YANGA SC YATAWAZWA MABINGWA WA NBC




*************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

KLABU ya Yanga imefanikiwa kunyakuwa ubingwa wa ligi kuu Tanzania bara mara baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya timu ya Coastal Union.

Yanga Sc ilikuwa inahitaji pointi tatu ambazo zingeifanya isifikiwe na timu yoyote ile kwa michezo iliyosalia ya kigi kuu ya NBC.

Mabao ya Yanga yamewekwa kimyani na mshambuliaji wao Fiston Kalala Mayele ambaye alipachika mabao mawili na bao lingine likifungwa na Chiko Ushindi.

Mayeke sasa ataendelea kuongoza ufungaji bora akiwa na mabao 16 akifuatia na mshambuliaji wa Geita Gold George Mpole.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments