JESHI LA POLISI LAMKAMATA MWANAMKE ALIYEMFANYIA UKATILI MTOTO WAKE


JESHI la Polisi nchini Uganda, linamshikilia Dorothy Nabulime (22) mkazi wa mji mdogo wa Busula, nje kidogo ya jiji la Kampala kwa tuhuma za kumpiga na kumfanyia ukatili mwanae wa kike mwenye umri wa miaka miwili.

Dorothy mama wa watoto watatu alirekodiwa video akimpiga mwanae huyo bila huruma na kumuangusha kwenye beseni alilokua anaogea.
Mwanae mkubwa ana miaka 5 ambaye alimzaa akiwa na miaka 17. Wa pili ana umri wa mitatu na wa mwisho ana miaka miwili ambaye ndiye aliyerekodiwa akimpiga. Dorothy ni “single mother” ambaye anadaiwa kupitia unyanyasaji wa kijinsia katika malezi yake, na anawalea watoto wote watatu peke yake kwa biashara ndogondogo.

Amefunguliwa kesi ya shambulio la kudhuru mwili (assault causing bodily harm) na unyanyasaji wa mtoto (child abuse) na anatarajiwa kupandishwa kizimbani kesho, jumatatu kujibu tuhuma zinazomkabili. Kwa sasa anashikiliwa kituo cha polisi Luwero, huko Busula na amefunguliwa kesi nambari SD/RF/06/03/09/2022.

Ikiwa atapatikana na hatia anaweza kufungwa kati ya miaka miwili hadi mitano Gerezani.!

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments