ASKARI POLISI AVAMIA SHULE NA KUMCHOMA KISU MHASIBU AKITAKA ARUDISHIWE ADA


Afisa wa polisi wa Kitui nchini Kenya ametiwa mbaroni baada ya kuvamia shule ya upili ya wasichana huko Mwingi na kumdunga kisu mhasibu.


Karao huyo, Haji Boru, anasemekana kufika kwa hasira katika Shule ya Sekondari ya Wavulana ya Mwingi, akitaka kurejeshewa karo ya ziada zinazolipwa kupitia Hazina ya Maendeleo ya Maeneo Bunge.

Katika ripoti ya Citizen TV, mhasibu aliyeathiriwa ilieleza kuwa pesa hazingeweza kurejeshwa lakini zingeweza kuhamishwa kwa karo ya chuo kikuu cha mwanawe, lakini afisa aliyeshtakiwa hakutaka kusikia hilo.

Mara moja alichomoa kisu na kumdunga mhasibu huyo aliyetambulika kwa jina la Alex Mwanzia.

OCPD wa Mwingi ya Kati Peter Mutuma alithibitisha kisa hicho akisema mshukiwa alikuwa amewekwa korokoroni na sasa anasubiri kufikishwa mahakamani.

 Mhasibu huyo kwa sasa amelazwa hospitalini kupokea matibabu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments