shinyanga.

Hafla fupi ya ugawaji wa pikipiki kwa maafisa ugani imefanyika leo Ijumaa Februari 10,2023 katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga na kuhudhuriwa na viongozi na maafisa ugani kutoka wilaya za Kishapu, Shinyanga na Kahama.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Yahaya Nawanda ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu amesema jumla ya pikipiki zilizotolewa mkoa wa Shinyanga ni 224 ambapo Wilaya ya Kahama inapata pikipiki 100, Shinyanga 82 na Kishapu 39.
“Pikipiki hizi ni kutoka kwa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan. Nendeni mkazitunze zidumu ili kufikia malengo ya 10/30 ambapo tunataka kilimo kichangie asilimia 10 ya mapato ya nchi ifikapo mwaka 2030. Msizigeuze za kufanyia anasa wala kufanyia biashara ya bodaboda bali kazitumieni kuleta tija kwa wananchi/wakulima. Tunataka mzitumie kusaidia wananchi na si vinginevyo”,amesema Dkt. Nawanda.

“Pikipiki hizi ni mali ya Serikali, hizi ni fedha za umma na Mhe. Rais Samia ameleta pikipiki hizi ili tuongeze tija katika kilimo, tufanye kilimo biashara. Tunataka tuone tija ya pikipiki hizi, hatuwezi kufikia ajenda ya 10/30 kwa kupiga maneno tu hivyo tunataka vitendo zaidi ili kuwasaidia wakulima”,ameongeza Dkt. Nawanda.

Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini, Mhe. Anord Makombe akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Mhe. Mabala Mlolwa ameipongeza serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa dhamira kubwa inayoonesha katika kuleta mageuzi makubwa kwenye sekta ya kilimo ikiwemo kuongeza bajeti katika sekta ya Kilimo huku akieleza kuwa Serikali itakeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa vitendo.

Kwa upande, Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude na Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Johari Samizi wameahidi kusimamia matumizi yaliyokusudiwa ya pikipiki hizo huku wakiwasisitiza maafisa ugani kuepuka kubadilisha matumizi ya pikipiki hizo.

Nao baadhi ya maafisa ugani wameishukuru serikali kwa kuwapatia vitendea kazi hivyo wakisema vitawasaidia kuwafikia wakulima wengi zaidi ili kuhakikisha kilimo kinakuwa na tija.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Yahaya Nawanda akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi pikipiki 224 kwa maafisa ugani mkoa wa Shinyanga leo Ijumaa Februari 10,2023. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Yahaya Nawanda akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi pikipiki 224 kwa maafisa ugani mkoa wa Shinyanga
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Yahaya Nawanda akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi pikipiki 224 kwa maafisa ugani mkoa wa Shinyanga
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Yahaya Nawanda akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi pikipiki 224 kwa maafisa ugani mkoa wa Shinyanga
Muonekano wa sehemu ya pikipiki 224 zilizotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maafisa ugani mkoa wa Shinyanga.
Muonekano wa sehemu ya pikipiki 224 zilizotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maafisa ugani mkoa wa Shinyanga.
Muonekano wa sehemu ya pikipiki 224 zilizotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maafisa ugani mkoa wa Shinyanga.
Muonekano wa sehemu ya pikipiki 224 zilizotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maafisa ugani mkoa wa Shinyanga.
Muonekano wa sehemu ya pikipiki 224 zilizotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maafisa ugani mkoa wa Shinyanga.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Yahaya Nawanda akikata utepe wakati wa hafla ya kukabidhi pikipiki 224 kwa maafisa ugani mkoa wa Shinyanga
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Yahaya Nawanda akikata utepe wakati wa hafla ya kukabidhi pikipiki 224 kwa maafisa ugani mkoa wa Shinyanga
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Yahaya Nawanda akikata utepe wakati wa hafla ya kukabidhi pikipiki 224 kwa maafisa ugani mkoa wa Shinyanga
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Yahaya Nawanda akimkabidhi Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude (kushoto) pikipiki kwa maafisa ugani wilayani Kishapu
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Yahaya Nawanda akimkabidhi Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Johari Samizi pikipiki kwa maafisa ugani wilayani Shinyanga.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Yahaya Nawanda akifuatiwa na Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude  (katikati) na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mhe. Elias Ramadhan Masumbuko wakijaribishia pikipiki zilizotolewa kwa maafisa ugani
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Yahaya Nawanda (katikati) , Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude  (wa pili kushoto) ,Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mhe. Elias Ramadhan Masumbuko (kushoto), Mwenyekiti wa CCM Shinyanga Mjini, Mhe. Anord Makombe na Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Johari Samizi wakiwa wamepanda kwenye pikipiki zilizotolewa kwa maafisa ugani
Maafisa ugani na wadau wakiwa kwenye hafla ya kukabidhi pikipiki kwa maafisa ugani mkoa wa Shinyanga
Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Prof. Siza Tumbo akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi pikipiki 224 kwa maafisa ugani mkoa wa Shinyanga
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini, Mhe. Anord Makombe akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi pikipiki 224 kwa maafisa ugani mkoa wa Shinyanga
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi pikipiki 224 kwa maafisa ugani mkoa wa Shinyanga
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Johari Samizi akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi pikipiki 224 kwa maafisa ugani mkoa wa Shinyanga 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments