YANGA YAJICHIMBIA KILELENI, YAICHAPA SINGIDA BIG STAR 4-1


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Yanga Sc wamerejea kileleni kwa kuiadhibu Singida Big Star kwa mabao 4-1 kwenye ligi kuu Tanzania Bara, mchezo ambao ulipigwa kwenye dimba la Benjamin Mkapa jijini dar es Salaam,

Stori kubwa kwenye mchezo huo ni Fiston Kalala Mayele ambaye amefunga mabao matatu, Hat trick baada ya kukaa muda mrefu bila kufakamia nyavu kwenye ligi kuu inayoendelea huku goli lingine likifungwa na Kibwana Shomari.

Singida Big Star bao lao pekee lilifungwa na Meddie Kagere ambaye nae amekaa muda mrefu bila kufunga huku kwenye ligi kifikisha mabao mawili tu na kwa upande wa Fisto Mayele akifikisha mabao sita ndani ya ligi msimu huu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments