MWANAUME ALIYEJIFANYA 'HOUSE GIRL' AKAMATWA AKIJARIBU KUMDHULUMU KIMAPENZI MTOTO WA KIUME WA BOSI WAKE

Mwanaume aliyejifanya mwanamke nchini Zambia ili kuajiriwa kama mjakazi 'House Girl' amekamatwa kwa kujaribu kumdhulumu kimapenzi mvulana wa miaka 19.

Christopher Mukutindwa, 29, ambaye anatoka Mtendere alijaribu kujilazimisha kwa mpwa wa mwajiri wake baada ya kufanya kazi nyumbani kwao kwa miezi mitano.


Mwebantu aliripoti Mukutindwa alimvuta mwathiriwa wake chumbani kwake na kujaribu kujilazimisha kwake lakini alizidiwa nguvu na kijana huyo ambaye alikimbia kuokoa maisha yake na kuripoti kisa hicho kwa polisi. 

“Ukweli kwa ufupi Mukutindwa alimuita mwathiriwa chumbani kwake, akavua kitenge alichokuwa amevaa ili afanye mapenzi naye.

 Hapo ndipo mwathiriwa alipogundua kuwa mjakazi huyo alikuwa ni mwanaume na kuanza kumenyana naye akafanikiwa kumzidi nguvu,” alisema msemaji wa Polisi Rae Hamoonga mnamo Alhamisi, Novemba 3, 2022.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments