TIGO NA XIAOMI WAZINDUA REDMI NOTE 11 KATIKA MAONESHO YA SABASABA

Meneja wa mauzo wa vifaa vya intaneti wa Tigo Edwin Mgoa akiongea na waandishi (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa kutambulisha sim mpya aina ya Redmi Note 11 katika viwanja vya sabasaba ikiwa na Ofa ya Intaneti ya GB 96 kwa mwaka,pembeni yake ni Meneja mauzo wa xiaomi Alex katagira akionesha simu. Leo tarehe 6 Julai 2021 , Kampuni namba moja ya huduma za Kidigitali hapa nchini Tigo pamoja na Kampuni ya Simu za mkononi Infinix wametambulisha simu mpya ya 4G aina ya Infinix HOT 10i.

Akizungumza wakati wa kutambulisha simu hiyo Meneja wa vifaa vya intaneti kutoka kampuni ya Tigo Bwana Edwin Mgoa amesema simu iyo itapatikana kwenye maduka ya Tigo na Infinix Nchi Nzimahuku ikiwa na Ofa ya Intaneti ya GB 96 kwa mwaka, na kusisitiza juu ya dhamira ya Kampuni ya Tigo kuleta simu hizi nzuri na za kisasa ni kuhakikisha wateja wake wanakwenda kwenye mawasiliano ya Kidigital na kutimiza dhamira ya serikali ya kuhakikisha kwamba kufikia mnamo 2025 asilimia 80 ya vifaa vya mawasiliano vinakidhi TEHAMA kwa mfumo wa Kiserikali. Kwa upande mwingine Meneja Mauzo wa Xiaomi Alex katagira amewapongeza Tigo kwa kuendelea kuwa nao bega kwa bega, "Redmi note 11 ni simu ambayo ni rafiki kuanzia bei yake hadi utumiaji , lakini pia simu hii ina kamera tatu (Main Camera ikiwa na Mega Pixels 50 na flash nne, huku camera ya mbele ikiwa na Mega pixels 8 na flash) zitakazomfanya mtumiaji kupiga picha nzuri wakati na mahala popote, lakini pia ina storage kubwa Ya 128 GB na RAM GB 8, Vile vile inauwezo wa kukaa na chaji kwa muda mrefu sana hata kwa zaidi ya siku 2, huku ikiwa na processor bora itayomwezesha mtumiaji kucheza game na kufanya vitu vingi kwa wakati mmoja maana pia ina kioo kikubwa cha 6.52, nawashauri Watanzania hasa katika msimu huu wa sabasaba watembelee banda la Tigo XIAOMI tupo hapa kuwahudumia" Alisema Katagira .

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments