PAPA FRANCIS ATEUA MAKARDINALI 20 WATAKAOSHIRIKI KUTEUA MRITHI WA KITI CHAKE


Papa Francis akiwatawaza Maaskofu kuwa Makardinali
Papa Francis akiwa katika kanisa la St.Peter’s

BABA Mtakatifu na mkuu wa kanisa katoliki duniani Papa Francis (85) amewateua maaskofu 20 na kuwatawaza kuwa makardinali watakaoongezeka kwenye jopo litakaloshiriki kumteua mrithi wa kiti chake.


Papa Francis katika uteuzi wake huo alijaribu kuwapa kipaumbele makardinali wa jamii zilizotengwa zaidi.

 Mmoja wa waliochaguliwa ni Askofu Hyderabad Anthony Poola kutoka nchini India mwingine ni Askofu Peter Ebere Okapaleke kutoka Nigeria.

Hafla hiyo ya kuwatawaza Maaskofu hao ilifanyika katika kanisa la St.Peters huko Vatican. Katika waliotawazwa 16 kati yao wana umri chini ya miaka 80.


Imeandikwa:Dunstan Mtili Erick kwa msaada wa mitandao

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments