MWALIMU WA ZAMU ATANDIKWA KOFI NA MWANAFUNZI WAKE HADI DAMU KUTOKA




Mwanafunzi wa darasa la 8 katika Shule ya Msingi ya Nkararo huko Transmara, Kaunti ya Narok, yuko mbioni baada ya kumpiga mwalimu wa zamu kofi alipotaka kuona kazi yake ya ziada.

Inasemekana mwalimu huyo anayefahamika kama Charles Miruka alitokwa na damu na kupoteza miwani yake.

Katibu wa Chama cha Kitaifa cha Walimu nchini (KNUT) Collins Oyuu alikashifu kisa hicho na kuwataka polisi kumtafuta na kumkamata mwanafunzi huyo.

Mwalimu huyo alikimbizwa hospitalini eneo hilo ambako alitibiwa na kuruhusiwa kwenda nyumbani huku mwanafunzi huyo akitoroka na bado hajapatikana.

Katibu huyo wa KNUT alitoa wito wa kukamatwa mara moja kwa mshukiwa anayedaiwa kuwa na umri wa zaidi ya miaka 18.

"Tunatoa wito kwa polisi kumkamata mara moja mtuhumiwa. Kwa nini mwalimu anapokosewa hakuna anayechukulia suala hilo kwa uzito? Tunaiomba serikali kuwapa ulinzi wa hali ya juu walimu wote nchini" alisema Bw. Korir.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments