TAZAMA HAPA MAJINA WALIOITWA KAZINI AJIRA ZA KADA YA AFYA


Wizara ya Afya imetoa orodha ya watumishi walioitwa kazini kufuatia waombaji wa ajira za kada za afya zilizotangazwa kwenye tovuti ya wizara ajira.moh.go.tz tarehe 16 Aprili, 2022 hadi tarehe 03 Mei, 2022.

Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Juni 30, 2022 na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya,Prof. Abel N. Makubi ambapo amefafanua kuwa, hatua hiyo imefikiwa baada ya zoezi la uchambuzi wa maombi ya kazi yaliyopokelewa kukamilika.

BOFYA <<HAPA>> KUTAZAMA 


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA AFYA 

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MATOKEO YA MAOMBI YA AJIRA MPYA ZA  KADA ZA AFYA ZILIZO CHINI YA USIMAMIZI WA  

MOJA KWA MOJA WA WIZARA YA AFYA  

Dodoma, Alhamisi Juni 30, 2022.  

Mnamo Mwezi Aprili, 2022 Wizara ya Afya, ilipata kibali cha kuajiri jumla ya nafasi 1,650 za Wataalamu wa kada mbalimbali ambao wataajiriwa na kupangiwa vituo vya kazi  ambavyo vipo chini ya usimamizi wa moja kwa moja wa Wizara ya Afya. Huu ni  utekelezaji wa ahadi iliyotolewa na Serikali ya Awamu ya Sita (6) inayoongozwa na  Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 

Kibali cha nafasi hizo za ajira 1,650 kutoka Ofisi ya Rais – UTUMISHI kilitoa fursa kwa  wataalamu wa kada mbalimbali katika vituo vilivyo chini ya usimamizi wa moja kwa moja  wa Wizara ya Afya. Kati ya nafasi hizo, nafasi 29 ambazo hazihusiani na afya moja kwa  moja zitatangazwa na Sekretariati ya Ajira na hivyo kubaki nafasi 1,621 chini ya Wizara  ya Afya pekee.  

Kada za afya ambazo zitanufaika na nafasi hizi ni; Madaktari, Wafamasia, Wateknolojia  wa Dawa, Wateknolojia wa Maabara, Wateknolojia wa Mionzi, Wateknolojia wa Macho,  Maafisa Uuguzi, Watoa Tiba kwa Vitendo, Wazoeza Viungo kwa Vitendo, Maafisa Afya  Mazingira pamoja na Wasaidizi wa Afya. 

Baada ya kupokea kibali hicho, Wizara ilitangaza nafasi 1,621 za kada ya afya kupitia  tovuti ya Wizara ya ajira.moh.go.tz kuanzia tarehe 16-29 Aprili, 2022. Hata hiyokutokana na umuhimu wa zoezi hili Wizara iliongeza muda hadi tarehe 03 Mei, 2022  ambapo ilikuwa ndiyo siku ya kufungwa kwa mfumo. Mpaka tangazo lilipofungwa jumla  

Ukurasa wa 1 kati ya

ya waombaji 19,464 ndiyo walikamilisha taratibu za uombaji kwenye mfumo na waombaji 8,404 hawakukamilisha taratibu za uombaji.Kati ya waombaji 19,464 waliofanyiwa  uchambuzi, waombaji 7,897 walikidhi vigezo vya awali kama ilivyoorodheshwa hapa chini: 

i. Kuzingatia Miundo ya Utumishi kwa kada za Afya (Alama 3). 

ii. Waombaji waliohitimu masomo yao kuanzia Mwaka 2020 kurudi nyuma isipokuwa  Madaktari Bingwa, Wahandisi Vifaa Tiba, Fundi Sanifu Vifaa Tiba, Watekinolojia  na Walemavu (Alama 2.5). 

iii. Waombaji wenye ulemavu (Alama 1.5) 

iv. Watumishi walioajiriwa kwa mkataba na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali  wanaofanya kazi kwa makubaliano ya kuajiriwa kupitia vibali vya ajira  vinapotolewa na ikiwa wamekidhi sifa. (Alama 1.5). 

v. Waombaji wenye umri mkubwa (kati ya miaka 35 hadi 44) na waliokidhi vigezo.  (Alama 1). 

Hatua hiyo ilifatiwa na uchambuzi wa kina na jumla ya waombaji 1,605 walichaguliwa,  wanaume 921(57%) na wanawake 684(43%) kwa kutumia vigezo vya ziada vifuatavyo: i. Waombaji waliopata alama za juu kupitia vigezo vilivyoainishwa awali  wakati wa zoezi la uchambuzi. 

ii. Waombaji walioonesha nia ya kwenda kufanya kazi kwenye maeneo ya  vipaumbele yalioainishwa kwenye tangazo la kazi. 

iii. Waombaji wenye nia ya kwenda kufundisha katika Vyuo vya Afya. iv. Waombaji wanaojitolea katika Hospitali za Mikoa ya pembezoni. 

Nafasi 16 za Madaktari bingwa, hazikupata waombaji hivyo, nafasi hizo zitajazwa kwa  mujibu wa kanuni na sheria za ajira katika Utumishi wa Umma. 

Aidha, watumishi hawa waliochaguliwa wamepangiwa vituo vya kazi kwa kuzingatia  vigezo vifuatavyo: 

i. Uanzishwaji wa Hospitali mpya za Kanda Mtwara na Chato. 

ii. Ujenzi wa Hospitali za Rufaa za Mikoa.

Ukurasa wa 2 kati ya

iii. Upanuzi wa majengo mapya katika Hospitali za zamani (Sekou Toure (Mwanza),  Mawenzi (Kilimanjaro), Maweni (Kigoma), Mbeya Mkoa na Kanda, Kibongoto,  Mirembe (Dodoma). 

iv. Mahitaji ya watumishi wanaohitajika katika Hospitali mbalimbali za Kanda,  Maalumu na Mikoa ukilinganisha na wagonjwa wanaopata huduma. Hii ni pamoja  na upungufu wa watumishi katika vyuo vya Afya. 

v. Kuongezeka kwa vifaa tiba vya kisasa ambavyo vinahitaji wataalamu wa kuvitumia  vifaa hivyo. 

Mgawanyo wa watumishi kwa kila hospitali ni kama unavyoonekana katika jedwali hapa  chini;

NA 

Jina la Hospitali/Chuo/idara 

Idadi ya  

watumishi

ARUSHA AIR PORT 

1

BUKOBA LAKE PORT KAGERA 

1

CHIEF PHARMASIST DODOMA 

2

CHUO CHA MAABARA SINGIDA 

1

5

CHUO CHA MAAFISA AFYA MAZINGIRA WASAISIZI  MWANZA 

1

CHUO CHA MAAFISA TABIBU BAGAMOYO PWANI 

1

CHUO CHA MAAFISA TABIBU BUGANDO MWANZA 

1

CHUO CHA MAAFISA TABIBU GEITA 

2

CHUO CHA MAAFISA TABIBU KAHAMA SHINYANGA 

1

10 

CHUO CHA MAAFISA TABIBU KIGOMA 

3

11 

CHUO CHA MAAFISA TABIBU KILIMANJARO 

5

12 

CHUO CHA MAAFISA TABIBU KILOSA MOROGORO 

3

13 

CHUO CHA MAAFISA TABIBU KIOMBOI SINGIDA 

1

14 

CHUO CHA MAAFISA TABIBU LINDI 

3

15 

CHUO CHA MAAFISA TABIBU MAFINGA IRINGA 

4

16 

CHUO CHA MAAFISA TABIBU MASASI MTWARA 

3

17 

CHUO CHA MAAFISA TABIBU MASWA SIMIYU 

3

18 

CHUO CHA MAAFISA TABIBU MBEYA 

4

19 

CHUO CHA MAAFISA TABIBU MBOZI SONGWE 

2

20 

CHUO CHA MAAFISA TABIBU MBULU MANYARA 

2

21 

CHUO CHA MAAFISA TABIBU MIREMBE DODOMA 

1

22

CHUO CHA MAAFISA TABIBU MKOMAINDO  MTWARA 

1

23 

CHUO CHA MAAFISA TABIBU MOROGORO 

1

24 

CHUO CHA MAAFISA TABIBU MTWARA 

6



Ukurasa wa 3 kati ya

CHUO CHA MAAFISA TABIBU MUHIMBILI DAR ES  

25 

SALAAM 3

26 

CHUO CHA MAAFISA TABIBU MUSOMA MARA 

4

27 

CHUO CHA MAAFISA TABIBU NACHINGWEA LINDI 

2

28 

CHUO CHA MAAFISA TABIBU NEWALA MTWARA 

2

29 

CHUO CHA MAAFISA TABIBU NJOMBE 

2

30 

CHUO CHA MAAFISA TABIBU NZEGA TABORA 

2

31 

CHUO CHA MAAFISA TABIBU SAME KILIMANJARO 

2

32 

CHUO CHA MAAFISA TABIBU SONGEA RUVUMA 

3

33

CHUO CHA MAAFISA TABIBU SUMBAWANGA  RUKWA 

3

34 

CHUO CHA MAAFISA TABIBU TANGA 

6

35 

CHUO CHA MAAFISA TABIBU TARIME MARA 

2

36 

CHUO CHA MAAFISA TABIBU TUKUYU MBEYA 

2

37

VITUO VYA DAMU SALAMA (MTWARA, TABORA NA  DODOMA) 

41

38 

DAR ES SALAAM SEA PORT 

11

39 

DODOMA AIR PORT 

3

40 

HOLILI KILIMANJARO 

2

41 

HOROHORO TANGA 

2

42 

HOSPITALI YA AFYA YA AKILI MIREMBE 

38

43 

HOSPITALI YA MAGONJWA AMBUKIZI KIBONG'OTO 

44

44 

HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA CHATO 

86

45 

HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MTWARA 

112

46 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA 

11

47 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA BOMBO 

25

48 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA BUKOBA 

47

49 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA DODOMA 

11

50 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA GEITA 

53

51 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA IRINGA 

39

52 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA KATAVI 

73

53 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA KITETE 

39

54 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA LIGULA 

45

55 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA MANYARA 

53

56 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA MAWENI 

57

57 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA MAWENZI 

17

58 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA MBEYA 

26

59 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA MOROGORO 

9

60 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA MT. MERU 

9

62 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA MUSOMA 

59

63 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA MWANANYAMALA 

9

64 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA NJOMBE 

64

65

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA SEKOTOURE  MWANZA 

26



Ukurasa wa 4 kati ya

66 HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA SHINYANGA 38

67 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA SIMIYU 

77

68 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA SINGIDA 

41

69 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA SOKOINE 

46

70 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA SONGEA 

36

71 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA SONGWE 

67

72 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA SUMBAWANGA 

51

73 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA TEMEKE 

15

74 

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA TUMBI 

18

75 

IKOLA KATAVI 

2

76 

ISAKA SHINYANGA 

1

77 

ISONGOLE SONGWE 

1


78 JULIUS NYERERE AIR PORT DAR ES SALAAM 

18

79 

KABANGA KAGERA 

2

80 

KABWE KIGOMA 

1

81 

KAGEMU KAGERA 

2

82 

KASANGA RUKWA 

2

83 

KASESYA RUKWA 

1

84 

KASUMULU MBEYA 

1

85 

KCMC TATCOT KILIMANJARO 

5

86 

KIBONDO NTC KIGOMA 

4

87 

KIGOMA PORT 

2

88 

KIGOMA RRH 

3

89 

KILIMANJARO AIR PORT 

7

90 

KIRANDO KIGOMA 

2

91 

KONDOA NTC DODOMA 

1

92 

KOROGWE NTC TANGA 

2

93 

MANYOVU KIGOMA 

2

94 

MBAMBA BAY RUVUMA 

1

95

MOROGORO COLLEGE OF HEALTH AND ALLIED  SCIENCE 

4

96 

MPWAPWA ENVIRONMENTAL HEALTH DODOMA 

1

97 

MSAJILI BARAZA LA RADIOLOJIA DODOMA 

1

98 

MTWARA SEA PORT 

2

99

MUHIMBILI COLLEGE OF HEALTH AND ALLIED  SCIENCE DAR ES SALAAM 

2

100 

MURONGO KAGERA 

1

101 

MURUSAGAMBA KAGERA 

1

102 

MUSOMA AIR PORT MARA 

1

103 

MUTUKULA KAGERA 

1

104 

MWANZA AIR PORT 

1

105

MWANZA COLLEGE OF HEALTH AND ALLIED  SCIENCE 

1

106 

MWANZA PORT 

1



Ukurasa wa 5 kati ya

107 

MWANZA SCHOOL OF HEALTH AND ALLIED  

SCIENCE 3 


108 

NAMANGA ARUSHA 

1

109

NJOMBE COLLEGE OF HEALTH AND ALLIED  SCIENCE 

5

110

NJOMBE SCHOOL OF HEALTH AND ALLIED  SCIENCE 

2

111 

PHCI IRINGA 

4

112 

RUSUMO KAGERA 

1

113 

SINGIDA SCHOOL OF LABORATORY 

1

114 

SIRARI MARA 

3

115 

SONGWE AIR PORT 

1

116

TABORA COLLEGE OF HEALTH AND ALLIED  SCIENCE 

1

117

TABORA SCHOOL OF HEALTH AND ALLIED  SCIENCE 

3


118 TANGA SEA PORT 

2


119 TANGA VECTOR CONTROL 

1


120 TARAKEA KILIMANJARO 

2


121 TUNDUMA SONGWE 

4


122 WIZARA YA AFYA MAKAO MAKUU DODOMA 

10

123

WIZARA YA AFYA MAKAO MAKUU IDARA YA TIBA  DODOMA 

1


JUMLA 

1,605



Mgawanyo wa watumishi watakaopelekwa katika Hospitali za Kanda, Maalum, Mikoa,  Vyuo, Mipakani na Vituo vya Damu Salama vya Kanda ni kama ifutavyo;

NA 

KITUO 

IDADI

HOSPITALI ZA RUFAA ZA MIKOA 

1063

HOSPITALI ZA KANDA 

200

VYUO VYA AFYA 

118

VITUO VYA DAMU SALAMA VYA KANDA 

38

HOSPITALI MAALUM 

90

VITUO VYA MIPAKANI 

96



Ukurasa wa 6 kati ya

Sababu zilizochangia baadhi ya waombaji wengine kukosa ajira 

i. Baadhi ya waombaji wa ajira kutojaza kabisa au kutojaza kwa ukamilifu namba  za usajili zilizotolewa na Mabaraza yao hivyo kusababisha kushindwa  kutambuliwa. 

ii. Baadhi ya waombaji kufanya makosa ya kutumia namba za usajili za  wanataaluma wengine wanaotambulika na Baraza au kutumia namba za  mtahiniwa zilizotumika wakati wa mitihani ya Baraza au chuo. 

iii. Waombaji kuomba nafasi za ajira ambazo hawana sifa nazo. Mfano mwombaji  mwenye sifa ya Stashahada kuomba nafasi ya Shahada (Skills mismatch). iv. Wapo ambao hawakukidhi vigezo vya miuundo. 

Majina ya waombaji wote waliopangiwa vituo vya kazi yanapatikana katika Tovuti ya  Wizara ya Afya www.moh.go.tz.  

 Prof. Abel N. Makubi 

KATIBU MKUU WIZARA YA AFYA

Ukurasa wa 7 kati ya


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments