YANGA SC YAENDELEA KUTESA LIGI KUU NBC



*********

NA EMMANUEL MBATILO,DAR ES SALAAM

MABINGWA wa Ligi Kuu Tanzania Bara NBC, Yanga imeendelea kutoa dozi kwenye lihi hiyo baada ya leo kuichapa timu ya Polisi Tanzania kwa mabao 2-0 mchezo ambao ulipigwa kwenye dimba la Benjamini Mkapa Jijini Dar es Salaam.

Mchezo huo ambao ulikuwa wa 28 kwenye ligi hikiwa Yanga Sc ikicheza bila kupoteza mchezo wowote huku mshambuliaji wao Fiston Mayele akishindwa kupachika bao kwenye mchezo wa leo.

Mabao pekee ya Yanga yamewekwa kimyani na Feisal Salum "Fei Toto" pamoja na Chico Ushindi ambapo mabao yote yamefungwa kipindi cha kwanza.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments