TAASISI YA DORIS MOLLEL YAZINDUA RASMI SIKU YA MTOTO NJITI


********************

Taasisi ya Doris Mollel (Mollel Foundation) leo imezindua rasmi Maadhimisho ya Mtoto Njiti Duniani ambayo yanatarajiwa kufikia kilele chake Novemba 20, 2022 ambayo yatafanyika katika Viwanja vya Robanda vilivyopo katika Wilaya ya Serengeti mkoani Mara.

Katika uzinduzi huo uliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Sea Shell, Kijitonyama jijini Dar, ulihudhuriwa na balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Dkt. Mehmet Gulluoglu.

Siku hiyo ya kilele, taasisi hiyo itakabidhi vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi 180,190,000 ambavyo vitakwenda katika Hospitali za Wilaya za Serengeti, Ukerewe, Kwimba na Magu pamoja na ufungaji wa mitambo ya hewa ya Oxygen kwa watoto wachanga.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments