WAFUGAJI WALIOHAMIA MSOMERA WAUNGA MKONO JUHUDI ZA UHIFADHI




Na Abel Paul wa Jeshi la Polisi

Wafugaji wa Jamii ya kimasaii waliohamia katika kijiji cha Msomera Wilaya ya Handeni Mkoa wa Tanga wamesema wameamua kwa hiari yao wenyewe kuhamia Msomera kuunga Juhudi za uhifadhi zinazofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Wafugaji hao ambao wamehamia eneo hilo wakitoka katika mamlaka ya hifadhi Ngorongoro wamesema watalitumia eneo hilo kwa kwa shughuli za ufugaji na kilimo tofauti na mwanzo walipokuwa katika mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro ambapo fulsa hiyo hawakuipata.

Hayo wamesema leo Oktoba 09 katika kijiji cha Msomera  baadhi ya wafugaji Wa Jamii ya kimasaii mara baada ya kuwasili kwa kundi la kumi na mbili katika Kijiji cha Msomera Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga, wafugaji hao wamesema wanamuunga Mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Jitihada zake za kukuza ufadhi na utalii alizoanza kujionyesha katika Nchi yetu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments