VIJANA WAMCHAPA MAKOFI MBUNGE WAO KISHA KUMWAGIA MAJI AHADI FEKI


Vijana wenye hasira nchini Ghana katika eneo la Suame, wamempiga makofi, kumtukana pamoja na kummwagia maji mbunge wao, Osei Kyei Mensah-Bonsu, kwa kile walichokieleza kwamba licha ya kuwawakilisha bungeni, lakini hatimizi ahadi zake za kurekebisha miundombinu ya barabara.

Osei Kyei Mensah-Bonsu ni mbunge wa chama cha New Patriotic Party (NPP), alikuwa katika eneo hilo kuzungumza na wananchi juu ya mahitaji yao ikiwa ni pamoja na miundombinu duni.

Mbunge huyo amesema kuwa hana wasiwasi kuhusu tukio hilo kwa sababu vijana wangefanya vivyo hivyo kwa afisa yeyote wa serikali, na sio yeye pekee.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments