WANAFUNZI WAFARIKI BAADA YA MASHUA KUZAMA


Wanafunzi watatu kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya wamefariki dunia baada ya mashua waliyokuwa wameabiri kuzama eneo la Budalangi, kaunti ya Busia.

Wanafunzi hao watatu walikuwa sehemu ya kundi cha wanafunzi saba ambao walikuwa wamekwenda kufurahia safari ya mashua kabla ya mambo kwenda mrama. 

Kwa mujibu wa ripoti ya runinga ya Citizen, kamanda wa polisi wa kaunti ndogo ya Bunyala Isaiah Mose alisema wanafunzi wanne kati ya saba wameokolewa huku miili mitatu ya ikiwa bado haijaopolewa.

Shughuli za kutafuta mabaki yao zilisitishwa baada ya giza kuingia Jumamosi, Disemba 1, na zinatarajiwa kurejea leo .

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments