RC MJEMA AONGOZA KIKAO CHA TATHMINI UTEKELEZAJI MKATABA WA LISHE, CHANJO YA UVIKO -19 NA POLIO SHINYANGA...AGEUKA MBOGO UPATIKANAJI TAKWIMU

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Sophia Mjema akizungumza wakati akifungua kikao cha Tathmini ya  Utekelezaji wa Mktaba wa Lishe kwa kipindi cha 2021/2022 na Kampeni ya Polio kwa awamu ya tatu kwa watoto chini ya miaka mitano. 

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Sophia Mjema ameziagiza Halmashauri za wilaya katika mkoa huo zitoe shilingi 1000 kwa kila mtoto aliye chini ya miaka mitano kila mwezi na kufanya vikao vya tathmini ya lishe ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Mkataba wa Lishe.


Mjema ametoa agizo hilo leo Ijumaa Septemba 2,2022 wakati wa Kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mktaba wa Lishe kwa kipindi cha 2021/2022 na Kampeni ya Polio kwa awamu ya tatu kwa watoto chini ya miaka mitano iliyoanza Septemba 1,2022.

Mjema amesema kikao hicho cha tathmini ni fursa ya kujipima na kuchukua hatua kwa kila halmashauri kubaini changamoto zinazokwamisha ili wazifanyie kazi na kuondokana na hali isiyoridhisha ya utekelezaji wa afua za lishe.

“Tukumbuke kuwa Lishe bora na Chanjo ya Polio ni msingi wa maendeleo ya taifa letu, nawatakia Utekelezaji mwema wa Kampeni ya Polio na shughuli za lishe ili kufikia lengo la uchanjaji na utekelezaji wa mkataba wa lishe”,amesema Mjema.


“Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan inaendelea na utekelezaji wa mkataba wa Lishe kupitia Mikoa, Halmashauri, kata na Vijiji/mitaa tangu mwaka 2018, utekelezaji huu wa mkataba wa Lishe umewezesha kuboresha utoaji wa huduma za lishe kwa wananchi”, ameongeza.

Amesema lengo la Mkataba wa Lishe ni kusimamia utekelezaji wa maelekezo ya serikali ya kutenga na kutumia shilingi 1000 kwa kila mtoto mwenye umri chini ya miaka mitano kwa ajili ya kutekeleza afua za lishe ngazi ya halmashauri.

“Katika utekelezaji wa Mkataba wa Lishe ngazi ya halmashauri kwa kipindi cha Julai 2021 hadi Juni 2022, mkoa wa Shinyanga umetoa fedha kwa asilimia 76.56 ambapo Manispaa ya Shinyanga imeongoza kwa utoaji wa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa afua za lishe kwa kutoa fedha kwa asilimia 100”,amefafanua.


Mkuu huyo wa Mkoa amewapongeza Wakuu wa Wilaya na viongozi wengine kwa kusimamia mkataba wa lishe na kufanya vikao vya tathmini kila baada ya miezi mitatu kama mwongozo unavyoelekeza.

Akizungumzia kuhusu Kampeni ya Chanjo ya Polio kwa awamu ya tatu iliyoanza Septemba 1,2022 , Mjema amesema Kampeni hiyo itafanyika hadi Septemba nyumba kwa nyumba ambapo walengwa kimkoa ni 445,681 walio chini ya miaka mitano.

Amesema Chanjo zinazotolewa na Serikali ni salama na zimedhibitishwa na Wizara ya Afya pamoja na Shirika la Afya Duniani (WHO) hivyo kuwaomba wadau wa afya kukanusha upotoshaji wowote unaoweza kujitokeza katika jamii kuhusu kampeni za chanjo pamoja na kuhamasisha wananchi kupata chanjo na kusimamia shughuli zote za utekelezaji wa kampeni za chanjo.


“Kwenye eneo la utoaji wa Chanjo za UVIKO 19, Mkoa unaendelea na utoaji wa chanjo hizo. Walengwa wa chanjo za UVIKO -19 ni watu walio chini ya umri wa kuanzia miaka 18 na kuendelea ambao kimkoa ni 1,011,085 na hadi kufikia Agosti 31,2022 wateja wapatao 735,844 wamepata kinga kamili dhidi ya ugonjwa wa UVIKO – 19 ambao ni sawa na asilimia 73 na kufanya mkoa wetu kushika nafasi ya tano kitaifa”, ameeleza Mjema.


“Kwa upande wa dirisha la dawa kwa wazee, tuhakikishe wazee wanapata dawa, malalamiko yapungue, wazee wapate dawa”,amesema.

Mjema pia ameziagiza halmashauri za wilaya kuhakikisha zinatoa takwimu kwa wakati

“Nimeona kuna tatizo kubwa la Takwimu kwenye Halmashauri zetu, hili donda ndugu nataka liondoke, kwenye kutoa taarifa naona kuna tatizo,unakuta kazi imefanywa vizuri sana lakini changamoto inakuja kwenye takwimu”,amesema

“Mimi sitaki kuona tena tatizo la takwimu, takwimu zikihitajika nataka tuzipate haraka, hili tatizo la taarifa sitaki kulisikia, zikitakiwa mkoani lazima tuzipate, hii iwe mwisho. Haiwezekani Mkuu wa mkoa, mkuu wa wilaya , kamati ya usalama inahangaika kutafuta takwimu…. Wafichueni wanaokwamisha, ukijiona wewe ni Slow Learner tuambie tukusaidie.

“Nataka takwimu ziwe zinakuja kwa wakati na zinaenda kwa wakati, hatuhitaji kugombana kuhusu takwimu, Mhe, RAS Ondoa mtu anayekwamisha, hatutaki kurudishwa nyuma” ,amesema Mjema.

“Siyo kazi ya Mkuu wa Mkoa, Kamati ya Usalama, Mkuu wa Wilaya kwenda kuhangaika kutafuta takwimu.. Unapochelewesha takwimu unakwamisha mambo, RAS niondolee watu wanaokwamisha upatikanaji wa takwimu. Tunataka kila mmoja afanye kazi, hatutawavumilia wanaoturudisha nyuma, ni lazima tumsaidie Mhe. Rais Samia Suluhu ambaye anafanya jitihada kubwa za kuleta fedha kwa ajili ya maendeleo”,ameongeza Mjema

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Sophia Mjema akizungumza leo Ijumaa Septemba 2,2022 wakati akifungua kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mktaba wa Lishe kwa kipindi cha 2021/2022, Chanjo ya UVIKO - 19 na Kampeni ya Polio kwa awamu ya tatu kwa watoto chini ya miaka mitano. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Sophia Mjema akizungumza leo Ijumaa Septemba 2,2022 wakati akifungua kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mktaba wa Lishe kwa kipindi cha 2021/2022, Chanjo ya UVIKO - 19 na Kampeni ya Polio kwa awamu ya tatu kwa watoto chini ya miaka mitano.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Sophia Mjema akizungumza leo Ijumaa Septemba 2,2022 wakati akifungua kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mktaba wa Lishe kwa kipindi cha 2021/2022, Chanjo ya UVIKO - 19 na Kampeni ya Polio kwa awamu ya tatu kwa watoto chini ya miaka mitano.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Sophia Mjema akizungumza leo Ijumaa Septemba 2,2022 wakati akifungua kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mktaba wa Lishe kwa kipindi cha 2021/2022, Chanjo ya UVIKO - 19 na Kampeni ya Polio kwa awamu ya tatu kwa watoto chini ya miaka mitano.

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akizungumza kwenye kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mktaba wa Lishe kwa kipindi cha 2021/2022, Chanjo ya UVIKO - 19 na Kampeni ya Polio kwa awamu ya tatu kwa watoto chini ya miaka mitano.

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akizungumza kwenye kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mktaba wa Lishe kwa kipindi cha 2021/2022, Chanjo ya UVIKO - 19 na Kampeni ya Polio kwa awamu ya tatu kwa watoto chini ya miaka mitano.

Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Festo Kiswaga akizungumza kwenye kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mktaba wa Lishe kwa kipindi cha 2021/2022, Chanjo ya UVIKO - 19 na Kampeni ya Polio kwa awamu ya tatu kwa watoto chini ya miaka mitano.


Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Sophia Mjema akiongoza kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mktaba wa Lishe kwa kipindi cha 2021/2022, Chanjo ya UVIKO - 19 na Kampeni ya Polio kwa awamu ya tatu kwa watoto chini ya miaka mitano.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Yudas Ndungile akizungumza kwenye kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mktaba wa Lishe kwa kipindi cha 2021/2022, Chanjo ya UVIKO - 19 na Kampeni ya Polio kwa awamu ya tatu kwa watoto chini ya miaka mitano.

Wadau wa afya wakiwa kwenye kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mktaba wa Lishe kwa kipindi cha 2021/2022, Chanjo ya UVIKO - 19 na Kampeni ya Polio kwa awamu ya tatu kwa watoto chini ya miaka mitano.

Wadau wa afya wakiwa kwenye kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mktaba wa Lishe kwa kipindi cha 2021/2022, Chanjo ya UVIKO - 19 na Kampeni ya Polio kwa awamu ya tatu kwa watoto chini ya miaka mitano.

Wadau wa afya wakiwa kwenye kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mktaba wa Lishe kwa kipindi cha 2021/2022, Chanjo ya UVIKO - 19 na Kampeni ya Polio kwa awamu ya tatu kwa watoto chini ya miaka mitano.

Wadau wa afya wakiwa kwenye kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mktaba wa Lishe kwa kipindi cha 2021/2022, Chanjo ya UVIKO - 19 na Kampeni ya Polio kwa awamu ya tatu kwa watoto chini ya miaka mitano.

Wadau wa afya wakiwa kwenye kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mktaba wa Lishe kwa kipindi cha 2021/2022, Chanjo ya UVIKO - 19 na Kampeni ya Polio kwa awamu ya tatu kwa watoto chini ya miaka mitano.




Wadau wa afya wakiwa kwenye kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mktaba wa Lishe kwa kipindi cha 2021/2022, Chanjo ya UVIKO - 19 na Kampeni ya Polio kwa awamu ya tatu kwa watoto chini ya miaka mitano.


Wadau wa afya wakiwa kwenye kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mktaba wa Lishe kwa kipindi cha 2021/2022, Chanjo ya UVIKO - 19 na Kampeni ya Polio kwa awamu ya tatu kwa watoto chini ya miaka mitano.

Wadau wa afya wakiwa kwenye kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mktaba wa Lishe kwa kipindi cha 2021/2022, Chanjo ya UVIKO - 19 na Kampeni ya Polio kwa awamu ya tatu kwa watoto chini ya miaka mitano.

Wadau wa afya wakiwa kwenye kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mktaba wa Lishe kwa kipindi cha 2021/2022, Chanjo ya UVIKO - 19 na Kampeni ya Polio kwa awamu ya tatu kwa watoto chini ya miaka mitano.

Wadau wa afya wakiwa kwenye kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mktaba wa Lishe kwa kipindi cha 2021/2022, Chanjo ya UVIKO - 19 na Kampeni ya Polio kwa awamu ya tatu kwa watoto chini ya miaka mitano.

Wadau wa afya wakiwa kwenye kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mktaba wa Lishe kwa kipindi cha 2021/2022, Chanjo ya UVIKO - 19 na Kampeni ya Polio kwa awamu ya tatu kwa watoto chini ya miaka mitano.

Wadau wa afya wakiwa kwenye kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mktaba wa Lishe kwa kipindi cha 2021/2022, Chanjo ya UVIKO - 19 na Kampeni ya Polio kwa awamu ya tatu kwa watoto chini ya miaka mitano.

Wadau wa afya wakiwa kwenye kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mktaba wa Lishe kwa kipindi cha 2021/2022, Chanjo ya UVIKO - 19 na Kampeni ya Polio kwa awamu ya tatu kwa watoto chini ya miaka mitano.


Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments