MLOGANZILA YAANZA KUPOKEA WAGONJWA WANAOHITAJI HUDUMA TIBA YA PUTO (INTRAGASTRICK BALLON) KUTOKA NJE


Naibu Mkurugenzi Mtendaji Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila Dkt. Julieth Magandi wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu kambi maalumu ya huduma tiba ya kuweka puto maalum (intragastic ballon) kwenye tumbo la chakula inayoendelea hospitalini hapo ambayo inaendeshwa na wataalamu wazalendo wa MNH-Mloganzila. Mjumbe wa kamati ya kitaifa ya kuratibu utalii tiba (medical tourism), Bw. Abdulmarik Mollel akielezea mipango ya kamati juu ya kutangaza huduma ya puto ndani na nje ya Nchi. 

Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Dkt. Faraja Chinga akieleze namna jopo la wataalamu linavyo shirikiana wakati wa kumuhudumia mtu anayehitaji kuwekewa puto. 

Daktari Bingwa wa Upasuaji na Mtaalamu wa Endoskopia MNH-Mloganzila Dkt. Eric Muhumba akielezea namna mwitikio wa watu wanaokuja kupata huduma kutoka ndani na nje ya nchi ulivyokuwa mkubwa. 

Kaimu Mkuu wa Huduma za Uuguzi na Ukunga Sis. Zuhura Mawona akielezea namna wauguzi walivyojipanga kuwahudumia wagonjwa kwanzia wanapofika hadi wanapomaliza kupatiwa huduma. 

Daktari Bingwa wa Upasuaji na Mtaalamu wa Endoskopia MNH-Mloganzila Dkt. Edwin Muhondezi akizungumza na waandishi wa habari namna zoezi la uwekaji wa puto linavyoendelea. 

Daktari Bingwa wa Upasuaji Mfumo wa Chakula MNH-Mloganzila Dkt. Richard Mliwa akizunguma na waandhishi wa habari kuhusu kambi hiyo. 

Daktari Bingwa wa Usingizi na Ganzi MNH-Mloganzila Dkt. Fillip Muhochi akizungumza na waandishi wa hapari wakati wa uzinduzi wa kambi hiyo. 

*************** 

Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila imeanza kupokea wagonjwa mbalimbali kutoka nje ya nchi, wanaofuata huduma za kibingwa ikiwemo huduma tiba ya kuweka puto kwenye tumbo la chakula ili kusaidia watu wenye uzito mkubwa kupungua. 

Hayo yameelezwa na Naibu Mkurugenzi Mtendaji Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila Dkt. Julieth Magandi wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu kambi maalumu ya huduma tiba ya kuweka puto maalum (intragastic ballon) kwenye tumbo la chakula inayoendelea katika hospitali hiyo ambayo inaendeshwa na wataalamu wazalendo wa MNH-Mloganzila. 

Dkt. Magandi ameeleza kuwa uwekezaji mkubwa uliofanywa na serikali pamoja na maboresho makubwa yaliyofanywa na uongozi wa hospitali ikiwemo uanzishwaji wa huduma za kibingwa umevutia raia wa kigeni kufika Mloganzila kufuata huduma. 

“Tumeanzisha huduma za kibingwa, lakini pia tumeboresha huduma kwa wateja. Kuna dawati la huduma kwa wateja ambalo linafanya kazi saa 24 ili kuhakikisha wateja wetu wanahudumiwa vizuri, jambo hili limevutia raia wa nchi mbalimbali ikiwemo Kenya, Afrika Kusini na Malawi kufuata huduma Mloganzila” ameeleza Dkt. Magandi 

Ameeleza kuwa mteja anapofika Mloganzila anaonwa na jopo la wataalamu kwa pamoja (Multdisplinary approch) ambalo linaundwa na madaktari bingwa wa magonjwa ya ndani, wa usingizi na ganzi, pamoja na wa pasuaji, wataalamu wa maabara na wauguzi ili kupunguza mzunguko na kufanya utaratibu wa matibabu ukamilike ndani ya muda mfupi. 

Dkt. Magandi ametaja huduma za kibingwa ambazo zinapatikana Mloganzila hadi sasa kuwa ni pamoja na kuvunja mawe kwenye figo kwa kutumia mawimbi mshtuko, upasuaji wa kubadilisha nyonga, pamoja na huduma tiba ya kuweka puto kwenye tumbo la chakula ili kusaidia kudhibiti uzito. 

Mjumbe wa kamati ya kitaifa ya kuratibu utalii tiba (medical tourism), Bw. Abdulmarik Mollel ameeleza kuwa kamati imejiridhisha na ubora wa huduma zinazotolewa Mloganzila na kwamba tayari imeanza kutengeneza utaratibu wa kutangaza fursa hiyo ya matibabu nje ya nchi. 

Naye Daktari Bingwa wa Upasuaji na Mtaalamu wa Endoskopia MNH-Mloganzila Dkt. Eric Muhumba amesema kuwa toka huduma hiyo ianzishwe mwezi uliopita tayari wagonjwa 20 wamenufaika na kwamba hadi mwisho wa kambi wanategemea idadi itafikia watu 30. 

Ameeleza kuwa huduma tiba ya kuweka puto maalumu kwenye tumbo la chakula kwa watu wenye uzito uliopitiliza (intragastic ballon) inasaidia kupunguza nafasi kwenye tumbo la chakula hivyo kusababisha mtu kula kidogo jambo ambalo litapelekea kupungua uzito.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments