TARI YAALIKA OFISI ZA HALMASHAURI KUPELEKA MAAFISA UGANI KUPIGWA MSASA


Mfano wa kifaa cha kupimia afya ya udongo
**
Na Mwandishi wetu - Mwanza
Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) Ukiriguru imewataka Maafisa Ugani kutoka kwenye Halmashauri za wilaya kwenda kupigwa msasa kwenye kituo hicho jinsi ya kutumia vifaa vya kupimia udongo (Soil Test Kit) walizopewa kwa ajili ya kupima afya ya udongo kwenye maeneo yao.


Akizungumza kwenye maonesho ya Nane Nane yanayoendelea katika viwanja vya Nyamhongolo jijini Mwanza ,Mtafiti kutoka Idara ya Udongo TARI Ukiriguru, Hainess Msuya amesema endapo maafisa ugani hawatapata mafunzo Soil Test Kit hiyo haitaleta matokeo yanayotarajiwa.

“Maafisa ugani waje wapewe semina ya jinsi ya kutafsiri taarifa zinazopatikana baada ya kupima udongo kuna uhakika wengi wao itakuwa vigumu kutafsiri taarifa hizo kutokana na ukweli kwamba wengi wametoka Chuo siku nyingi na wengine hawajawahi hata kukutana na hizo Soil Test Kit",amesema Mtafiti huyo.

Mtafiti huyo alisema tunapima udongo ili kujua afya ya udongo na vipimo hivyo ndiyo vitatusaidia kwenye eneo husika ni nini tunahitaji kupanda na ni mbolea gani tuweke kwenye udongo huo

“Vifaa ni vizuri nashauri Halmashauri ziwapeleke maafisa ugani kwenye vituo vya TARI wapewe mafunzo ya muda mfupi. Huku Kanda ya Ziwa Magharibi waje Ukiriguru na wa Kanda zingine waende kwenye vituo vya TARI vilivyopo kwenye maeneo yao ili wawahi msimu wa mvua huu kabla ya kilimo kuanza”,amesema

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments