KIONGOZI WA UVCCM ATIWA NGEU KWA JAGI NA KIONGOZI WA UMOJA WA WANAWAKE CCM 'UWT' WIVU WA MAPENZI KWA MAMA LISHE




Ni mshangao, ndivyo unavyoweza kueleza mkasa uliompata mmoja wa viongozi wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) wilayani Chemba Mkoa wa Dodoma, kupigwa na kitu chenye ncha kali kichwani na kiongozi wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) katika mgogoro unaodaiwa kuwa wa mapenzi.

Tangu juzi zilisambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) wa wilaya kupasuliwa ngeu na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake (UWT) wa wilaya hiyo.

Taarifa hiyo, imesema kuwa kiongozi wa kiongozi huyo wa UWT kumfuata kiongozi mwenzake katika kibanda cha Mama lishe na kisha kumpiga kwa kutumia jagi la kioo ambalo lilimpasua sehemu kubwa ya kichwa.


Taarifa zinaeleza kuwa alipokwenda Kiula ni mgahawa wa mwanamke mmoja ambaye amekuwa akitiliwa shaka na kiongozi huyo wa UWT anayedaiw akuwa na uhusiano naye kimapenzi.

Taarifa hizo zinasema kuwa, kiongozi huyo wa UVCCM alifuatwa na kabla ya kupigwa ngeu, aliulizwa ni kwa nini alikwenda mahali ambapo amekuwa akizuiwa kutofika.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments