YANGA SC RASMI YAKABIDHIWA KOMBE LAO, SHEREHE KUFANYIKA JUMAPILI HII DAR




*************

NA EMMANUEL MBATILO

KLABU ya Yanga leo imekabidhiwa kombe lao la Ligi Kuu Tanzania Bara NBC mara baada ya kutangazwa mabingwa wa ligi hiyo hivi karibuni.

Yanga Sc imekabidhiwa kombe hilo leo Sokoine mkoani Mbeya ambapo walikuwa wanacheza mchezo wao wa 29 bila kufungwa hivyo na kubakia na mechi moja wamalize ligi bila kufungwa.

Yanga Sc wamecheza na Mbeya City na kulazimishwa sare ya 1-1, mchezo ambao ulijawa na hisia za mashabiki ambao waliujaza uwanja huo kushuhudia Yanga ikikabidhiwa kombe hilo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments