MWENDESHA BODABODA AUAWA KWA KUPIGWA RISASI NA MAJAMBAZI GEITA

Kijana Amin Salum Mkazi wa Mtaa wa Nyamarembo Wilaya ya Geita Mkoani Geita Ambaye ni Dereva wa Pikipiki Maarufu Kama Bodaboda amefariki dunia kwa kupigwa risasi na watu wanaozaniwa kuwa majambazi nyakati za usiku.


Salum Alipigwa risasi wakati akiendelea na Majukumu yake ya kutoa huduma ya usafiri wakati wa usiku ndipo tukio hilo la kupigwa risasi eneo la Nyamarembo lilitokea kwa kupigwa Risasi hadi kufariki dunia.


Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita Safia Jongo amesema Amin Salum dereva Bodaboda alipigwa risasi na majambazi ambao walitaka kufanya uporaji kwa Mfanya Biashara ambaye jina lake limehifadhiwa nyakati za usiku na ndipo majambazi hao walipokimbia na kumfyatulia risasi Dereva huyo.


Kamanda Safia Amesema kufuatia tukio hilo jeshi la polisi litaendesha msako wa kuwasaka majambazi hao ambao wametekeleza tukio la mauaji la kijana Amin Salum na watakapo kamatwa watafikishwa katika mamlaka husika na kushugulikiwa kwa mjibu wa sheria.

https://www.instagram.com/p/CkdgnY0NQHH/?igshid=MDJmNzVkMjY=

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments