YANGA SC YAENDELEA KUWEKA REKODI LIGI YA NBC, YAICHAPA RUVU SHOOTING 2-1



*******************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

KLABU ya Yanga imeendelea kutoa matokeo mazuri kwenye ligi ya NBC baada ya leo kuibuka mshindi wa 2-1 na kujinyakulia pointi tatu dhidi ya Ruvu Shooting, mechi ambayo imepigwa kwenye dimba la Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.

Ruvu Shooting walicheza kandanda murua kwenye mchezo huo katika kipindi cha kwanza licha ya kutengeneza nafasi kadhaa na kushindwa kuzitumia vizuri na kufanya matokeo kuwa 0-0 kipindi cha kwanza.

Kipindi cha pili Yanga iliingia ikiwa imeimarika kwani walibadika kwa kiasi kikubwa na kufanikiwa kupata bao la kwanza kupitia kwa Feisal Salum ambaye alipata bao akipokea krosi nzuri kutoka kwa Joyce Lomalisa.

Bao la pili la Yanga Sc liliwekwa kimyani na nahodha wao Bakari Mwamnyeto ambaye ni goli lake la pili kwa msimu huu 2022/2023.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments