MOSES PHIRI AENDELEZA MAKALI YAKE, SIMBA YAICHAPA 3-0 DODOMA JIJI



******************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

KLABU ya Simba imeendelea kutoa dozi kwenye Ligi Kuu Tanzania NBC baada ya leo kuichapa Dodoma Jiji Fc kwa mabao 3-0, mchezo ambao ulipigwa katika dimba la Benjamini Mkapa.

Simba Sc imecheza mchezo huo siku chache baada ya kutoka visiwani Zanzibar kwaajili ya kujiweka sawa kwa michezo ya ligi kuu bara pamoja na ligi ya mabingwa Afrika ambayo michuano hiyo inaendelea wiki ijayo.

Simba imepata mabao yake kupitia kwa mshambuliaji wake Moses Phiri, Habibu Kyombo pamoja na bao lingine Dodoma Jiji wakijifunga wakijaribu kuokoa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post